< Hesabu 35 >

1 BWANA akanena na Musa kwenye nyanda za Moabu karibu na Yorodani kule Yeriko akasema,
And the LORD spoke unto Moses in the plains of Moab by the Jordan at Jericho, saying:
2 “Waamuru watu wa Israeli kutoa sehemu ya urithi wa ardhi yao kwa Walawi. Watawapa miji ya kuishi ndani yake na eneo la malisho kuzunguka miji hiyo.
'Command the children of Israel, that they give unto the Levites of the inheritance of their possession cities to dwell in; and open land round about the cities shall ye give unto the Levites.
3 Walawi watakuwa na miji hiyo ya kuishi. Eneo la malisho litakuwa kwa ajili ya ng'ombe zao, kondoo zao, na wanyama wao wote.
And the cities shall they have to dwell in; and their open land shall be for their cattle, and for their substance, and for all their beasts.
4 Hayo malisho yatakayozunguka miji hiyo ambayo mtawapa Walawi yataanzia kwenye maboma kwa ukubwa wa “mita 457” kila upande.
And the open land about the cities, which ye shall give unto the Levites, shall be from the wall of the city and outward a thousand cubits round about.
5 Utapima dhiraa elfu mbili kutoka nje ya mji kuelekea mashariki, na dhiraa elfu mbili kuelekea kusini, na dhiraa elfu mbili kuelekea upande wa magharibi, na dhiraa elfu mbilii kuelekea upandewa kaskazini. Haya yatakuwa maeneo ya malisho yao. Miji itakuwa katikati.
And ye shall measure without the city for the east side two thousand cubits, and for the south side two thousand cubits, and for the west side two thousand cubits, and for the north side two thousand cubits, the city being in the midst. This shall be to them the open land about the cities.
6 Katika hiyo miji sita mtakayowapatia Walawi itatumika kama miji ya ukimbizi. Mtatoa maeneo haya ili kama mtu ameua mtu apate mahali pa kukimbilia. Pia mtatoa miji mingine arobaini na mbli.
And the cities which ye shall give unto the Levites, they shall be the six cities of refuge, which ye shall give for the manslayer to flee thither; and beside them ye shall give forty and two cities.
7 Jumla ya miji ambyo mtawapa Walawi itakuwa arobaini na nane. Mtawapa hiyo miji pamoja na maeneo yao ya malisho.
All the cities which ye shall give to the Levites shall be forty and eight cities: them shall ye give with the open land about them.
8 Zile kabila kubwa za watu wa Israeli, kabila ambalo lina ardhi zaidi, watatoa ardhi zaidi. Makabila madogo madogo watatoa miji michache. Kila kabila lazima watoe kwa ajili ya Walawi kwa kufuata mgawo waliopata.”
And concerning the cities which ye shall give of the possession of the children of Israel, from the many ye shall take many, and from the few ye shall take few; each tribe according to its inheritance which it inheriteth shall give of its cities unto the Levites.'
9 Kisha BWANA akanena na Musa akamwambia,
And the LORD spoke unto Moses, saying:
10 “Sema na wana wa Israeli na uwaambie, 'Mtakapovuka Yorodani kuingia Kanaani,
'Speak unto the children of Israel, and say unto them: When ye pass over the Jordan into the land of Canaan,
11 Kisha mchague miji itakayotumika kama miji ya ukimbizi kwa, ajili yenu, mahali ambapo mtu aliyeua mtu pasipo kukusudia anaweza kukimbilia.
then ye shall appoint you cities to be cities of refuge for you, that the manslayer that killeth any person through error may flee thither.
12 Hii miji itakuwa kwenu miji ya ukimbizi kwa mtu anayetaka kulipa kisasi. ili kwamba mtuhumiwa asije akauawa bila kwanza kusikilizwa na jamii.
And the cities shall be unto you for refuge from the avenger, that the manslayer die not, until he stand before the congregation for judgment.
13 Mtachagua miji sita kuwa miji ya ukimbizi.
And as to the cities which ye shall give, there shall be for you six cities of refuge.
14 Mtatoa miji mitatu kule ng'ambo ya Yorodani na miji mitatu huko Kanaani. Itakuwa miji ya ukimbizi.
Ye shall give three cities beyond the Jordan, and three cities shall ye give in the land of Canaan; they shall be cities of refuge.
15 Kwa ajili ya watu wa Israeli, wageni, kwa, yeyote anayeishi kati yenu, hii miji sita itatumika kama miji ya ukimbizi kwa mtu yeyote atakayeua mtu bila kukusudia anaweza kukimbila.
For the children of Israel, and for the stranger and for the settler among them, shall these six cities be for refuge, that every one that killeth any person through error may flee thither.
16 Lakini kama mtuhumiwa amempiga mtu na chombo cha chuma, na huyo mtu akafa, basi kwa hakika yule mtuhumiwa ni muuaji. Kwa hiyo anatakiwa kuuawa.
But if he smote him with an instrument of iron, so that he died, he is a murderer; the murderer shall surely be put to death.
17 Kama yule mtuhumiwa amempiga mtu kwa jiwe mkonono mwake ambalo linaweza kumwua mtu, na kama yule mtu atakufa, basi hakika huyo mtuhumiwa ni mwuaji. Kwa hakika anatakiwa kuuawa.
And if he smote him with a stone in the hand, whereby a man may die, and he died, he is a murderer; the murderer shall surely be put to death.
18 Kama mtuhumiwa amempiga mtu kwa silaha ya mti ambayo inaweza kuua mtu na kama huyo mtu atakufa, basi kwa hakika huyo mtuhumiwa ni mwuaji. kwa hakika huyo anataikwa kuuawa.
Or if he smote him with a weapon of wood in the hand, whereby a man may die, and he died, he is a murderer; the murderer shall surely be put to death.
19 Mwenye kulipa kisasi cha damu ndiye atakayemwua mwuaji. atkapokutana naye, anaweza kumwua.
The avenger of blood shall himself put the murderer to death; when he meeteth him, he shall put him to death.
20 Lakini kama yule mtuhumiwa atamshinda mtu yeyote yule anayemchukia au kama atamtupia kitu, wakati akimvizia, kiasi kwamba huyo mtu akafa,
And if he thrust him of hatred, or hurled at him any thing, lying in wait, so that he died;
21 au kama atampiga ngumi kwa chuki na mtu huyo akafa, ndipo yule mtuhumiwa aliyempiga hakika atauawa. Yeye ni mwuaji. Yule mlipa kisasi cha damu anaweza kumwua muuaji pale atakapokutana naye.
or in enmity smote him with his hand, that he died; he that smote him shall surely be put to death: he is a murderer; the avenger of blood shall put the murderer to death when he meeteth him.
22 Lakini kama mtuhumiwa atampiga mtu ghafla bila kuwa na chuki hapo awali, au kama atamtupia kitu ambacho kitampiga mtu bila kumvizia
But if he thrust him suddenly without enmity, or hurled upon him any thing without lying in wait,
23 au kama atatupa jiwe amabalo linaweza kumwua mtu bila kumwona, basi huyo mtu hakua adui yake, hakukusudia kumwumiza huyo mtu. Basi hiki ndicho kitachofanywa kama mtu huyo atakufa.
or with any stone, whereby a man may die, seeing him not, and cast it upon him, so that he died, and he was not his enemy, neither sought his harm;
24 Kwa tatizo la jinsi hiyo, Watu wataamua kati ya mlipa kisasi na mtuhumiwa kwa kufuata taratibu zifuatazo.
then the congregation shall judge between the smiter and the avenger of blood according to these ordinances;
25 Watu watamwokoa mtuhumiwa kutoka kwenye nguvu za mlipa kisasi cha damu. Watu watamrudisha mtuhumiwa katika mji wa ukimbizi ambao hapo awali alikimbilia. Ataishi pale mpaka yule kuhani anayetumikia atakapokufa, ambaye alipakwa mafuta matakatifu.
and the congregation shall deliver the manslayer out of the hand of the avenger of blood, and the congregation shall restore him to his city of refuge, whither he was fled; and he shall dwell therein until the death of the high priest, who was anointed with the holy oil.
26 Lakini kama yule mtuhumiwa muda fulani ataenda nje ya mipaka ya mji a ukimbizi ambao alikimbilia,
But if the manslayer shall at any time go beyond the border of his city of refuge, whither he fleeth;
27 na kama yule mlipa kisasi cha damu atamwona nje ya mipaka ya mji wake wa ukimbizi, kama atamwua huyo mtuhumiwa, mlipa kisasi cha damu hatakuwa na hatia ya mauaji hayo.
and the avenger of blood find him without the border of his city of refuge, and the avenger of blood slay the manslayer; there shall be no bloodguiltiness for him;
28 Hii ni kwa sababu yule mtuhumiwa alitakiwa kubaki katika mji wake wa ukimbizi mpaka kuhani mkuu atakapokufa. Baada ya kifo cha kuhani mkuu, yule mtuhumiwa atarejea kwenye nchi yake ambako kuna mali yake.
because he must remain in his city of refuge until the death of the high priest; but after the death of the high priest the manslayer may return into the land of his possession.
29 Hizi amri zitakuwa maagizo kwenu kwa kizazi chote mahali kote mnakoishi.
And these things shall be for a statute of judgment unto you throughout your generations in all your dwellings.
30 Yeyote amwuaye mtu, mwuaji atauawa, kama neno la ushahidi litakavyotolewa. Lakini ushahidi wa mtu mmoja unaweza usitoshe kusababisha mtu kuuawa.
Whoso killeth any person, the murderer shall be slain at the mouth of witnesses; but one witness shall not testify against any person that he die.
31 Pia, msipokee fidia kwa ajili ya uhai wa mwuaji ambaye ana hatia ya mauti. Kwa hakika lazima auawe.
Moreover ye shall take no ransom for the life of a murderer, that is guilty of death; but he shall surely be put to death.
32 Na msipokee fidia ya mtu aliyekimbilia kwenye miji ya ukimbizi. Msimruhusu kwa namna yeyote kurudi kwenye mali zake mpaka pale kuhani mkuu atakapokufa.
And ye shall take no ransom for him that is fled to his city of refuge, that he should come again to dwell in the land, until the death of the priest.
33 Msiiharibu nchi mnayokaa kwa namna hii, kwa kuwa damu ya mwuaji huharibu nchi. Hakuna sadaka ya upatanisho inayoweza kufanywa kwa nchi pale damu inapomwagika juu yake, isipokuwa kwa damu ya mtu aliyeimwaga.
So ye shall not pollute the land wherein ye are; for blood, it polluteth the land; and no expiation can be made for the land for the blood that is shed therein, but by the blood of him that shed it.
34 Kwa hiyo msiinajisi nchi mnayoishi kwa sababu Mimi ninaishi ndani yake. Mimi BWANA huishi kati ya watu wa Israeli.”'
And thou shalt not defile the land which ye inhabit, in the midst of which I dwell; for I the LORD dwell in the midst of the children of Israel.'

< Hesabu 35 >