< Hesabu 17 >

1 BWANA akanena na Musa, akasema,
Yahweh spoke to Moses. He said,
2 “Waambie wana wa Israeli wakuletee fimbo za kutembelea moja kwa kila jamaa, fimbo kumi na mbili. Uandika jina la kila mmoja kwenye hizo fimbo.
“Speak to the people of Israel and get staffs from them, one for each ancestral tribe, twelve staffs. Write each man's name on his staff.
3 Utaandika jina la Haruni kwenye jina la Lawi. Kutakuwa na fimbo moja kwa kila kiongozi kutoka kwenye kabila la mababu zake.
You must write Aaron's name on Levi's staff. There must be one staff for each leader from his ancestors' tribe.
4 Utaziweka hizo fimbo kwenye hema ya kukutania mbele ya amri za agano, ambapo Mimi hukutana na wewe. Itakuwa hivi,
You must place the staffs in the tent of meeting in front of the covenant decrees, where I meet with you.
5 fimbo ya mtu yule ninayemchagua itachipua. Nitazuia watu wa Israeli walalamikao, ambao wanaongea kinyume na wewe.”
It will happen that the staff of the man whom I choose will bud. I will cause the complaints from the people of Israel to stop, which they are speaking against you.”
6 Kwa hiyo Musa akawaambia wana wa Israeli. Viongozi wote wa kabila wakampatia fimbo, fimbo moja kutoka kwa kila kiongozi, aliyechaguliwa kutoka kwenye kila kabila ya babu zao, jumla yake fimbo kumi na mbili. Fimbo ya Haruni ilikuwa miongoni mwa fimbo hizo.
So Moses spoke to the people of Israel. All the tribal leaders gave him staffs, one staff from each leader, selected from each of the ancestral tribes, twelve staffs in all. Aaron's staff was among them.
7 Ndipo Musa alipoziweka zile fimbo mbele ya BWANA katika hema ya amri ya agano.
Then Moses deposited the staffs before Yahweh in the tent of the covenant decrees.
8 Siku iliyofuata Musa aliingia kwenye hema ya amri ya agano, na tazama, fimbo ya Haruni kwa ajili ya Kabila la Lawi ilikuwa imetoa machipukizi. Machipukizi yalikuwa hadi kuchanua maua na kuzaa malozi mabivu!
The next day Moses went into the tent of the covenant decrees and, behold, Aaron's staff for the tribe of Levi had budded. It grew buds and produced blossoms and ripe almonds!
9 Musa akazitoa fimbo zote kutoka kwa BWANA kwa watu wote wa Israeli, na kila mtu akachukua fimbo yake.
Moses brought out all the staffs from before Yahweh to all the people of Israel, and each man took his staff.
10 BWANA akamwambua Musa, “Iweke fimbo ya Haruni mbele ya amri za agano. Iweke iwe ishara ya hatia mbele ya watu waliopinga ili ukomeshe malalamiko dhidi yangu, vinginevyo watakufa.”
Yahweh said to Moses, “Put Aaron's staff in front of the covenant decrees. Keep it as a sign of guilt against the people who rebelled so that you may end complaints against me, or they will die.”
11 Musa akafanya kama BWANA alivyoagiza.
Moses did just as Yahweh had commanded him.
12 Wana wa Israeli wakanena na Musa wakisema, “tutakufa hapa! Wote tutaangamia!
The people of Israel spoke to Moses and said, “We will die here. We will all perish!
13 Kila mmoja anayekuja hapa, anayekaribia masikani ya BWANA, atakufa. Je, ni lazima wote tuangamie?”
Everyone who comes up, who approaches Yahweh's tabernacle, will die. Must we all perish?”

< Hesabu 17 >