< Hesabu 16 >

1 Sasa Kora mwana wa Izihari mwana wa Kohathi mwana wa Lawi, pamoja na Dathani na Abiramu mwana wa Eliabu, na Oni mwana wa Peleti, wa uzao wa Reubeni, waliwakusanya wanaume kadhaa.
Now Korah, the son of Izhar, the son of Kohath, the son of Levi, with Dathan and Abiram, the sons of Eliab, and On, the son of Peleth, sons of Reuben, took men;
2 Wakamwinukia Musa, pamoja na wanaume fulani kutoka wana wa Israeli, viongozi wa watu wapatao mia mbili na hamsini waliokuwa wakifahamika katika ile jamii.
and they rose up in face of Moses, with certain of the children of Israel, two hundred and fifty men; they were princes of the congregation, the elect men of the assembly, men of renown;
3 Walikusanyika pamoja kumpinga Musa na Haruni. Wakawaambia, “Ninyi sasa mnatumia mamlaka zaidi ya uwezo wenu! Watu wote wamejitenga, kila mmoja wao, na BWANA yuko pamoja nao. Kwa nini mnajiinua sana juu ya watu wengine wa BWANA?”
and they assembled themselves together against Moses and against Aaron, and said unto them: 'Ye take too much upon you, seeing all the congregation are holy, every one of them, and the LORD is among them; wherefore then lift ye up yourselves above the assembly of the LORD?'
4 Musa alipoyasikia hayo, akalala kifudifudi.
And when Moses heard it, he fell upon his face.
5 Akamwambia Kora na wote aliokuwa nao, “Asubuhi BWANA atafanya ijulikane ni nani walio wake na nani aliyetengwa kwa ajili yake. Atamleta huyo mtu karibu na yeye. Yule anayemchagua atamleta karibu naye.
And he spoke unto Korah and unto all his company, saying: 'In the morning the LORD will show who are His, and who is holy, and will cause him to come near unto Him; even him whom He may choose will He cause to come near unto Him.
6 Fanya hivi, wewe Kora na kundi lako.
This do: take you censors, Korah, and all his company;
7 Kesho mchukue vyetezo na muweke moto na ubani ndani yake mbele ya BWANA. Yule ambaye BWANA amemchagua, atamtenga kwa BWANA. Sasa imetosha ninyi watu wa uzao wa Lawi,”
and put fire therein, and put incense upon them before the LORD to-morrow; and it shall be that the man whom the LORD doth choose, he shall be holy; ye take too much upon you, ye sons of Levi.'
8 Tena Musa akamwambia Kora, “Sasa unisililize, ninyi watu wa uzao wa Lawi:
And Moses said unto Korah: 'Hear now, ye sons of Levi:
9 Je ni jambo dogo kwenu kwamba Mngu wa mbinguni amewatenga ninyi kutoka watu wa Israeli, ili awalete ninyi karibu na yeye, ili mfanye kazi katika masikani ya BWANA na kusimama mbele ya watu ili muwatumikie?
is it but a small thing unto you, that the God of Israel hath separated you from the congregation of Israel, to bring you near to Himself, to do the service of the tabernacle of the LORD, and to stand before the congregation to minister unto them;
10 Amewasogeza karibu, na ndugu zako, wa uzao wa Lawi pamoja nanyi, na sasa mnataka na ukuhani pia!
and that He hath brought thee near, and all thy brethren the sons of Levi with thee? and will ye seek the priesthood also?
11 Hiyo ndiyo sababu wewe na kundi lako mmekusanyika pamoja kinyume na BWANA. Kwa nini mnalalamika juu ya Haruni, ambaye anamtii BWANA?”
Therefore thou and all thy company that are gathered together against the LORD —; and as to Aaron, what is he that ye murmur against him?'
12 Kisha Musa akamwita Dathani na Abiramu, wana wa Eliabu, lakini wakasema, “hatutakuja.
And Moses sent to call Dathan and Abiram, the sons of Eliab; and they said: 'We will not come up;
13 Kwani jambo dogo kwamba umetuleta mpaka kwenye nchi inayotiririka maziwa na asali, ili kutuua katika jangwa hili? Sasa unataka kujifanya kuwa mtawala wetu!
is it a small thing that thou hast brought us up out of a land flowing with milk and honey, to kill us in the wilderness, but thou must needs make thyself also a prince over us?
14 Na kwa nyongeza, haujatuingiza kwenye nchi ya kutiririka maziwa na asali, au kutupa urithi wa mashamba na mashamba ya mizabibu. Sasa unataka kutupofusha na ahadi hewa? Hatutakuja kwako.”
Moreover thou hast not brought us into a land flowing with milk and honey, nor given us inheritance of fields and vineyards; wilt thou put out the eyes of these men? we will not come up.'
15 Musa alikasirika sana na akamwambia BWANA, “Usisipokee sadaka zao. Sijachukua punda mmoja kutoka kwao, na sijamdhuru hata mmoja wao.”
And Moses was very wroth, and said unto the LORD: 'Respect not Thou their offering; I have not taken one ass from them, neither have I hurt one of them.'
16 Kisha Musa akamwambia Kora, “Kesho wewe na kundi lako mtaenda mbele za BWANA-wewe na wao na Haruni.
And Moses said unto Korah: 'Be thou and all thy congregation before the LORD, thou, and they, and Aaron, to-morrow;
17 Kila mmoja wenu atatwaa chetezo na kuweka ubani ndani yake. Ndipo kila mtu atamletea BWANA chetezo chake, vyetezo mia mbili na hamsini. Wewe na Haruni, pia, kila mmoja ataleta chetezo chake.
and take ye every man his fire-pan, and put incense upon them, and bring ye before the LORD every man his fire-pan, two hundred and fifty fire-pans; thou also, and Aaron, each his fire-pan.'
18 Kwa hiyo kila mtu alitwaa chetezo chake, akaweka moto ndani yake, akaweka na ubani ndani yake, na kusimama mbele ya lango la hema ya kukutania pamoja na Musa na Haruni.
And they took every man his fire-pan, and put fire in them, and laid incense thereon, and stood at the door of the tent of meeting with Moses and Aaron.
19 Kora naye akawakusanya watu wote waliokuwa kinyume na Musa na Haruni hapo kwenye lango la hema ya kukutania, na kisha utukufu wa BWANA ukaonekana kwa watu wote.
And Korah assembled all the congregation against them unto the door of the tent of meeting; and the glory of the LORD appeared unto all the congregation.
20 Ndipo BWANA aliposema na Musa na Haruni:
And the LORD spoke unto Moses and unto Aaron, saying:
21 “Tokeni ninyi kutoka hawa watu ili nipate kuwaangamiza haraka.”
'Separate yourselves from among this congregation, that I may consume them in a moment.'
22 Musa na Haruni wakalala kifudifudi na kusema, “Mungu, Mungu wa wote wenye mwili, kama mtu akitenda dhambi, ni lazima uwe na hasira na watu wote?”
And they fell upon their faces, and said: 'O God, the God of the spirits of all flesh, shall one man sin, and wilt Thou be wroth with all the congregation?'
23 BWANA akanena na Musa, akamwambia,
And the LORD spoke unto Moses, saying:
24 “Sema na watu wote, uwaaambie, 'Tokeni kwenye hema ya Kora, Dathani, na Abiramu.'”
'Speak unto the congregation, saying: Get you up from about the dwelling of Korah, Dathan, and Abiram.'
25 Kisha Musa akaamuka akaenda kwa Dathani na Kwa Abiramu; viongozi wa Israeli wakamfuata.
And Moses rose up and went unto Dathan and Abiram; and the elders of Israel followed him.
26 Akaongea na watu wote akasema, “Sasa jitengeni na hema ya hawa watu waovu na msiguse kitu chochote kilicho chao, vinginevyo mtaangamizwa na dhambi zao.”
And he spoke unto the congregation, saying: 'Depart, I pray you, from the tents of these wicked men, and touch nothing of theirs, lest ye be swept away in all their sins.'
27 Kwa hiyo watu wote toka pande zote za hema ya Kora, Dathani na Abiramu wakaondoka. Dathani na Abiramu wakatoka nje wakasimama kwenye lango la hema zao, wakiwa na wake wao, wana, na watoto wao.
So they got them up from the dwelling of Korah, Dathan, and Abiram, on every side; and Dathan and Abiram came out, and stood at the door of their tents, with their wives, and their sons, and their little ones.
28 Kisha Musa akasema, “Kwa hili sasa mtatambua kuwa BWANA amenituma kufanya kazi hizi zote, kwa kuwa sijazifanya kwa uwezo wangu.
And Moses said: 'Hereby ye shall know that the LORD hath sent me to do all these works, and that I have not done them of mine own mind.
29 Kama hawa watu watakufa kifo cha kawaida ambacho humpata kila mmoja, basi BWANA hakunituma.
If these men die the common death of all men, and be visited after the visitation of all men, then the LORD hath not sent Me.
30 Lakini kama BWANA aumbaye malango ya ardhi ambayo huwameza kama mdomo mkubwa, pamoja na familia zao, na kama wataingia ndani ya shimo wakiwa hai, ndipo mtakapojua kuwa wamemdharau BWANA,” (Sheol h7585)
But if the LORD make a new thing, and the ground open her mouth, and swallow them up, with all that appertain unto them, and they go down alive into the pit, then ye shall understand that these men have despised the LORD.' (Sheol h7585)
31 Mara ghafla Musa alipomaliza kusema maneno haya, aridhi ya pale walipokuwa ikafunguka.
And it came to pass, as he made an end of speaking all these words, that the ground did cleave asunder that was under them.
32 Dunia ikafungua makanwa yake na kuwameza, familia zao na watu wote wa Kora, pamoja na mali zao zote.
And the earth opened her mouth and swallowed them up, and their households, and all the men that appertained unto Korah, and all their goods.
33 Wao na kila mmoja kwenye familia zao wakaingia ndani shimoni wakiwa hai. Dunia ikwafunika, na kwa njia hii wakapotea kutoka miongoni mwa ile jamii. (Sheol h7585)
So they, and all that appertained to them, went down alive into the pit; and the earth closed upon them, and they perished from among the assembly. (Sheol h7585)
34 Nao Israeli yote waliokuwa karibu nao wakakimbia kwa sababu ya vilio vyao. Walisema kwa mshangao, “Nchi isije kutumeza na sisi!”
And all Israel that were round about them fled at the cry of them; for they said: 'Lest the earth swallow us up.'
35 Kisha moto ukashuka toka kwa BWANA na kuwaangamiza wale wanaume 250 waliokuwa wametoa ubani.
And fire came forth from the LORD, and devoured the two hundred and fifty men that offered the incense.
36 Tena BWANA akanena na Musa, akasema,
And the LORD spoke unto Moses, saying:
37 “Mwambie Eliazari mwana wa Haruni yule kuhani achukue vile vyetezo kutoka ule moto, kwa kuwa vile vyetezo vimetengwa ka ajili yangu. Na aumwage ule moto mbali.
'Speak unto Eleazar the son of Aaron the priest, that he take up the fire-pans out of the burning, and scatter thou the fire yonder; for they are become holy;
38 Vitwae vile vyetezo vya wale waliopoteza maisha yao kwa sababu ya dhambi zao. Na vifanyike kuwa mbao za kufuliwa ili viwe vifuniko vya madhabahu. Kwa kuwa wale watu walivitoa kwangu, kwa hiyo ni vitakatifu. Vitakuwa ishara ya uwepo wangu kwa wana wa Israeli.”
even the fire-pans of these men who have sinned at the cost of their lives, and let them be made beaten plates for a covering of the altar — for they are become holy, because they were offered before the LORD — that they may be a sign unto the children of Israel.'
39 Naye Eleazari yule kuhani akavichukue vile vyetezo vya shaba ambavyo vilikuwa vimetumiwa na wale watu walioungua, na vikafuliwa kuwa vifuniko vya madhbahu,
And Eleazar the priest took the brazen fire-pans, which they that were burnt had offered; and they beat them out for a covering of the altar,
40 ili kuwa ukumbusho kwa wana wa Israeli, ili kwamba asije akatokea mtu toka nje ya uzao wa Haruni akaja kutoa ubani kwa BWANA, ili wasije kuwa kama Kora na kundi lake— kama vile BWANA alivyoamuru kupitia kinywa cha Musa.
to be a memorial unto the children of Israel, to the end that no common man, that is not of the seed of Aaron, draw near to burn incense before the LORD; that he fare not as Korah, and as his company; as the LORD spoke unto him by the hand of Moses.
41 Lakini siku iliyofuata asubuhi watu wa Israeli wakamlalamikia Musa na Haruni. Nao walisema, “Umeua watu wa BWANA.”
But on the morrow all the congregation of the children of Israel murmured against Moses and against Aaron, saying: 'Ye have killed the people of the LORD.'
42 Kisha ikatokea, wakati watu walipokuwa wamekusanyika kinyume na Musa na Haruni, wakatazama kuielekea hema ya kukutania, na tazama lile wingu lilikuwa likiifunika. Utukufu wa BWANA ukaonekana,
And it came to pass, when the congregation was assembled against Moses and against Aaron, that they looked toward the tent of meeting; and, behold, the cloud covered it, and the glory of the LORD appeared.
43 Musa na Haruni wakaja mbele ya hema ya kukutania.
And Moses and Aaron came to the front of the tent of meeting.
44 Kisha BWANA akanena na Musa, akamwambia,
And the LORD spoke unto Moses, saying:
45 “Toka kati ya watu hawa ili niwaangamize haraka.” Musa na Haruni wakalala chini kifudifudi.
'Get you up from among this congregation, that I may consume them in a moment.' And they fell upon their faces.
46 Musa akamwambia Haruni, uchukue chetezo, na utie ndani moto kutoka madhabahuni, tia na uvumba ndani yake, upeleke haraka kwa watu, na ukafanye upatanisho kwao, kwa sababu hasira hii inatoka kwa BWANA. Tauni imeanza.”
And Moses said unto Aaron: 'Take thy fire-pan, and put fire therein from off the altar, and lay incense thereon, and carry it quickly unto the congregation, and make atonement for them; for there is wrath gone out from the LORD: the plague is begun.'
47 Kwa hiyo Haruni akafanya kama alivyoelekezwa na Musa. Akakimbia kati ya watu. na Tauni ilikuwa imeanza kuenea kati ya watu, kwa hiyo akaweka ndani yake uvumba na akafanya upatanisho wa watu.
And Aaron took as Moses spoke, and ran into the midst of the assembly; and, behold, the plague was begun among the people; and he put on the incense, and made atonement for the people.
48 Haruni akasimama kati kati ya zile maiti na watu hai; na kwa njia hii ile tauni ikazuiwa.
And he stood between the dead and the living; and the plague was stayed.
49 Idadi ya wale waliokuwa wamekufa kwa tauni walikuwa 14, 000, nje na wale waliokufa kutokana na swala la Kora.
Now they that died by the plague were fourteen thousand and seven hundred, besides them that died about the matter of Korah.
50 Haruni akarudi kwa Musa kwenye lango la hema ya kukutania, na ile tauni ikakoma.
And Aaron returned unto Moses unto the door of the tent of meeting, and the plague was stayed.

< Hesabu 16 >