< Hesabu 10 >

1 BWANA alinena na Musa, akasema,
Adonai spoke to Moses [Drawn out], saying,
2 “tengenza tarumbeta mbili za fedha. Uzitengeneze kwa kufua hizo fedha. Utazitumia hizo tarumbeta kwa kuwaita watu waje pamoja na kwa kuwaita watu wote wakati wa kuondoka kwenye kambi zao.
“Make two trumpets of silver. You shall make them of beaten work. You shall use them for the calling of the congregation, and for the journeying of the camps.
3 Makuhani watapiga tarumbeta kwa ajili ya kuwaita watu wote mbele yako kwenye lango la hema ya kukutania.
When they blow them, all the congregation shall gather themselves to you at the door of the Tent of Meeting.
4 Kama makuhani watapiga tarumbeta moja tu, basi viongozi, vichwa koo za Israeli ndipo watakapokutana kwako.
If they blow just one, then the princes, the heads of the thousands of Israel [God prevails], shall gather themselves to you.
5 Utakapopiga tarumbeta ya sauti kuu, ile kambi ya upande wa mashariki itaanza kusafiri.
When you blow an alarm, the camps that lie on the east side shall go forward.
6 Nawe utakapopiga tarumeta kwa sauti kuu mara ya pili, ile kambi ya upande wa kusini wataanza kusafiri. Watapiga tarumbeta kwa sauti kuu ili kuanza safari yao.
When you blow an alarm the second time, the camps that lie on the south side shall go forward. They shall blow an alarm for their journeys.
7 Watu wote watakapokutana pamoja, piga hizo tarumbeta lakini si kwa sauti kuu.
But when the assembly is to be gathered together, you shall blow, but you shall not sound an alarm.
8 Wana wa Haruni, makuhani, watapiga hizo tarumbeta. Huu ndio utakaokuwa utaratibu wa watu wako kwa vizazi vyote.
“The sons of Aaron [Light-bringer], the priests, shall blow the trumpets. This shall be to you for a statute forever throughout all your generations.
9 Nanyi mtakapoenda vitani katika ardhi yenu dhidi ya maadui wenu wanaowakandamiza, ndipo mtakapotoa ishara ya sauti ya tarumbeta. Mimi, BWANA Mungu wako nitawaita kuwakumbuka na kuwaokoa kutoka kwa maadui wenu.
When you go to war in your land against the adversary who oppresses you, then you shall sound an alarm with the trumpets. Then you will be remembered before Adonai your God, and you will be saved from your enemies.
10 Pia, wakati wa kusherehekea, sikukuu zenu za kawaida na katika miandamo ya miezi, mtapiga tarumbeta zenu kwa heshima ya sadaka zenu za kuteketezwa na kwa sadaka zenu za amani. Huu utakuwa ukumbusho wenu kwangu, Mungu wenu. Mimi ndimi BWANA Mungu wenu.”
“Also in the day of your gladness, and in your set feasts, and in the beginnings of your months, you shall blow the trumpets over your burnt offerings, and over the sacrifices of your peace offerings; and they shall be to you for a memorial before your God. I am Adonai your God.”
11 Katika siku ya ishrini, mwezi wa pili, mwaka wa pili, Lile wingu liliinuliwa toka masikani ya amri za maagano.
In the second year, in the second month, on the twentieth day of the month, the cloud was taken up from over the tabernacle of the testimony.
12 Wana wa Israeli wakaendelea na safari yao toka jangwa la Sinai. Lile wingu likasimama kwenye jangwa la Parani.
The children of Israel [God prevails] went forward according to their journeys out of the wilderness of Sinai [Thorn]; and the cloud stayed in the wilderness of Paran.
13 Walifanya safari yao ya kwanza, kufuatia amri ya BWANA iliyotolewa kupitia kwa Musa.
They first went forward according to the order of Adonai through Moses [Drawn out].
14 Kambi ya mahali pa uzao wa Yuda iliondoka ya kanza, wakiondoa majeshi yao binafsi. Nashoni mwana wa Aminadabu ndiye aliyeongoza jeshi la Yuda.
First, the standard of the camp of the children of Judah [Praised] went forward according to their armies. Nahshon the son of Amminadab was over his army.
15 Nethaneli mwana wa Zuari aliongoza jeshi la kabila la uzao wa Isakari.
Nethanel the son of Zuar was over the army of the tribe of the children of Issachar [Hire, Reward].
16 Eliabu mwana wa Heloni aliongoza jeshi la kabila la Zabuloni.
Eliab the son of Helon was over the army of the tribe of the children of Zebulun [Living together].
17 Uzao wa Gerishoni na Merari, ambao walitunza masikani, na kuanza kusafiri.
The tabernacle was taken down; and the sons of Gershon and the sons of Merari, who bore the tabernacle, went forward.
18 Baadaye Walifuata jeshi la mahali pa kambi ya Reubeni walianza safari yao. Elizuri mwana wa Shedeuri alliongoza jeshi la Reubebni.
The standard of the camp of Reuben [See, a son!] went forward according to their armies. Elizur the son of Shedeur was over his army.
19 Shelumieli mwana wa Zurishadai aliliongoza jeshi la kabila la uzao wa Simeoni.
Shelumiel the son of Zurishaddai [My rock almighty] was over the army of the tribe of the children of Simeon [Hearing].
20 Eliasafu mwana Deuli aliliongoza jeshi la kabila la uzao wa Gadi.
Eliasaph the son of Deuel was over the army of the tribe of the children of Gad [Good fortune].
21 Kabila la Kohathi nalo lilianza safari. Wao walibebba vyombo vya mahali patakatifu. Wengine waliisimamisha masikani kabla ya Wakohathi kufika kambi inayofuata.
The Kohathites set forward, bearing the sanctuary. The others set up the tabernacle before they arrived.
22 Majeshi ya kabila la uzao wa Efraimu ndio waliofuata. Elishama mwana wa Amihudi ndiye aliyeongoza jeshi la Efraimu.
The standard of the camp of the children of Ephraim [Fruit] set forward according to their armies. Elishama the son of Ammihud was over his army.
23 Gamalieli mwana wa Pedazuri aliongoza jeshi la uzao wa Manase.
Gamaliel the son of Pedahzur was over the army of the tribe of the children of Manasseh [Causing to forget].
24 Abidani mwana wa Gidioni aliongoza jeshi la uzao wa kabila la Benjamini.
Abidan the son of Gideoni was over the army of the tribe of the children of Benjamin [Son of right hand, Son of south].
25 Lile jeshi lililoweka kambi mahali pa bango la uzao wa Dani lilikuwa la mwisho kuondoka. Ahizeri mwana wa Amishadai ndiye aliyeongoza jeshi la Dani.
The standard of the camp of the children of Dan [He judged], which was the rear guard of all the camps, set forward according to their armies. Ahiezer the son of Ammishaddai was over his army.
26 Pagieli mwana wa Okirani aliongoza jeshi la wana wa uzao wa Asheri.
Pagiel the son of Ochran was over the army of the tribe of the children of Asher [Happy].
27 Ahira mwana wa Enani aliongoza jeshi la uzao wa kabila ya Naftali.
Ahira the son of Enan was over the army of the tribe of the children of Naphtali [My wrestling].
28 Hivi ndivyo majeshi ya wana wa Israeli yalivyosafiri.
Thus were the travels of the children of Israel [God prevails] according to their armies; and they went forward.
29 Musa alinena na Hobibu mwana wa Reueli wa Kabila la Midiani. Reueli alikuwa baba mke wa Musa. Musa akanena na Hobibu akasema, “Tunasafiri kuelekea mahali ambapo BWANA ametuahidi. BWANA alisema kuwa, “Nitawapeni ninyi hilo eneo, 'Njoni pamoja nasi na tutawatendea mema. BWANA ameahidi kuwafanyia mema Waisraeli.”
Moses [Drawn out] said to Hobab, the son of Reuel the Midianite [Descendant of Strife], Moses [Drawn out]’ father-in-law, “We are journeying to the place of which Adonai said, ‘I will give it to you.’ Come with us, and we will treat you well; for Adonai has spoken good concerning Israel [God prevails].”
30 Lakini Hobibu akmwambia Musa, “Sitaambatana nanyi.”
He said to him, “I will not go; but I will depart to my own land, and to my relatives.”
31 Naye Musa akamjibu, “Tafadhali msituache. Mnajua jinsi ilivyo kuweka kambi jangwani. Tunaomba mtujali.
He said, “Don’t leave us, please; because you know how we are to encamp in the wilderness, and you can be our eyes.
32 Kama mtaambatana nasi tutawatendea mema sawa na jinsi BWANA anavyotutendea.”
It shall be, if you go with us, yes, it shall be, that whatever good Adonai does to us, we will do the same to you.”
33 Walisafiri kutoka mlima wa BWANA kwa siku tatu. Sanduku la agano la BWANA liliwatangulia kwa siku tatu ili kupata mahali pa kupumzika.
They set forward from the Mount of Adonai three days’ journey. The ark of Adonai’s covenant went before them three days’ journey, to seek out a resting place for them.
34 Wingu la BWANA lilikuwa juu yao muda wote wa mchana walipokuwa safarini.
The cloud of Adonai was over them by day, when they set forward from the camp.
35 Kila hilo sanduku liliposafiri kwenda mbele, Musa alisema, “Inuka BWANA, Uwatawanye maadui wako. Uwafanye wale wanaokuchukia kukukimbia.”
When the ark went forward, Moses [Drawn out] said, “Rise up, Adonai, and let your enemies be scattered! Let those who hate you flee before you!”
36 Na kila lile sanduku liliposimama, Musa alisema, “BWANA uwarudie, hawa Waisraeli makumi elfu.”
When it rested, he said, “Teshuvah ·Completely return·, Adonai, to the ten thousands of the thousands of Israel [God prevails].”

< Hesabu 10 >