< Hesabu 1 >

1 Mungu alimwambia Musa katika hema ya kukutania walipokuwa katika jangwa la Sinai. Hii ilitokea katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili miaka miwili baadaya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Mungu alisema,
Adonai spoke to Moses [Drawn out] in the wilderness of Sinai [Thorn], in the Tent of Meeting, on the first day of the second month, in the second year after they had come out of the land of Egypt [Abode of slavery], saying,
2 'fanya sensa ya wanaume wote wa Israel kutoka kila ukoo, katika familia za baba zao. Wahesabu kwa majina, wahesabu kila mume, kila mwanamume
“Take a census of all the congregation of the children of Israel [God prevails], by their families, by their fathers’ houses, according to the number of the names, every male, one by one;
3 kuanzia umri a miaka ishirini na zaidi. Uwahesabu wote wanaoweza kupigana kama askari wa Israel. Wewe na Haruni mtaandika idadi ya wanaume katika makundi ya majeshi yao.
from twenty years old and upward, all who are able to go out to war in Israel [God prevails]. You and Aaron [Light-bringer] shall count them by their divisions.
4 Kila mwanamume kwa kila kabila, kichwa cha ukoo, lazima atumike na wewe kama kiongozi wa kabila.
With you there shall be a man of every tribe; everyone head of his fathers’ house.
5 Haya ndiyo majina ya viongozi ambao watapigana pamoja na wewe: Kutoka kabila la Reubeni, Elizuri mwana wa Shedeuri;
These are the names of the men who shall stand with you: Of Reuben [See, a son!]: Elizur the son of Shedeur.
6 kutoka kabila la Simeoni, Shelumiel mwana wa Zurishadai
Of Simeon [Hearing]: Shelumiel the son of Zurishaddai [My rock almighty].
7 Kutoka kabila la Yuda, Nashoni mwana wa Aminadabu;
Of Judah [Praised]: Nahshon the son of Amminadab.
8 Ktoka kabila la Isakari, Nethaneli mwana wa Zuari;
Of Issachar [Hire, Reward]: Nethanel the son of Zuar.
9 kutoka kabila Zebuluni, Eliabu mwana wa Heloni
Of Zebulun [Living together]: Eliab the son of Helon.
10 kutoka kabila la Efraimu mwana wa Yusufu, Elishama mwana wa Ammihudi; kutoka kabila la Manase, Gamaliel mwan wa Pedazuri;
Of the children of Joseph [May he add]: Of Ephraim [Fruit]: Elishama the son of Ammihud. Of Manasseh [Causing to forget]: Gamaliel the son of Pedahzur.
11 kutoka kabila la Benjamini mwana wa Ysufu, Abidani mwan wa Gidion;
Of Benjamin [Son of right hand, Son of south]: Abidan the son of Gideoni.
12 Kutoka kabila la Dan, Ahizeri mwana wa Amishadai;
Of Dan [He judged]: Ahiezer the son of Ammishaddai.
13 kutoka kabila Asheri, Pagieli mwana wa Okirani;
Of Asher [Happy]: Pagiel the son of Ochran.
14 kutoka kabila la Gadi, Eliasafu mwana wa Deuli;
Of Gad [Good fortune]: Eliasaph the son of Deuel.
15 na kutoka kabila la Naftali, Ahira mwana wa Enani.”
Of Naphtali [My wrestling]: Ahira the son of Enan.”
16 Hawa ndio wanaume waliochaguliwa kutoka kwa watu. Waliongoza kabila za mababu zao. Walikuwa viongozi wa koo katika Israel.
These are those who were called of the congregation, the princes of the tribes of their fathers; they were the heads of the thousands of Israel [God prevails].
17 Musa na Haruni wakawachukua wale wanaume, waliokuwa wameandikwa kwa majina,
Moses [Drawn out] and Aaron [Light-bringer] took these men who are mentioned by name.
18 na pamoja na wanaume hao waliwakusanya wanume wote katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Kisha kila mwanume wa miaka ishirini na zaidi alitambua babu zake. Alitakiwa kutaja koo na famila kutoka katika ukoo.
They assembled all the congregation together on the first day of the second month; and they declared their ancestry by their families, by their fathers’ houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, one by one.
19 Kisha Musa akaandika hesabu yao huko katika nyika ya Sinai, Kama Mungu alivyokuwa amemwamuru kufanya.
As Adonai enjoined Moses [Drawn out], so he counted them in the wilderness of Sinai [Thorn].
20 Kutoka uzao wa Reubeni, mtoto wa kwanza wa Israel, yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini na zaidi wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka hesabu ya ukoo na familia.
The children of Reuben [See, a son!], Israel [God prevails]’s firstborn, their generations, by their families, by their fathers’ houses, according to the number of the names, one by one, every male from twenty years old and upward, all who were able to go out to war;
21 Waliwahesabu wanaume 46, 000 kutoka ukoo wa Reubeni.
those who were counted of them, of the tribe of Reuben [See, a son!], were forty-six thousand five hundred.
22 Kutoka uzao wa Simeoni yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini na zaidi au wenye uwezo wa kwenda vitani, kutokana na hesabu ya ukoo na familia.
Of the children of Simeon [Hearing], their generations, by their families, by their fathers’ houses, those who were counted of it, according to the number of the names, one by one, every male from twenty years old and upward, all who were able to go out to war;
23 Walihesabu wanaume 59, 300 kutoka kabila la Simeoni.
those who were counted of them, of the tribe of Simeon [Hearing], were fifty-nine thousand three hundred.
24 Kutoka uzao wa Gadi yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Of the children of Gad [Good fortune], their generations, by their families, by their fathers’ houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war;
25 Walihesabu wanaume 45, 650 kutoka kabila la Gadi.
those who were counted of them, of the tribe of Gad [Good fortune], were forty-five thousand six hundred fifty.
26 Kutoka uzao wa Yuda yalihesabiwa majina yote ya wanaume wenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Of the children of Judah [Praised], their generations, by their families, by their fathers’ houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war;
27 walihesabiwa wanume 74, 000 kutoka kabila la Yuda.
those who were counted of them, of the tribe of Judah [Praised], were seventy-four thousand six hundred.
28 Kutoka uzao wa Isakari yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Of the children of Issachar [Hire, Reward], their generations, by their families, by their fathers’ houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war;
29 Walihesabiwa wanaume 54, 000 kutoka kabila la Isakari.
those who were counted of them, of the tribe of Issachar [Hire, Reward], were fifty-four thousand four hundred.
30 Kutoka uzao wa Zabuloni yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Of the children of Zebulun [Living together], their generations, by their families, by their fathers’ houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war;
31 Walihesabiwa wanume 57, 400 kutoka kabila la Zabuloni.
those who were counted of them, of the tribe of Zebulun [Living together], were fifty-seven thousand four hundred.
32 Kutoka uzao wa Efraimu mwana wa Yusufu yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Of the children of Joseph [May he add], of the children of Ephraim [Fruit], their generations, by their families, by their fathers’ houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war;
33 Walihesabiwa wanaume 40, 500 kutoka kabila la Efraimu.
those who were counted of them, of the tribe of Ephraim [Fruit], were forty thousand five hundred.
34 Kutoka uzao wa Manase mwana wa Yusufu yaliheabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu y a ukoo na familia.
Of the children of Manasseh [Causing to forget], their generations, by their families, by their fathers’ houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war;
35 Walihesabiwa wanaume 32, 000 kutoka kabila la Manase.
those who were counted of them, of the tribe of Manasseh [Causing to forget], were thirty-two thousand two hundred.
36 Kutoka uzao wa Benjamini yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Of the children of Benjamin [Son of right hand, Son of south], their generations, by their families, by their fathers’ houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war;
37 Walihesabiwa wanaume 35, 000 kutoka kabila la Benjamini.
those who were counted of them, of the tribe of Benjamin [Son of right hand, Son of south], were thirty-five thousand four hundred.
38 Kutoka uzao wa Dani yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na mwenye uwezo wa kwenda vitani, Kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Of the children of Dan [He judged], their generations, by their families, by their fathers’ houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war;
39 Walihesabiwa wanaume 62, 000 kutoka kabila la Dani.
those who were counted of them, of the tribe of Dan [He judged], were sixty-two thousand seven hundred.
40 Kutoka uzao wa Asheri yalihesabiwa majina yote ya kila mwanume mwenye umri wa miaka ishirini au zadi na mwenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu y a ukoo na familia.
Of the children of Asher [Happy], their generations, by their families, by their fathers’ houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war;
41 Walihesabiwa wanaume 41, 500 kutoka ukoo wa Asheri.
those who were counted of them, of the tribe of Asher [Happy], were forty-one thousand five hundred.
42 Kutoka ukoo wa Naftali yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na mwenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia.
Of the children of Naphtali [My wrestling], their generations, by their families, by their fathers’ houses, according to the number of the names, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war;
43 Walihesabiwa wanaume 53, 400 kutoka kabila la Naftari
those who were counted of them, of the tribe of Naphtali [My wrestling], were fifty-three thousand four hundred.
44 Musa na Haruni waliwahesabu wanaume wote hawa, pamoja na wale wanaume kumi na wawili waliokuwa wakiongoza yale makabila kumi na mawili ya Israeli.
These are those who were counted, whom Moses [Drawn out] and Aaron [Light-bringer] counted, and the princes of Israel [God prevails], being twelve men: they were each one for his fathers’ house.
45 Kwa hiyo wanaume wote wa Israeli wenye umri wa miak ishirini au zaidi, wote wenye uwezo wa kwenda vitani, walihesabiwa kutoka kwenye familia zao.
So all those who were counted of the children of Israel [God prevails] by their fathers’ houses, from twenty years old and upward, all who were able to go out to war in Israel [God prevails];
46 Walihesabu wanaume 603, 550.
even all those who were counted were six hundred three thousand five hundred fifty.
47 Lakini wanaume toka uzao wa Lawi hawakuhesabiwa,
But the Levites [Descendants of United with] after the tribe of their fathers was not counted among them.
48 Kwa sababu BWANA alimwambia Musa,
For Adonai spoke to Moses [Drawn out], saying,
49 “usiwahesabu wale wa kabila la Lawi wala kuwajumuisha kwenye jumla ya watu wa Israeli.
“Only the tribe of Levi [United with] you shall not count, neither shall you take a census of them among the children of Israel [God prevails];
50 Badala yake, waagize Walawi kuliangalia hema la amri za agano, na kuangalia mapambo ya hema na vyote vilivyomo. Walawi watalazimika kulibeba hema na lazima wayabebe mapambo ya hema. Lazima waliangalie hema na kuyatengeneza mazingira yake. Wataiangalia masikani na kuzitengeneza kambi zinazolizunguka.
but appoint the Levites [Descendants of United with] over the Tabernacle of the Testimony, and over all its furnishings, and over all that belongs to it. They shall carry the tabernacle, and all its furnishings; and they shall take care of it, and shall encamp around it.
51 Kila hema litakapotakiwa kuhamishiwa eneo jingine, Walawi ndio watakaolipeleka pale. Na kila hema litakapotakiwa kusimamishwa, Walawi ndio watakao lisimamisha. Na mgeni yeyote atakayelisogelea hema lazima auawe.
When the tabernacle is to move, the Levites [Descendants of United with] shall take it down; and when the tabernacle is to be set up, the Levites [Descendants of United with] shall set it up. The stranger who comes near shall be put to death.
52 Wakati watu wa Israeli watakaposimamisha hema zao, kila mwanaume lazima awe karibu na bango la jeshi lake.
The children of Israel [God prevails] shall pitch their tents, every man by his own camp, and every man by his own standard, according to their divisions.
53 Hata hivyo Walawi lazima waweke hema zao kuizunguka hiyo masikani ya amri za agano ili kwamba hasira yangu isije ikawaka juu ya wana wa Israeli. Walawi lazima wailinde hiyo masikani ya amri za agano.”
But the Levites [Descendants of United with] shall encamp around the Tabernacle of the Testimony, that there may be no wrath on the congregation of the children of Israel [God prevails]: and the Levites [Descendants of United with] shall be responsible for the Tabernacle of the Testimony.”
54 Wana wa Israeli walifanya yote haya. Walifanya yote ambayo BWANA aliagiza kupitia Musa.
Thus the children of Israel [God prevails] did. According to all that Adonai enjoined Moses [Drawn out], so they did.

< Hesabu 1 >