< Torati 1 >

1 Haya ni maneno ambayo Musa aliyasema kwa Israeli wote ng'ambo ya jangwa la Yordani, katika tambarare ya mto wa Yordani juu ya Suph, katikati mwa Paran, Topheli, Laban, Hazeroth, na Di Zahab.
These be the words which Moses spake unto all Israel beyond Jordan in the wilderness, in the Arabah over against Suph, between Paran, and Tophel, and Laban, and Hazeroth, and Di-zahab.
2 Ni safari ya siku kumi na moja toka Horabu kupitia njia ya mlima wa Seir kwenda Kadeshi Barnea.
It is eleven days’ [journey] from Horeb by the way of mount Seir unto Kadesh-barnea.
3 Ilitokea kwenye mwaka wa nne, mwezi wa kumi na moja, siku ya kwanza ya mwezi, Musa alizungumza kwa watu wa Israeli, kuambia yote yale Yahwe aliyomwamuru kuhusu wao.
And it came to pass in the fortieth year, in the eleventh month, on the first day of the month, that Moses spake unto the children of Israel, according unto all that the LORD had given him in commandment unto them;
4 Hii ilikuwa baada ya Yahwe kumvamia Sihoni mfalme wa Amoria, ambaye aliishi huko Heshboni, na Ogi mfalme wa Bashani, ambaye aliishi huko Ashtarothi ya Edrei.
after he had smitten Sihon the king of the Amorites, which dwelt in Heshbon, and Og the king of Bashan, which dwelt in Ashtaroth, at Edrei:
5 Ng'ambo ya Yordani, katika nchi ya Moabu, Musa alianza kutangaza maelekezo haya, akisema,
beyond Jordan, in the land of Moab, began Moses to declare this law, saying,
6 “Yahwe Mungu wetu alisema nasi huko Horebu, akisema, umeishi vya kutosha katika milima ya nchi hii.
The LORD our God spake unto us in Horeb, saying, Ye have dwelt long enough in this mountain:
7 Geuka na uanze safari yako, na uende kwenye nchi ya milima ya Amorites, na kwenye maeneo yote karibu na tambarare ya mto Yordani, katika nchi ya milima, na nyanda za chini, huko Negev, na pwani - nchi ya Wakanani na huko Lebanoni mbali ya mto mkuu wa Euphratesi.
turn you, and take your journey, and go to the hill country of the Amorites, and unto all [the places] nigh thereunto, in the Arabah, in the hill country, and in the lowland, and in the South, and by the sea shore, the land of the Canaanites, and Lebanon, as far as the great river, the river Euphrates.
8 Tazama, nimetenga nchi kwa ajili yako, nenda ndani na umiliki nchi ambayo Yahwe aliapa kwa baba zako, Ibrahimu, Isaka na Yakobo, kuwapa na uzao wao baada yao.
Behold, I have set the land before you: go in and possess the land which the LORD sware unto your fathers, to Abraham, to Isaac, and to Jacob, to give unto them and to their seed after them.
9 Nilisema nawe kwa wakati huo, nikisema, siwezi nikakubeba peke yangu,
And I spake unto you at that time, saying, I am not able to bear you myself alone:
10 Yahwe Mungu wako amekuzidisha, na tazama, leo umekuwa umati wa nyota angani.
The LORD your God hath multiplied you, and, behold, ye are this day as the stars of heaven for multitude.
11 Yahwe aweza, Mungu wa baba zako, kukufanya wewe mara elfu moja zaidi ya ulivyo, na kukubariki, kama alivyokuahidi!
The LORD, the God of your fathers, make you a thousand times so many more as ye are, and bless you, as he hath promised you!
12 Lakini inawezekanaje mimi peke yangu kubeba shehena zako, mizigo yako, na migogoro yako?
How can I myself alone bear your cumbrance, and your burden, and your strife?
13 Chukua wanaume wa hekima, wanaume waelewa, na wanaume walio na sifa nzuri toka kila kabila, nitawafaya kuwa vichwa juu yenu.
Take you wise men, and understanding, and known, according to your tribes, and I will make them heads over you.
14 Mlinijibu na kusema, 'Jambo ulilolisema ni zuri kwetu kufanya.'
And ye answered me, and said, The thing which thou hast spoken is good [for us] to do.
15 Kwa hiyo nilichukua vichwa vya makabila yenu, wanaume wa hekima, na wanaume wenye sifa nzuri, na nikawafanya kuwa vichwa juu yenu, jemedari kwa elfu, jemedari kwa hamsini, jemedari kwa kumi, na maakida, kabila kwa kabila.
So I took the heads of your tribes, wise men, and known, and made them heads over you, captains of thousands, and captains of hundreds, and captains of fifties, and captains of tens, and officers, according to your tribes.
16 Niliwaamuru waamuzi wenu kwa wakati huo, kusema, 'Zikiliza mabishano kati ya ndugu zenu, na muhukumu ya haki kati ya ndugu na ndugu zake, na mgeni aliye pamoja naye.
And I charged your judges at that time, saying, Hear [the causes] between your brethren, and judge righteously between a man and his brother, and the stranger that is with him.
17 Hamtaonesha upendeleo kwa yeyote katika mgogoro, mtasikia madogo na makubwa pia. Hamtaogopa uso wa mtu, kwa kuwa hukumu ni ya Mungu. Migogoro iliyo migumu kwenu, mtaniletea mimi, na mimi nitaisikiliza.
Ye shall not respect persons in judgment; ye shall hear the small and the great alike; ye shall not be afraid of the face of man; for the judgment is God’s: and the cause that is too hard for you ye shall bring unto me, and I will hear it.
18 Niliwaamuru kwa wakati huo mambo yote mtakayofanya.
And I commanded you at that time all the things which ye should do.
19 Tulisafiri toka Horebu na kwenda kupitia jangwa lile kubwa lote na lenye kutisha lile mliloliona, katika njia yetu kuelekea nchi ya milima huko Amorites, kama Yahwe Mungu wetu alivyotuamuru sisi, na tukaja Kadeshi ya Barnea.
And we journeyed from Horeb, and went through all that great and terrible wilderness which ye saw, by the way to the hill country of the Amorites, as the LORD our God commanded us; and we came to Kadesh-barnea.
20 Niliwambia, mmekuja kwenye nchi ya milima ya Amorites, ambayo Yahwe Mungu wetu anatupa sisi.
And I said unto you, Ye are come unto the hill country of the Amorites, which the LORD our God giveth unto us.
21 Tazama, Yahwe Mungu wenu amekwisha weka nchi mbele yenu; nenda juu, muimiliki, kama Yahwe, Mungu wa baba zenu, amekwisha zungumza nanyi, msiogope wala kukata tamaa.
Behold, the LORD thy God hath set the land before thee: go up, take possession, as the LORD, the God of thy fathers, hath spoken unto thee; fear not, neither be dismayed.
22 Kila moja wenu alikuja kwangu na kusema, 'Basi tutume watu mbele yetu, ili kwamba waweze kupepeleza nchi kwa ajili yetu, na kutuletea sisi neno kuhusiana na njia ya wapi tuvamie, na kuhusiana na miji tutakayoingia.
And ye came near unto me every one of you, and said, Let us send men before us, that they may search the land for us, and bring us word again of the way by which we must go up, and the cities unto which we shall come.
23 Shauri hilo lilinibariki mimi, 'Nilichukua watu kumi na mbili kutoka kwenu, mtu moja kwa kila kabila.
And the thing pleased me well: and I took twelve men of you, one man for every tribe:
24 Waligeuka na kwenda juu ya nchi ya milima, kufika kwenye bonde la Eshcol na kufanya upepelezi wa kina.
and they turned and went up into the mountain, and came unto the valley of Eshcol, and spied it out.
25 Walichukua baadhi ya mazao ya ardhi mikononi mwao na kuleta kwetu, Pia walileta neno na kusema, 'Ni nchi nzuri ambayo Yahweh Mungu wetu anatupa sisi'
And they took of the fruit of the land in their hands, and brought it down unto us, and brought us word again, and said, It is a good land which the LORD our God giveth unto us.
26 Bado mlikataa kushambulia, lakini mliasi dhidi ya amri ya Yahwe Mungu wenu.
Yet ye would not go up, but rebelled against the commandment of the LORD your God:
27 Mlilalamika katika mahema yenu na kusema, “Ni kwa sababu Yahwe alituchukia sisi kwa kuwa ametutoa katika nchi ya Misri, kuteweka katika mikono ya Amorites kutuangamiza.
and ye murmured in your tents, and said, Because the LORD hated us, he hath brought us forth out of the land of Egypt, to deliver us into the hand of the Amorites, to destroy us.
28 Tuende wapi sasa? Ndugu zetu wamefanya mioyo yetu kuyeyuka, kusema, Hao watu ni wakubwa na warefu zaidi yetu, miji yao ni mikubwa na imeimarishwa kwenda mbinguni; zaidi ya yote, tumewaona wana wa Anakim huko”
Whither are we going up? our brethren have made our heart to melt, saying, The people is greater and taller than we; the cities are great and fenced up to heaven; and moreover we have seen the sons of the Anakim there.
29 Kisha nikasema nao, msitishwe wala msiwaogope.
Then I said unto you, Dread not, neither be afraid of them.
30 Yahwe Mungu wenu, ambaye aenda mbele yenu, atawapigania, kama yote aliyofanya kwa ajili yenu huko Misri mbele ya macho yenu,
The LORD your God who goeth before you, he shall fight for you, according to all that he did for you in Egypt before your eyes;
31 na pia katika jangwa, ambapo mmekwisha muona Yahwe Mungu wenu jinsi alivyowabeba, kama mtu abebavyo mtoto wake, kokote mlikoenda mpaka kufika hapa.'
and in the wilderness, where thou hast seen how that the LORD thy God bare thee, as a man doth bear his son, in all the way that ye went, until ye came unto this place.
32 Bado licha ya neno hili hakumwamini Yahwe Mungu wenu,
Yet in this thing ye did not believe the LORD your God,
33 aliyeenda mbele yenu kwenye njia kutafuta eneo kwa ajili yenu kuweka kambi, katika moto kwa usiku, katika mawingu kwa mchana.
who went before you in the way, to seek you out a place to pitch your tents in, in fire by night, to shew you by what way ye should go, and in the cloud by day.
34 Yahwe alisikia sauti ya maneno yenu na alikasirika; aliapa na kusema,
And the LORD heard the voice of your words, and was wroth, and sware, saying,
35 Hakika hakuna mmoja ya hawa watu wa kizazi hiki kiovu wataona nchi nzuri ambayo niliapa kuwapa babu zao,
Surely there shall not one of these men of this evil generation see the good land, which I sware to give unto your fathers,
36 kasoro Kalebu mwana wa Jephuneeh; yeye ataiona. Yeye nitampa nchi ambayo amekwisha kuikanyanga, na watoto wake, kwa sababu alimfuata Yahwe kwa ukamilifu.'
save Caleb the son of Jephunneh, he shall see it; and to him will I give the land that he hath trodden upon, and to his children: because he hath wholly followed the LORD.
37 Pia Yahweh alinikasirikia mimi kwa sababu yenu, kusema, 'Wewe pia hautaingia huko,
Also the LORD was angry with me for your sakes, saying, Thou also shalt not go in thither:
38 Yoshua mwana wa Nuh, ambaye amesimama mbele yako, yeye ataingia, mtie moyo, kwani yeye atawaongoza Israeli kuimiliki.
Joshua the son of Nun, which standeth before thee, he shall go in thither: encourage thou him; for he shall cause Israel to inherit it.
39 Zaidi ya yote, watoto wenu wadogo, ambao mlisema watakuwa waathirika, ambao leo hawana elimu ya uzuri au ubaya-wataenda ndani huko. Wao nitawapa nchi hiyo, na wataimiliki.
Moreover your little ones, which ye said should be a prey, and your children, which this day have no knowledge of good or evil, they shall go in thither, and unto them will I give it, and they shall possess it.
40 Lakini ninyi, geuka na muuanza safari kwenda jangwani kwa kuambaa njia ya bahari ya mianzi'.
But as for you, turn you, and take your journey into the wilderness by the way to the Red Sea.
41 Kisha mlinijibu na kusema kwangu, 'Tumetenda dhambi dhidi ya Yahwe, tutaenda juu na kupigana, tutafuata yote ambayo Yahwe Mungu wetu ametuamuru sisi kufanya'. Kila mtu miongoni mwenu aliweka silaha za vita, na mlikuwa tayari kuvamia nchi ya milima.
Then ye answered and said unto me, We have sinned against the LORD, we will go up and fight, according to all that the LORD our God commanded us. And ye girded on every man his weapons of war, and were forward to go up into the mountain.
42 Yahwe alisema nami, 'Waambie, msivamie na kupigana, kwa kuwa sitakuwa pamoja nanyi, na mtashindwa na adui zenu'.
And the LORD said unto me, Say unto them, Go not up, neither fight; for I am not among you; lest ye be smitten before your enemies.
43 Nilizungumza nanyi kwa njia hii, lakini hamkunisikiliza, Mliasi dhidi ya amri ya Yahwe, mlikuwa wenye kiburi na mlivamia nchi ya milima.
So I spake unto you, and ye hearkened not; but ye rebelled against the commandment of the LORD, and were presumptuous, and went up into the mountain.
44 Lakini Amorites, ambayo waliishi katika nchi hiyo ya milima, walitoka dhidi yenu na kuwafukuza kama nyuki, na kuwapiga chini huko Seir, mbali kama Hormah.
And the Amorites, which dwelt in that mountain, came out against you, and chased you, as bees do, and beat you down in Seir, even unto Hormah.
45 Mlirudi na kulia mbele ya Yahwe; lakini Yahwe hakusikiliza sauti zenu, wala hakuwa makini kwenu.
And ye returned and wept before the LORD; but the LORD hearkened not to your voice, nor gave ear unto you.
46 Kwa hiyo mlibaki Kadeshi siku nyingi, siku zote mlibaki huko.
So ye abode in Kadesh many days, according unto the days that ye abode [there].

< Torati 1 >