< Hesabu 3 >

1 Sasa hii ndiyo historia ya uzao wa Haruni na Musa wakati BWANA aliposema na Musa kwenye mlima Sinai.
Now this is the history of the generations of Aaron [Light-bringer] and Moses [Drawn out] in the day that Adonai spoke with Moses [Drawn out] in Mount Sinai [Thorn].
2 Majina ya watoto wa Haruni walikuwa Nadabu ambaye ndiyo mtoto wa kwanza, na Abihu, na Eliezeri, na Ithamari.
These are the names of the sons of Aaron [Light-bringer]: Nadab the firstborn, and Abihu, Eleazar [Help of God], and Ithamar.
3 Haya ndiyo majina ya wana wa Haruni, makuhani waliokuwa wamepakwa mafuta na kuwekwa wakfu kutumika kama makuhani.
These are the names of the sons of Aaron [Light-bringer], the priests who were anointed, whom he consecrated to minister in the priest’s office.
4 Lakini Nadabu na Abihu walikufa mbele ya BWANA walipomtolea moto usiokubalika walipokuwa katika nyika ya Sinai. Nadabu na Abihu hawakuwa na watoto, kwa hiyo Eliazari na Ithamari walitumika kama makuhani pamoja na baba yao.
Nadab and Abihu died before Adonai, when they offered strange fire before Adonai, in the wilderness of Sinai [Thorn], and they had no children. Eleazar [Help of God] and Ithamar ministered in the priest’s office in the presence of Aaron [Light-bringer] their father.
5 BWANA alinena na Musa, akamwambia,
Adonai spoke to Moses [Drawn out], saying,
6 “Walete kabila ya Lawi na uwaweke kwa Haruni kuhani ili wamsaidie
“Bring the tribe of Levi [United with] near, and set them before Aaron [Light-bringer] the priest, that they may minister to him.
7 Nao lazima wafanye majukumu badala ya Haruni na jumuiya yote mbele ya hema ya kukutania. Lazima watumike hemani.
They shall keep his requirements, and the requirements of the whole congregation before the Tent of Meeting, to do the service of the tabernacle.
8 Watayatunza mapambo ya hema ya kukutania, na watawatumikia makabila ya Israel kwa huduma ya hemani.
They shall keep all the furnishings of the Tent of Meeting, and the obligations of the children of Israel [God prevails], to do the service of the tabernacle.
9 Uwaweke Walawi kwa Haruni na watoto wake. Nimewatoa kikamilifu ili wamsaidie kuwatumikia watu wa Israel.
You shall give the Levites [Descendants of United with] to Aaron [Light-bringer] and to his sons. They are wholly given to him on the behalf of the children of Israel [God prevails].
10 Umchague Haruni na watoto wake kuwa makuhani, lakini mgeni yeyote atakayekaribia lazima auawe.”
You shall appoint Aaron [Light-bringer] and his sons, and they shall keep their priesthood. The stranger who comes near shall be put to death.”
11 BWANA alinena na Musa. akamwambia,
Adonai spoke to Moses [Drawn out], saying,
12 “Tazama, nimewachagua Walawi katika watu wa Israel. Nimefanya hivyo badala ya kuchukua mzaliwa wa kwanza wa kiume wa wana wa Israel. Hawa Walawi ni wangu.
“Behold, I have taken the Levites [Descendants of United with] from among the children of Israel [God prevails] instead of all the firstborn who open the womb among the children of Israel [God prevails]; and the Levites [Descendants of United with] shall be mine:
13 Na hata wazaliwa wa kwanza ni mali yangu. Katika siku ambyo niliwavamia wazaliwa wote wa kwanza wa nchi ya Misri, Niliwatenga wazaliwa wa kwanza wa Israeli kwa ajili yangu, watu na wanyama pia. Ni mali yangu. Mimi ndimi BWANA.”
for all the firstborn are mine. On the day that I struck down all the firstborn in the land of Egypt [Abode of slavery] I made holy to me all the firstborn in Israel [God prevails], both man and animal. They shall be mine. I am Adonai.”
14 BWANA alinena na Musa katika nyika ya Sinai. Akasema,
Adonai spoke to Moses [Drawn out] in the wilderness of Sinai [Thorn], saying,
15 “Wahesabu uzao wa Lawi katika kila familia, katika nyumba za koo zao. Hesabu kila mume kuanzia mwezi mmoja au zaidi.”
“Count the children of Levi [United with] by their fathers’ houses, by their families. You shall count every male from a month old and upward.”
16 Musa aliwahesabu, kufuata maelekezo ya BWANA, kama alivyoamriwa kufanya.
Moses [Drawn out] counted them according to Adonai’s word, as he was enjoined.
17 Majina ya watoto waLawi yalikuwa Gerishoni, Kohathi, na Merari.
These were the sons of Levi [United with] by their names: Gershon, and Kohath, and Merari.
18 Ukoo uliotokana na watoto wa Gerishoni walikuwa ni Libni na Shimei.
These are the names of the sons of Gershon by their families: Libni and Shimei.
19 Ukoo uliotokana na watoto Kohathi walikuwa ni Amramu na, Izihari, Hebroni, na Uzieli.
The sons of Kohath by their families: Amram, and Izhar, Hebron, and Uzziel.
20 Ukoo uliotokana na watoto wa Merari walikuwa ni Mahili na Mushi. Hizi ndizo koo za Walawi, zilizoorodheshwa ukoo kwa ukoo.
The sons of Merari by their families: Mahli and Mushi. These are the families of the Levites [Descendants of United with] according to their fathers’ houses.
21 Koo za Walibini na Washimei zilitokana na Wagerishoni. Hizi ndizo koo za Wagerishoni.
Of Gershon was the family of the Libnites, and the family of the Shimeites: these are the families of the Gershonites.
22 Wanaume wote wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi walihesabiwa na kufikia idadi ya 7, 500.
Those who were counted of them, according to the number of all the males, from a month old and upward, even those who were counted of them were seven thousand five hundred.
23 Koo za Wagerishoni watapanga upande wa magharibi wa hema.
The families of the Gershonites shall encamp behind the tabernacle westward.
24 Eliasafu mwana wa Laeli ataongoza koo za uzao wa Wagerishoni.
The prince of the fathers’ house of the Gershonites shall be Eliasaph the son of Lael.
25 Familia ya Gerishoni watalilinda hema la kukutania pamoja na hiyo masikani. Watalilinda hema, kifuniko chake, na lile pazia la lango la hema ya kukutania.
The duty of the sons of Gershon in the Tent of Meeting shall be the tabernacle, and the tent, its covering, and the screen for the door of the Tent of Meeting,
26 Wataulinda ua, lile pazia la kwenye lango—ua unaozunguka mahali patakatifu na madhabahu. Watazilinda kamba za hema ya kukutania na vyote vilivyomo.
and the hangings of the court, and the screen for the door of the court, which is by the tabernacle, and around the altar, and its cords for all of its service.
27 Koo zifuatazo zinatokana na Kohathi: ukoo wa Waamrami, ukoo wa Waizihari ukoo wa Wahebroni, na ukoo wa Wauzieli. Koo hizi zinatokana na Wakohathi.
Of Kohath was the family of the Amramites, and the family of the Izharites, and the family of the Hebronites, and the family of the Uzzielites: these are the families of the Kohathites.
28 Wanaume 8, 600 wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi walihesabiwa ili kulinda vitu vya BWANA.
According to the number of all the males, from a month old and upward, there were eight thousand six hundred, keeping the requirements of the sanctuary.
29 Familia ya uzao wa Kohathi watapanga upande wa kusini wa Hema.
The families of the sons of Kohath shall encamp on the south side of the tabernacle.
30 Elizafani mwana wa Uzieli ndiye atakayeongoza ukoo wa Wakohathi.
The prince of the fathers’ house of the families of the Kohathites shall be Elizaphan the son of Uzziel.
31 Watalilinda sanduku, meza, vikalishio vya taa, madhabahu, vitu vitakatifu ambvyo hutumika katika huduma yao, pazia, na kazi zote zinazoambatana na hema.
Their duty shall be the ark, the table, the menorah ·lamp·, the altars, the utensils of the sanctuary with which they minister, and the screen, and all its service.
32 Eliazari mwana wa Haruni kuhani atawaongoza wanaume wanaowaongoza Walawi. Atawasimamia wanaume wanaongoza eneo takatifu.
Eleazar [Help of God] the son of Aaron [Light-bringer] the priest shall be prince of the princes of the Levites [Descendants of United with], with the oversight of those who keep the requirements of the sanctuary.
33 Koo mbili zimetoka kwa Merari: Ukoo wa Mahili na ukoo wa Mushi. Koo hizi zimetokana na Merari,
Of Merari was the family of the Mahlites, and the family of the Mushites. These are the families of Merari.
34 Wanaume 6, 200 wenye umri wa mwezi mmoja na zaidi walihesabiwa.
Those who were counted of them, according to the number of all the males, from a month old and upward, were six thousand two hundred.
35 Zurieli mwana wa Abihaili ataongoza ukoo wa Merari. Hawa watapanga upande wa kaskazini mwa hema.
The prince of the fathers’ house of the families of Merari was Zuriel the son of Abihail. They shall encamp on the north side of the tabernacle.
36 Uzao wa Merari utatunza mbao za hema, mataruma, nguzo, makalishio, viifaa vya ujenzi na vitu vyote vinavyohusika,
The appointed duty of the sons of Merari shall be the tabernacle’s boards, its bars, its pillars, its sockets, all its instruments, all its service,
37 na nguzo za ua zinazozunguka hema, makalishio, vigingi na kamba zake.
the pillars of the court around it, their sockets, their pins, and their cords.
38 Musa na Haruni na watoto wake watapanga upande wa mashariki wa masikani, mbele ya hema ya kukutania kuelekea mawio ya jua. Wao wataajibika na majukumu ya mahali patakatifu na majukumu ya wana wa Israeli. Mgeni atakayekaribia mahali patakatifu auawe.
Those who encamp before the tabernacle eastward, in front of the Tent of Meeting toward the sunrise, shall be Moses [Drawn out], and Aaron [Light-bringer] and his sons, keeping the requirements of the sanctuary for the duty of the children of Israel [God prevails]. The stranger who comes near shall be put to death.
39 Musa na Haruni wakawahesabu wanaume wote wa ukoo wa Walawi walikuwa na umri wa mwezi mmoja na zaidi, kama vile BWANA alivyokuwa ameagiza. Walihesabu wanaume ishirini na mbili elfu.
All who were counted of the Levites [Descendants of United with], whom Moses [Drawn out] and Aaron [Light-bringer] counted by their families, all the males from a month old and upward, were twenty-two thousand.
40 BWANA alisema na Musa, “Wahesabu wanaume wote ambo ni wazaliwa wa kwanza wa Israeli ambao wana umri wa mwezi mmoja na zaidi. Orodhesha majina yao.
Adonai said to Moses [Drawn out], “Count all the firstborn males of the children of Israel [God prevails] from a month old and upward, and take the number of their names.
41 Unitwalie walawi kwa ajili yangu badala ya wazaliwa wa kwanza wa Israeli, Mimi ndimi BWANA. Na utwae wanyama wa Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wa wanyama wa uzao wa Israeli,”
You shall take the Levites [Descendants of United with] for me (I am Adonai ·) instead of all the firstborn among the children of Israel [God prevails]; and the livestock of the Levites [Descendants of United with] instead of all the firstborn among the livestock of the children of Israel [God prevails].”
42 Musa akawahesabu wazaliwa wa kwanza wote wa Israeli kama BWANA alivyomwagiza kufanya.
Moses [Drawn out] counted, as Adonai enjoined him, all the firstborn among the children of Israel [God prevails].
43 Aliwahesabu wazaliwa wote wa kwanza kwa mjina, wenye umri wa mwezi mmoja na zaidi. Alihesabu wanaume 22, 273.
All the firstborn males according to the number of names, from a month old and upward, of those who were counted of them, were twenty-two thousand two hundred seventy-three.
44 Tena BWANA alinena na Musa. Akasema,
Adonai spoke to Moses [Drawn out], saying,
45 “Watwae Walawi badala ya wazaliwa wote wa kwanza wa wana wa Israeli. Na utwae wanyama wa Walawi badala ya wanyama wa Waisreli wengine. Walawi ni mali yangu. Mimi ndimi BWANA.
“Take the Levites [Descendants of United with] instead of all the firstborn among the children of Israel [God prevails], and the livestock of the Levites [Descendants of United with] instead of their livestock; and the Levites [Descendants of United with] shall be mine. I am Adonai.
46 Unikusanyie shekeli tano za wokovu kwa kila hao 273 za hao wazaliwa wa kwanza wa Israeli za hao wanaozidi idadi ya Walawi.
For the redemption of the two hundred seventy-three of the firstborn of the children of Israel [God prevails], who exceed the number of the Levites [Descendants of United with],
47 Utazitumia hizo shekeli tano kwa kipimo cha mahali patakatifu. Shekeli moja ni sawa na gera ishirini.
you shall take five shekels [2 oz; 56.7 g] for each one, that is 273 shekels [6.83 lb; 3.1 kg] total; after the shekel of the sanctuary you shall take them; (the shekel is 0.4oz; 11.34 g; or called twenty gerahs 20/50 of an oz):
48 Utawalipa hizo shekeli za wokovu kwa Haruni na wanawe.”
and you shall give the money, with which their remainder is redeemed, to Aaron [Light-bringer] and to his sons.”
49 Kwa hiyo Musa akakusanya shakeli za wokovu kutoka kwa wale waliozidi idadi ya wale waliookolewa na Walawi.
Moses [Drawn out] took the redemption money from those who exceeded the number of those who were redeemed by the Levites [Descendants of United with];
50 Musa akakusanya zile fedha kutoka kwa hao wazaliwa wa kwanza wa wana wa Israeli. Alikusanya jumla ya shekeli 1, 365, zenye kipimo sawa na mahali patakatifu. Musa akamlipa Haruni na wanawe hizo shekeli za wokovu.
from the firstborn of the children of Israel [God prevails] he took the money, one thousand three hundred sixty-five shekels [34.13 lb; 15.48 kg], after the shekel of the sanctuary [0.4 oz; 11.34 g]:
51 Musa akafanya kila kitu alichoagizwa na neno la BWANA kama BWANA alivyomwagiza.
and Moses [Drawn out] gave the redemption money to Aaron [Light-bringer] and to his sons, according to Adonai’s word, as Adonai enjoined Moses [Drawn out].

< Hesabu 3 >