< Hesabu 9 >

1 BWANA akanena na Musa katika katika jangwa la Sinai, mwezi wa kwanza wa mwaka wa pili baada ya kutoka katika nci ya Misri. Akasema,
Adonai spoke to Moses [Drawn out] in the wilderness of Sinai [Thorn], in the first month of the second year after they had come out of the land of Egypt [Abode of slavery], saying,
2 “Wana wa Israeli wataikumbuka Pasaka katika wakati wake kila mwaka.
“Moreover let the children of Israel [God prevails] keep the Pesac ·Passover· in its appointed season.
3 Siku ya kumi na nne ya mwezi huu, muda wa jioni, utaikumbuka Pasaka kila mwaka kwa muda uliopanggwa. Lazima uikumbuke, fuata taratibu zake zote na utii sheria zake zote zinazohusiana na tukio hilo.
On the fourteenth day of this month, at evening, you shall keep it in its appointed season— according to all its statutes, and according to all its judgments, you shall keep it.”
4 Kwa hiyo, Musa akawaambia wana wa Isareli kuwa wataishika sikukuu ya Pasaka.
Moses [Drawn out] spoke to the children of Israel [God prevails], that they should keep the Pesac ·Passover·.
5 Kwa hiyo wakaishika sikuu ya Pasaka katika mwezi wa kwanza, wakati wa jioni wa siku ya kumi na nne ya mwezi katika jangwa la Sinai. Wana wa Israeli walitii kila kitu ambacho BWANA alimwamuru Musa kukifanya.
They kept the Pesac ·Passover· in the first month, on the fourteenth day of the month, at evening, in the wilderness of Sinai [Thorn]. According to all that Adonai enjoined Moses [Drawn out], so the children of Israel [God prevails] did.
6 Kulikuwa na watu fulani walionajisika kwa sababu ya maiti ya mtu. Hawakuweza kuishika Pasaka siku hiyo. Kwa hiyo walikwenda kwa Musa na Haruni siku hiyohiyo.
There were certain men, who were unclean because of the dead body of a man, so that they could not keep the Pesac ·Passover· on that day, and they came before Moses [Drawn out] and before Aaron [Light-bringer] on that day.
7 Wakamwambia Musa, “Sisi tumenajisika kwa sababu ya maiti ya mtu. Kwa nini basi unatutaka tuendelee kutoa sadaka kwa BWANA kwa wakati wa mwaka uliopangwa kwa wana wa Israeli?”
Those men said to him, “We are unclean because of the dead body of a man. Why are we kept back, that we may not offer the offering of Adonai in its appointed season among the children of Israel [God prevails]?”
8 Naye Musa akawaambia, “Subirini nimsikilize BWANA ataniambia nini juu Yenu.”
Moses [Drawn out] answered them, “Wait, that I may sh'ma ·hear obey· what Adonai will enjoin concerning you.”
9 BWANA akanena na Musa, akamwambia,
Adonai spoke to Moses [Drawn out], saying,
10 “Nena na wana wa Israeli, uwaambie, 'kama mmoja wenu au mwana wa uzao wenu amenajisika kwa sababu ya maiti, au ana safari ndefu, bado anaweza kuishika Pasaka ya BWANA.
“Say to the children of Israel [God prevails], ‘If any man of you or of your generations is unclean by reason of a dead body, or is on a journey far away, he shall still keep the Pesac ·Passover· to Adonai.
11 Wataishika Pasaka siku ya kumi na nne ya mwezi wa pili wakati wa jioni. Wataila kwa mikate isyotiwa chahcu na mboga chungu.
In the second month, on the fourteenth day at evening they shall keep it; they shall eat it with matzah ·unleavened bread· and bitter herbs.
12 Wasiiache mpaka jioni, au kuvunja mifupa yake. Watafuata taratibu zote za Pasaka.
They shall leave none of it until the morning, nor break a bone of it. According to all the statute of the Pesac ·Passover· they shall keep it.
13 Lakini mtu yeyote asiye najisi na hayuko safarini, na akashindwa kuishika Pasaka, huyo mtu lazima aondolewe kati ya watu wake kwa sababu hakutoa sadaka ambayo BWANA huitaka kwa wakati wa mwaka uliopangwa. Huyo mtu lazima aibebe dhambi yake.
But the man who is clean, and is not on a journey, and fails to keep the Pesac ·Passover·, that soul shall be cut off from his people. Because he didn’t offer the offering of Adonai in its appointed season, that man shall bear his sin.
14 Kama mtu mgeni anayeishi kati yenu na akaishika, Pasaka kwa heshima ya BWANA, ataishika na kufanya amri zote, na kutii taratibu zake. Utakuwa na sheria hizohizo kwa wageni na kwa wote waliaozaliwa katika nchi.
“‘If a foreigner lives among you, and desires to keep the Pesac ·Passover· to Adonai; according to the statute of the Passover, and according to its ordinance, so shall he do. You shall have one statute, both for the foreigner, and for him who is born in the land.’”
15 Na siku hiyo ambayo masikani iliposimamishwa, wingu lilifunika masikani, ile hema ya amari ya agano. Ilipokuwa jioni wingu lilkuwa juu ya masikani. Lilionekana kama moto mpaka asubuhi.
On the day that the tabernacle was raised up, the cloud covered the tabernacle, even the Tent of the Testimony: and at evening it was over the tabernacle as it were the appearance of fire, until morning.
16 Liliendelea hivyohivyo. Lile wingu lilifunika masikani na kuonekana kama moto wakati wa usiku.
So it was continually. The cloud covered it, and the appearance of fire by night.
17 Na kila wingu lilipochukuliwa kutoka kwenye hema, wana wa Isareli waliendelea na safari yao. Na kila wingu liliposimama, watu waliweka kambi.
Whenever the cloud was taken up from over the Tent, then after that the children of Israel [God prevails] traveled; and in the place where the cloud remained, there the children of Israel [God prevails] encamped.
18 Wana wa Israrli walisafiri kwa amri ya BWANA, na kwa amri yake waliweka kambi. Wakati wingu liliposimama juu ya masikani, nao walikaa kwenye kambi zao.
At the order of Adonai, the children of Israel [God prevails] traveled, and at the order of Adonai they encamped. As long as the cloud remained on the tabernacle they remained encamped.
19 Na wingu lilipobaki kwenye masikani kwa siku nyingi, wana wa Israeli walitakiwa kutii maelekezo ya BWANA na kusitisha safari yao.
When the cloud stayed on the tabernacle many days, then the children of Israel [God prevails] kept Adonai’s charge, and didn’t travel.
20 Wakati mwingine wingu lilibaki kwa siku chache tu kwenye masikani. Kwa mazingira kama hayo walilazimika kutii amri ya BWANA - waliweka kambi na kisha kuendelea na safari tena kwa amri yake.
Sometimes the cloud was a few days on the tabernacle; then according to the order of Adonai they remained encamped, and according to the order of Adonai they traveled.
21 Wakati mwingine wingu lilikuwepo kambini kuanzia jioni mpaka asubuhi. Na wingu liliponyanyuliwa asubuhi, walisafiri. Kama liliendelea kwa mchana wote na kwa usiku wote, ni pale tu wingu liliponyanyuliwa ndipo walipoendelea na safari.
Sometimes the cloud was from evening until morning; and when the cloud was taken up in the morning, they traveled: or by day and by night, when the cloud was taken up, they traveled.
22 Hata kama wingu lilibaki kwenye masikini kwa siku mbili, kwa mwezi mmoja, au kwa mwaka mmoja, ili mradi tu limebaki pale, wana wa Israeli walibaki kwenye kambi zao na kusitisha safari. Lakini pale wingu liliponyanyuliwa, walianza safari yao.
Whether it was two days, or a month, or a year that the cloud stayed on the tabernacle, remaining on it, the children of Israel [God prevails] remained encamped, and didn’t travel; but when it was taken up, they traveled.
23 Walifanya kambi kwa amri ya BWANA, na walisafiri kwa amri yake. Walitii amri ya BWANA iliyotolewa kupitia kwa Musa
At the order of Adonai they encamped, and at the order of Adonai they traveled. They did what Adonai charged them to do through Moses [Drawn out].

< Hesabu 9 >