< Hesabu 10 >

1 BWANA alinena na Musa, akasema,
And the LORD spake unto Moses, saying,
2 “tengenza tarumbeta mbili za fedha. Uzitengeneze kwa kufua hizo fedha. Utazitumia hizo tarumbeta kwa kuwaita watu waje pamoja na kwa kuwaita watu wote wakati wa kuondoka kwenye kambi zao.
Make thee two trumpets of silver; of beaten work shalt thou make them: and thou shalt use them for the calling of the congregation, and for the journeying of the camps.
3 Makuhani watapiga tarumbeta kwa ajili ya kuwaita watu wote mbele yako kwenye lango la hema ya kukutania.
And when they shall blow with them, all the congregation shall gather themselves unto thee at the door of the tent of meeting.
4 Kama makuhani watapiga tarumbeta moja tu, basi viongozi, vichwa koo za Israeli ndipo watakapokutana kwako.
And if they blow but with one, then the princes, the heads of the thousands of Israel, shall gather themselves unto thee.
5 Utakapopiga tarumbeta ya sauti kuu, ile kambi ya upande wa mashariki itaanza kusafiri.
And when ye blow an alarm, the camps that lie on the east side shall take their journey.
6 Nawe utakapopiga tarumeta kwa sauti kuu mara ya pili, ile kambi ya upande wa kusini wataanza kusafiri. Watapiga tarumbeta kwa sauti kuu ili kuanza safari yao.
And when ye blow an alarm the second time, the camps that lie on the south side shall take their journey: they shall blow an alarm for their journeys.
7 Watu wote watakapokutana pamoja, piga hizo tarumbeta lakini si kwa sauti kuu.
But when the assembly is to be gathered together, ye shall blow, but ye shall not sound an alarm.
8 Wana wa Haruni, makuhani, watapiga hizo tarumbeta. Huu ndio utakaokuwa utaratibu wa watu wako kwa vizazi vyote.
And the sons of Aaron, the priests, shall blow with the trumpets; and they shall be to you for a statute for ever throughout your generations.
9 Nanyi mtakapoenda vitani katika ardhi yenu dhidi ya maadui wenu wanaowakandamiza, ndipo mtakapotoa ishara ya sauti ya tarumbeta. Mimi, BWANA Mungu wako nitawaita kuwakumbuka na kuwaokoa kutoka kwa maadui wenu.
And when ye go to war in your land against the adversary that oppresseth you, then ye shall sound an alarm with the trumpets; and ye shall be remembered before the LORD your God, and ye shall be saved from your enemies.
10 Pia, wakati wa kusherehekea, sikukuu zenu za kawaida na katika miandamo ya miezi, mtapiga tarumbeta zenu kwa heshima ya sadaka zenu za kuteketezwa na kwa sadaka zenu za amani. Huu utakuwa ukumbusho wenu kwangu, Mungu wenu. Mimi ndimi BWANA Mungu wenu.”
Also in the day of your gladness, and in your set feasts, and in the beginnings of your months, ye shall blow with the trumpets over your burnt offerings, and over the sacrifices of your peace offerings; and they shall be to you for a memorial before your God: I am the LORD your God.
11 Katika siku ya ishrini, mwezi wa pili, mwaka wa pili, Lile wingu liliinuliwa toka masikani ya amri za maagano.
And it came to pass in the second year, in the second month, on the twentieth day of the month, that the cloud was taken up from over the tabernacle of the testimony.
12 Wana wa Israeli wakaendelea na safari yao toka jangwa la Sinai. Lile wingu likasimama kwenye jangwa la Parani.
And the children of Israel set forward according to their journeys out of the wilderness of Sinai; and the cloud abode in the wilderness of Paran.
13 Walifanya safari yao ya kwanza, kufuatia amri ya BWANA iliyotolewa kupitia kwa Musa.
And they first took their journey according to the commandment of the LORD by the hand of Moses.
14 Kambi ya mahali pa uzao wa Yuda iliondoka ya kanza, wakiondoa majeshi yao binafsi. Nashoni mwana wa Aminadabu ndiye aliyeongoza jeshi la Yuda.
And in the first [place] the standard of the camp of the children of Judah set forward according to their hosts: and over his host was Nahshon the son of Amminadab.
15 Nethaneli mwana wa Zuari aliongoza jeshi la kabila la uzao wa Isakari.
And over the host of the tribe of the children of Issachar was Nethanel the son of Zuar.
16 Eliabu mwana wa Heloni aliongoza jeshi la kabila la Zabuloni.
And over the host of the tribe of the children of Zebulun was Eliab the son of Helon.
17 Uzao wa Gerishoni na Merari, ambao walitunza masikani, na kuanza kusafiri.
And the tabernacle was taken down; and the sons of Gershon and the sons of Merari, who bare the tabernacle, set forward.
18 Baadaye Walifuata jeshi la mahali pa kambi ya Reubeni walianza safari yao. Elizuri mwana wa Shedeuri alliongoza jeshi la Reubebni.
And the standard of the camp of Reuben set forward according to their hosts: and over his host was Elizur the son of Shedeur.
19 Shelumieli mwana wa Zurishadai aliliongoza jeshi la kabila la uzao wa Simeoni.
And over the host of the tribe of the children of Simeon was Shelumiel the son of Zurishaddai.
20 Eliasafu mwana Deuli aliliongoza jeshi la kabila la uzao wa Gadi.
And over the host of the tribe of the children of Gad was Eliasaph the son of Deuel.
21 Kabila la Kohathi nalo lilianza safari. Wao walibebba vyombo vya mahali patakatifu. Wengine waliisimamisha masikani kabla ya Wakohathi kufika kambi inayofuata.
And the Kohathites set forward, bearing the sanctuary: and [the other] did set up the tabernacle against they came.
22 Majeshi ya kabila la uzao wa Efraimu ndio waliofuata. Elishama mwana wa Amihudi ndiye aliyeongoza jeshi la Efraimu.
And the standard of the camp of the children of Ephraim set forward according to their hosts: and over his host was Elishama the son of Ammihud.
23 Gamalieli mwana wa Pedazuri aliongoza jeshi la uzao wa Manase.
And over the host of the tribe of the children of Manasseh was Gamaliel the son of Pedahzur.
24 Abidani mwana wa Gidioni aliongoza jeshi la uzao wa kabila la Benjamini.
And over the host of the tribe of the children of Benjamin was Abidan the son of Gideoni.
25 Lile jeshi lililoweka kambi mahali pa bango la uzao wa Dani lilikuwa la mwisho kuondoka. Ahizeri mwana wa Amishadai ndiye aliyeongoza jeshi la Dani.
And the standard of the camp of the children of Dan, which was the rearward of all the camps, set forward according to their hosts: and over his host was Ahiezer the son of Ammishaddai.
26 Pagieli mwana wa Okirani aliongoza jeshi la wana wa uzao wa Asheri.
And over the host of the tribe of the children of Asher was Pagiel the son of Ochran.
27 Ahira mwana wa Enani aliongoza jeshi la uzao wa kabila ya Naftali.
And over the host of the tribe of the children of Naphtali was Ahira the son of Enan.
28 Hivi ndivyo majeshi ya wana wa Israeli yalivyosafiri.
Thus were the journeyings of the children of Israel according to their hosts; and they set forward.
29 Musa alinena na Hobibu mwana wa Reueli wa Kabila la Midiani. Reueli alikuwa baba mke wa Musa. Musa akanena na Hobibu akasema, “Tunasafiri kuelekea mahali ambapo BWANA ametuahidi. BWANA alisema kuwa, “Nitawapeni ninyi hilo eneo, 'Njoni pamoja nasi na tutawatendea mema. BWANA ameahidi kuwafanyia mema Waisraeli.”
And Moses said unto Hobab, the son of Reuel the Midianite, Moses’ father in law, We are journeying unto the place of which the LORD said, I will give it you: come thou with us, and we will do thee good: for the LORD hath spoken good concerning Israel.
30 Lakini Hobibu akmwambia Musa, “Sitaambatana nanyi.”
And he said unto him, I will not go; but I will depart to mine own land, and to my kindred.
31 Naye Musa akamjibu, “Tafadhali msituache. Mnajua jinsi ilivyo kuweka kambi jangwani. Tunaomba mtujali.
And he said, Leave us not, I pray thee; forasmuch as thou knowest how we are to encamp in the wilderness, and thou shalt be to us instead of eyes.
32 Kama mtaambatana nasi tutawatendea mema sawa na jinsi BWANA anavyotutendea.”
And it shall be, if thou go with us, yea, it shall be, that what good soever the LORD shall do unto us, the same will we do unto thee.
33 Walisafiri kutoka mlima wa BWANA kwa siku tatu. Sanduku la agano la BWANA liliwatangulia kwa siku tatu ili kupata mahali pa kupumzika.
And they set forward from the mount of the LORD three days’ journey; and the ark of the covenant of the LORD went before them three days’ journey, to seek out a resting place for them.
34 Wingu la BWANA lilikuwa juu yao muda wote wa mchana walipokuwa safarini.
And the cloud of the LORD was over them by day, when they set forward from the camp.
35 Kila hilo sanduku liliposafiri kwenda mbele, Musa alisema, “Inuka BWANA, Uwatawanye maadui wako. Uwafanye wale wanaokuchukia kukukimbia.”
And it came to pass, when the ark set forward, that Moses said, Rise up, O LORD, and let thine enemies be scattered; and let them that hate thee flee before thee.
36 Na kila lile sanduku liliposimama, Musa alisema, “BWANA uwarudie, hawa Waisraeli makumi elfu.”
And when it rested, he said, Return, O LORD, unto the ten thousands of the thousands of Israel.

< Hesabu 10 >