< Hesabu 34 >

1 BWANA akanena na Musa akasema,
And the LORD spoke unto Moses, saying:
2 “Waamuru watu wa Israeli na uwaambie, 'Mtakapoingia katika nchi ya Kanaani, nchi ambayo itakuwa mali yenu, nchi ya Kanaani na mipaka yake, mpaka wenu wa kusini utaendelea kutoka nyika ya Sini hadi mpaka wa Edomu.
'Command the children of Israel, and say unto them: When ye come into the land of Canaan, this shall be the land that shall fall unto you for an inheritance, even the land of Canaan according to the borders thereof.
3 Mwisho wa mpaka wa kusini utakuwa mwisho wa bahari ya chumvi kuelekea mashariki.
Thus your south side shall be from the wilderness of Zin close by the side of Edom, and your south border shall begin at the end of the Salt Sea eastward;
4 Mpaka wenu utageukia kusini kutoka mlima kuelekea Akrabimu na kupitia nyika ya Sini. na kutokea huko utaelelkea kusini mwa Kadeshi Barinea na kuelekea Hazari Adari mpaka Azimoni.
and your border shall turn about southward of the ascent of Akrabbim, and pass along to Zin; and the goings out thereof shall be southward of Kadesh-barnea; and it shall go forth to Hazar-addar, and pass along to Azmon;
5 Kutoka huko, mpaka utageuka kutoka Azimoni kuelekea kijito cha Misri na kukifuata mpaka baharini.
and the border shall turn about from Azmon unto the Brook of Egypt, and the goings out thereof shall be at the Sea.
6 Mpaka wa Magharibi utakuwa pwani ya bahari kuu. Huu ndio utakuwa mpaka wenuwa Magharibi.
And for the western border, ye shall have the Great Sea for a border; this shall be your west border.
7 Mpaka wenu wa kaskazini utaanzia kwenye bahari kuu hadi Mlima Hori,
And this shall be your north border: from the Great Sea ye shall mark out your line unto mount Hor;
8 kisha kutoka Mlima Hori hadi Lebo Hamathi, kisha Zedadi.
from mount Hor ye shall mark out a line unto the entrance to Hamath; and the goings out of the border shall be at Zedad;
9 Mpaka utaendelea hadi Zifroni na kuishia Hazari Enani. Huu ndio utakuwa mpaka wenu wa kaskazini.
and the border shall go forth to Ziphron, and the goings out thereof shall be at Hazar-enan; this shall be your north border.
10 Kisha mtaweka alama za mpaka wenu wa mashariki ambao utaanzia Hazari Enani kuelekea kusini Shefamu.
And ye shall mark out your line for the east border from Hazar-enan to Shepham;
11 Kisha mpaka wa kusini utaendelea kutoka Shefamu hadi Ribla, upande wa masharikia mwa Aini. Mpaka utaedelea upande huo wa mashariki hadi upande wa mashariki wa bahari ya Kinerethi.
and the border shall go down from Shepham to Riblah, on the east side of Ain; and the border shall go down, and shall strike upon the slope of the sea of Chinnereth eastward;
12 Kisha mpaka utaendelea kuelekea kusini hadi mto Yorodani na hadi bahari ya chumvi. Hii ndiyo itakuwa nchi yenu, kwa kuifuata mipaka yake yote inayozunguka.'”
and the border shall go down to the Jordan, and the goings out thereof shall be at the Salt Sea; this shall be your land according to the borders thereof round about.'
13 Kisha Musa akawaamuru watu wa Israeli akasema, “Hii ndiyo nchi ambayo mtaipokes kwa kura, ambayo BWANA ameamuru kuwapa wale makabila tisa na nusu.
And Moses commanded the children of Israel, saying: 'This is the land wherein ye shall receive inheritance by lot, which the LORD hath commanded to give unto the nine tribes, and to the half-tribe;
14 Kabila ya uzao wa Reubeni, kwa kufuata jinsi walivyopewa urithi kwa jamaa ya kabila yao, na uzao wa kabila la Gadi, kwa kufuata jinsi walivyopewa urithi kwa jamaa ya kabila yao, na nusu ya Manase wamepata ardhi yao.
for the tribe of the children of Reuben according to their fathers' houses, and the tribe of the children of Gad according to their fathers' houses, have received, and the half-tribe of Manasseh have received, their inheritance;
15 Wale makabila mawili na nusu wameshapata mgawo wao ng'ambo ya mto Yorodani upande wa mashariki, kuelekea kule linakotokea jua.”
the two tribes and the half-tribe have received their inheritance beyond the Jordan at Jericho eastward, toward the sun-rising.'
16 BWANA akanena na Musa akasema,
And the LORD spoke unto Moses, saying:
17 “Haya ndiyo majinaya watu watakaoigawa ardhi kwa ajili ya urithi wao: Eliazari kuhani na Joshua mwana wa Nuni.
'These are the names of the men that shall take possession of the land for you: Eleazar the priest, and Joshua the son of Nun.
18 Mtachagua kiongozi mmoja toka kila kabila ili kuigawa ardhi kwa koo zao.
And ye shall take one prince of every tribe, to take possession of the land.
19 Haya ndiyo majina ya wanaume: Kutoka kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune.
And these are the names of the men: of the tribe of Judah, Caleb the son of Jephunneh.
20 Kutoka kwenye kabila la uzao wa Simeoni, Shemueli mwana wa Amihudi.
And of the tribe of the children of Simeon, Shemuel the son of Ammihud.
21 Kutoka kabila la Benjamini, Elidadi mwana wa Kisloni.
Of the tribe of Benjamin, Elidad the son of Chislon.
22 Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Dani, Buki mwana wa Jogili.
And of the tribe of the children of Dan a prince, Bukki the son of Jogli.
23 Kiongozi kutoka uzao wa Yusufu, kwenye kabila la Manase, Hannieli mwana wa Efodi.
Of the children of Joseph: of the tribe of the children of Manasseh a prince, Hanniel the son of Ephod;
24 Kiongozi kutoka kwenye kabila la uzao wa Efraimu, Kemueli mwana wa Shiftani.
and of the tribe of the children of Ephraim a prince, Kemuel the son of Shiphtan.
25 Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Zabuloni, Elizafani mwana wa Parinaki.
And of the tribe of the children of Zebulun a prince, Eli-zaphan the son of Parnach.
26 Kiongozi kutoka kwenye kabila la uzao wa Isakari, Palitieli mwana wa Azzani.
And of the tribe of the children of Issachar a prince, Paltiel the son of Azzan.
27 Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Asheri, Ahihudi mwana wa Shelomi.
And of the tribe of the children of Asher a prince, Ahihud the son of Shelomi.
28 Kiongozi kutoka kabila la uzao wa Naftali, Pedaheli mwana wa Amihudi.”
And of the tribe of the children of Naphtali a prince, Pedahel the son of Ammihud.
29 BWANA aliwaamuru wanaume hawa kuigawa nchi ya Kanaani na kuwapa kila kabla sehemu yao.
These are they whom the LORD commanded to divide the inheritance unto the children of Israel in the land of Canaan.'

< Hesabu 34 >