< Mithali 19 >

1 Bora mtu masikini ambaye huenenda katika uadilifu wake kuliko mwenye ukaidi katika maneno yake na ni mpumbavu.
Mejor es el pobre que anda en su integridad, Que el de labios perversos y necio.
2 Tena, si vizuri kuwa na hamu bila maarifa na mwenye kukimbia haraka sana hukosea njia.
La persona sin conocimiento no es buena, Y el que se apresura con sus pies tropieza.
3 Upuuzi wa mtu unaharibu maisha yake na moyo wake hughadhabika dhidi ya Yehova.
La insensatez del hombre destruye su camino, Y luego su corazón se irrita contra Yavé.
4 Utajiri huongeza marafiki wengi, bali mtu masikini hutengwa na rafiki zake.
Las riquezas atraen muchos amigos, Pero el pobre es abandonado por su amigo.
5 Shahidi wa uongo hatakosa adhabu na mwenye kupumua uongo hataokoka.
El testigo falso no quedará impune, Y el que alienta mentiras no escapará.
6 Wengi wataomba fadhila kutoka kwa mtu mkarimu na kila mtu ni rafiki wa yule anayetoa zawadi.
Muchos buscan el favor del generoso, Y todos son amigos del hombre que da regalos.
7 Mtu masikini huchukiwa na ndugu zake wote; je marafiki wengi kiasi gani hujitenga kutoka kwake! Anawaita, lakini wameondoka.
Todos los hermanos del pobre lo aborrecen, ¡Cuánto más se alejarán de él sus amigos! Los persigue con palabras, pero ya no están.
8 Anayepata hekima huyapenda maisha yake mwenyewe; yeye atunzaye ufahamu atapata kilicho chema.
El que adquiere cordura se ama a sí mismo, Al que guarda la prudencia le irá bien.
9 Shahidi wa uongo hatakosa kuadhibiwa, bali mwenye kupumua uongo ataangamia.
El testigo falso no se irá sin castigo, Y el que alienta mentiras perecerá.
10 Haifai kwa mpumbavu kuishi kwa anasa- wala kwa mtumwa kutawala juu ya wafalme.
El lujo no conviene al insensato, ¡Cuánto menos al esclavo tener dominio sobre gobernantes!
11 Busara humfanya mtu achelewe kukasirika na utukufu wake ni kusamehe kosa.
La cordura del hombre detiene su furor, Y su honra es pasar por alto la ofensa.
12 Ghadhabu ya mfalme ni kama muungurumo wa simba kijana, bali fadhila yake ni kama umande kwenye majani.
Rugido de león es la amenaza del rey, Rocío sobre la hierba su favor.
13 Mwana mpumbavu ni uharibifu kwa baba yake na mke mgomvi ni maji yanayochuruzika daima.
El hijo necio es la ruina de su padre, Y gotera continua las contiendas de una esposa.
14 Nyumba na utajiri ni urithi kutoka kwa wazazi, bali mke mwenye busara hutoka kwa Yehova.
Casa y fortuna son herencia de los padres, Pero la esposa prudente es un regalo de Yavé.
15 Uvivu unamtupa mtu kwenye usingizi mzito, bali asiyetamani kufanya kazi atakwenda njaa.
La pereza produce un sueño profundo, Y la persona ociosa pasará hambre.
16 Yeye anayetii amri huyaongoza maisha yake, bali mtu asiyefikiri juu ya njia zake atakufa.
El que guarda el mandamiento, guarda su vida, Pero el que menosprecia sus caminos morirá.
17 Mwenye ukarimu kwa masikini humkopesha Yehova na atalipwa kwa kile alichofanya.
El que da al pobre presta a Yavé, Y Él le dará su recompensa.
18 Mrudi mwanao wakati kuna matumaini na usiwe na shauku ya kumweka katika mauti.
Corrige a tu hijo mientras haya esperanza, Pero no se exceda tu alma para destruirlo.
19 Mtu mwenye hasira kali lazima alipe adhabu; kama ukimwokoa, utafanya hivyo mara mbili.
El hombre de gran ira sufrirá castigo, Pero si lo perdonas, lo tendrá que aumentar.
20 Sikiliza ushauri na ukubali maelekezo, ili uweze kuwa na hekima mwishoni mwa maisha yako.
Escucha el consejo y acepta la corrección Para que seas sabio.
21 Moyoni mwa mtu kuna mipango mingi, bali kusudi la Yehova ndilo litakalo simama.
Muchos designios hay en el corazón del hombre, Pero el propósito de Yavé es el que prevalece.
22 Shauku ya mtu ni uaminifu na mtu masikini ni bora kuliko muongo.
Lo que los hombres aprecian es la lealtad: Es preferible ser pobre que engañador.
23 Kumheshimu Yehova huwaelekeza watu kwenye uzima; mwenye nayo atashibishwa na hatadhurika kwa madhara.
El temor a Yavé es para vida, El que lo tiene vivirá satisfecho, Y no será visitado por el mal.
24 Mtu goigoi huuzika mkono wake ndani ya dishi; hataurudisha juu ya kinywa chake.
El perezoso mete la mano en el plato, Pero ni aun a su boca lo llevará.
25 Kama utampiga mwenye mzaha, wajinga watakuwa na hekima; mwelekeze mwenye ufahamu, naye atapata maarifa.
Golpea al burlador, y el ingenuo será prudente, Corrige al entendido, y aumentará su saber.
26 Anayempora baba yake na kumfukuza mama yake ni mwana anayeleta aibu na shutuma.
El que roba a su padre y echa fuera a su madre Es hijo que trae vergüenza y deshonra.
27 Mwanangu, kama utaacha kusikiliza maelekezo, utapotea kutoka kwenye maneno ya maarifa.
Hijo mío, deja de oír consejos Que te apartan de las palabras de sabiduría.
28 Shahidi mpotofu huidhihaki haki na kinywa cha waovu humeza uovu.
El testigo perverso se burla de la justicia, Y la boca de los impíos encubre la iniquidad.
29 Hukumu ipo tayari kwa wenye dhihaka na mjeledi kwa migongo ya wapumbavu.
Hay castigos preparados para los burladores, Y azotes para la espalda del necio.

< Mithali 19 >