< Hesabu 13 >

1 Kisha BWANA akanena na Musa, akamwambia, “tuma watu waende kuipeleleza nchi ya Kanani, ambayo nimewapa wana wa Israeli.
And the LORD spoke unto Moses, saying:
2 Tuma mwanamume mmoja kutoka kila jamaa ya kabila. Kila mwanamume awe kiongozi katika kabila lake.”
'Send thou men, that they may spy out the land of Canaan, which I give unto the children of Israel; of every tribe of their fathers shall ye send a man, every one a prince among them.'
3 Musa akawatuma kutoka jangwa la Parani, ili watii amri ya BWANA. Watu wote hao walikuwa viongozi wa watu wa Israeli.
And Moses sent them from the wilderness of Paran according to the commandment of the LORD; all of them men who were heads of the children of Israel.
4 Majina yao yalikuwa haya yafuatayo: kutoka kabila la Reubeni, Shamua mwana wa Zakuri;
And these were their names: of the tribe of Reuben, Shammua the son of Zaccur.
5 Kutoka kabila la Simeoni, Shafati mwana wa Hori;
Of the tribe of Simeon, Shaphat the son of Hori.
6 Kutoka kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune;
Of the tribe of Judah, Caleb the son of Jephunneh.
7 Kutoka kabila la Isakari, Igali mwana wa Yusufu,
Of the tribe of Issachar, Igal the son of Joseph.
8 Kutoka kabila la Efraimu, Hoshea mwana wa Nuni;
Of the tribe of Ephraim, Hoshea the son of Nun.
9 Kutoka kabila la Benjamini, Paliti mwana wa Rafu;
Of the tribe of Benjamin, Palti the son of Raphu.
10 kutoka kabila ya Zabuloni, Gadieli mwana wa Sodi;
Of the tribe of Zebulun, Gaddiel the son of Sodi.
11 kutoka kabila la Yusufu (hiyo inamaanisha kutoka kabila la Manase), Gadi mwana wa Susi;
Of the tribe of Joseph, namely, of the tribe of Manasseh, Gaddi the son of Susi.
12 kutoka kabila la Dani, Amieli mwana wa Gemalili;
Of the tribe of Dan, Ammiel the son of Gemalli.
13 kutoka kabila Asheri, Setu mwana wa Mikaili;
Of the tribe of Asher, Sethur the son of Michael.
14 kutoka kabila la Naftali, Nabi mwana wa Vofisi;
Of the tribe of Naphtali, Nahbi the son of Vophsi.
15 kutoka kabila la Gadi, Geuli mwana wa Machi.
Of the tribe of Gad, Geuel the son of Machi.
16 Haya ndiyo majina ya wanaume ambao Musa aliwatuma kwenda kuipelelza ile nchi. Musa akamwita Hoshea mwana wa Nuni kwa jina la Joshua.
These are the names of the men that Moses sent to spy out the land. And Moses called Hoshea the son of Nun Joshua.
17 Musa akawatuma kwenda kuipeleleza ile nchi ya Kanani. Naye akawaambia, “Mkaanzie Negebu hadi mahali pa milima.
And Moses sent them to spy out the land of Canaan, and said unto them: 'Get you up here into the South, and go up into the mountains;
18 Kaipelelezeni nchi kujua ni nchi ya namna gani. Wachunguzeni watu wake, kama ni watu wenye nguvu au dhaifu, kama ni wachache au ni wengi.
and see the land, what it is; and the people that dwelleth therein, whether they are strong or weak, whether they are few or many;
19 Chunguzeni nchi hiyo wanayoishi ni nchi ya namna gani. Ni nzuri au mbaya? Miji yao ikoje? Je iko kama kambi au ni miji yenye ngome?
and what the land is that they dwell in, whether it is good or bad; and what cities they are that they dwell in, whether in camps, or in strongholds;
20 Chunguzeni ni nchi ya namna gani, kama ni njema kwa mazao au la kama kuna miti au hapana. Mwe hodari mkalete sampuli za mazao ya nchi,” Sasa ni muda wa msimu wa malimbuko ya mizabibu.
and what the land is, whether it is fat or lean, whether there is wood therein, or not. And be ye of good courage, and bring of the fruit of the land.' — Now the time was the time of the first-ripe grapes. —
21 Kwa hiyo wale wanaume wakaenda kuipeleleza ile nchi kutoka jangwa la Sini mpaka Rehobi, karibu na Lebo Hamati.
So they went up, and spied out the land from the wilderness of Zin unto Rehob, at the entrance to Hamath.
22 Walienda kutoka Negebu nao wakafika Hebroni. Ahimani, Sheshai, na Talmai, Uzao wa Anaki nao walikuweko, Sasa Hebroni ilikuwa imejengwa miaka saba iliyokuwa imepita kabla ya Zoani wa Misri.
And they went up into the South, and came unto Hebron; and Ahiman, Sheshai, and Talmai, the children of Anak, were there. — Now Hebron was built seven years before Zoan in Egypt. —
23 Nao walipofika katika bonde la Eshikoli, walikata matawi ya mizabibu lenye kishada cha zabibu. Na makundi mawili ya wapelelezi wakakibeba kwenye mti. Pia wakaleta makomamanga na mtini.
And they came unto the valley of Eshcol, and cut down from thence a branch with one cluster of grapes, and they bore it upon a pole between two; they took also of the pomegranates, and of the figs. —
24 Mahali pale paliitwa Eshikoli, kwa sababu ya kishada cha mizabibu ambacho wana wa Israeli walikata kule.
That place was called the valley of Eshcol, because of the cluster which the children of Israel cut down from thence. —
25 Baada ya siku arobaini, wakarudi kutoka kuipeleleza nchi.
And they returned from spying out the land at the end of forty days.
26 Wakaja kwa Musa, Haruni na kwa watu wote wa Israeli katka jangwa la Parani, kule Kadeshi. Wakaleta taarifa kwao na kwa Waisraeli wote, na kuwaonyesha matunda ya nchi ile.
And they went and came to Moses, and to Aaron, and to all the congregation of the children of Israel, unto the wilderness of Paran, to Kadesh; and brought back word unto them, and unto all the congregation, and showed them the fruit of the land.
27 Wakamwambia Musa, “Tulifika katika ile nchi uliyotutuma. Kwa hakika ni nchi ya kutiririka maziwa na asali. Na baadhi ya matunda yake ni haya hapa.
And they told him, and said: 'We came unto the land whither thou sentest us, and surely it floweth with milk and honey; and this is the fruit of it.
28 Hata hivyo, watu wanaoishi huko ni wenye nguvu. Miji yao ni mikubwa tena ina maboma. Pia tuliwaona wana wa Anaki huko.
Howbeit the people that dwell in the land are fierce, and the cities are fortified, and very great; and moreover we saw the children of Anak there.
29 Waamaleki wanaishi Negebu. Wahiti, Wayebusi, na Waamori nao wanaishi katika milima ya hiyo nchi. Wakanaani wanaishi kando ya bahari na mto Yorodani.”
Amalek dwelleth in the land of the South; and the Hittite, and the Jebusite, and the Amorite, dwell in the mountains; and the Canaanite dwelleth by the sea, and along by the side of the Jordan.'
30 Kisha Kalebu akawatuliza watu waliokuwa mbele ya Musa, akasema, “Twendeni tukaiteke nyara hiyo nchi, kwa kuwa tuna uhakika wa kuikamata.”
And Caleb stilled the people toward Moses, and said: 'We should go up at once, and possess it; for we are well able to overcome it.'
31 Lakini wale watu waliokuwa wameenda naye walisema, “Hatutaweza kuwashinda hao watu kwa kuwa wao ni hodari kuliko sisi.”
But the men that went up with him said: 'We are not able to go up against the people; for they are stronger than we.'
32 Kwa hiyo wakasambaza taarifa za kukatisha tamaa kwa Wana wa Israeli juu ya nchi ile waliyoipeleleza. Walisema, “Ile nchi tuliyoiona ni nchi inayowala watu wake. Watu wote tuliowaona ni watu warefu.
And they spread an evil report of the land which they had spied out unto the children of Israel, saying: 'The land, through which we have passed to spy it out, is a land that eateth up the inhabitants thereof; and all the people that we saw in it are men of great stature.
33 Kule tuliiona majitu, wana wa uzao wa Anaki, ambao nii uzao wa majitu. Sisi tulionekana kama panzi machoni mwao tulipojilingsnisha nao, hivyo ndivyo tulivyoonekana machoni mwao pia.”
And there we saw the Nephilim, the sons of Anak, who come of the Nephilim; and we were in our own sight as grasshoppers, and so we were in their sight.'

< Hesabu 13 >