< Marko 3 >

1 Na tena aliingia ndani ya sinagogi na mle palikuwa na mtu mwenye mkono uliopooza.
Et il entra encore dans la synagogue; et il y avait là un homme qui avait la main desséchée.
2 Baadhi ya watu walikuwa wakimfuatilia kwa ukaribu kuona kama atamponya siku ya Sabato ili kwamba wamshitaki.
Et ils l’observaient [pour voir] s’il le guérirait le jour de sabbat, afin de l’accuser.
3 Yesu alimwambia mtu mwenye mkono uliopooza, “Inuka na usimame katikati ya umati huu.”
Et il dit à l’homme qui avait la main desséchée: Lève-toi là devant tous.
4 Kisha akawaambia watu, “Je ni halali kutenda tendo jema siku ya Sabato au kutenda yasiyo haki; kuokoa maisha, au kuua?” Lakini walibaki kimya.
Et il leur dit: Est-il permis de faire du bien le jour de sabbat, ou de faire du mal? de sauver la vie, ou de tuer? Mais ils gardaient le silence.
5 Akawaangalia kwa hasira, akihuzunika kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao, na akamwambia yule mtu, “Nyoosha mkono wako”. Akaunyoosha na Yesu akamponya mkono wake.
Et les ayant regardés à l’entour avec colère, étant attristé de l’endurcissement de leur cœur, il dit à l’homme: Étends ta main. Et il l’étendit, et sa main fut rétablie.
6 Mafarisayo wakaenda nje na mara wakafanya njama pamoja na Maherode dhidi yake ili kumuua.
Et les pharisiens, sortant aussitôt avec les hérodiens, tinrent conseil contre lui pour le faire périr.
7 Kisha Yesu, pamoja na wanafunzi wake, walienda baharini, na umati mkubwa wa watu uliwafuata ukitokea Galilaya na Uyahudi
Et Jésus se retira avec ses disciples vers la mer; et une grande multitude le suivit de la Galilée, et de la Judée,
8 na kutoka Yerusalemu na kutoka Idumaya na mbele ya Yorodani na jirani ya Tiro na Sidoni, umati mkubwa, uliposikia kila kitu alichokuwa anakifanya, walikuja kwake.
et de Jérusalem, et de l’Idumée, et de par-delà le Jourdain. Et ceux des environs de Tyr et de Sidon, une grande multitude, ayant entendu les choses qu’il faisait, vinrent vers lui.
9 Na aliwaambia wanafunzi wake kuandaa mtubwi mdongo kwa ajili yake kwa sababu ya umati, ili kwamba wasije wakamsonga.
Et il dit à ses disciples qu’un petit bateau soit là à sa disposition, à cause de la foule, afin qu’elle ne le presse pas;
10 Kwa kuwa aliponya wengi, ili kila mtu aliyekuwa na mateso alikuwa na shauku ya kumfikia ili amguse.
car il en guérit beaucoup, de sorte que tous ceux qui étaient affligés de quelque fléau se jetaient sur lui afin de le toucher.
11 Popote roho wachafu walipomwona, walianguka chini mbele yake na kulia, na walisema, “Wewe ni Mwana wa Mungu”.
Et les esprits immondes, quand ils le voyaient, se jetaient devant lui et s’écriaient, disant: Tu es le Fils de Dieu.
12 Aliwaamuru kwa msisitizo wasifanye ajulikane.
Et il leur défendait très expressément de le faire connaître.
13 Alienda juu ya mlima, na akawaita aliowataka, na wakaenda kwake.
Et il monte sur une montagne, et il appelle ceux qu’il voulait; et ils vinrent à lui;
14 Akawachagua kumi na wawili (aliowaita mitume), ili kwamba wawe pamoja naye na aweze kuwatuma kuhubiri,
et il en établit douze pour être avec lui, et pour les envoyer prêcher,
15 na kuwa na mamlaka ya kutoa mapepo.
et pour avoir autorité [de guérir les maladies et] de chasser les démons;
16 Na akawachagua kumi na wawili: Simoni, aliyempa jina la Petro,
et il surnomma Simon, Pierre;
17 Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohana ndugu yake Yakobo, aliyepewa jina la Bonagesi, hao ni, wana wa ngurumo,
et Jacques le [fils] de Zébédée et Jean le frère de Jacques, et il les surnomma Boanergès, ce qui est: fils de tonnerre;
18 na Andrea, Filipo, Bartholomayo, Mathayo, Tomaso, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkananayo,
et André, et Philippe, et Barthélemy, et Matthieu, et Thomas, et Jacques le [fils] d’Alphée, et Thaddée, et Simon le Cananéen,
19 na Yuda Iskariote, ambaye atamsaliti.
et Judas Iscariote, qui aussi le livra.
20 Kisha alienda nyumbani, na umati wa watu wakaja pamoja tena, hata wasiweze kula hata mkate.
Et ils viennent à la maison; et la foule s’assemble de nouveau, en sorte qu’ils ne pouvaient pas même manger leur pain.
21 Familia yake waliposikia habari hiyo, walienda kumkamata, kwani walisema, “Amerukwa na akili”.
Et ses proches, ayant entendu cela, sortirent pour se saisir de lui; car ils disaient: Il est hors de sens.
22 Waandishi waliokuja kutoka Yerusalemu walisema, “Amepagawa na Beelzebuli,” na, “Kwa mtawala wa mapepo anatoa mapepo”.
Et les scribes qui étaient descendus de Jérusalem, dirent: Il a Béelzébul; et: Par le chef des démons, il chasse les démons.
23 Yesu aliwaita kwake na kusema nao kwa mifano, “Jinsi gani Shetani aweza kumtoa Shetani?
Et les ayant appelés, il leur dit par des paraboles: Comment Satan peut-il chasser Satan?
24 Kama ufalme ukigawanyika wenyewe, ufalme huo hauwezi kusimama.
Et si un royaume est divisé contre lui-même, ce royaume-là ne peut pas subsister.
25 Kama nyumba ikigawanyika yenyewe, nyumba hiyo haiwezi kusimama.
Et si une maison est divisée contre elle-même, cette maison-là ne peut pas subsister.
26 Kama Shetani atainuka kinyume chake mwenyewe na kugawanyika, hawezi kusimama, na atakuwa amefika mwisho wake.
Et si Satan s’élève contre lui-même et est divisé, il ne peut pas subsister, mais il vient à sa fin.
27 Lakini hakuna hata mmoja awezaye kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuiba vitu vyake bila kumfunga mwenye nguvu kwanza, na kisha kukusanya kilichomo nyumbani.
Nul ne peut entrer dans la maison de l’homme fort, et piller ses biens, si premièrement il n’a lié l’homme fort; et alors il pillera sa maison.
28 Kweli nawambieni, dhambi zote za wana wa watu zitasamehewa, pamoja na kufuru ambazo wanatamka,
En vérité, je vous dis que tous les péchés seront pardonnés aux fils des hommes, et les paroles injurieuses, quelles qu’elles soient, par lesquelles ils blasphèment;
29 lakini yeyote atakaye mkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa kamwe, bali ana hatia ya dhambi ya milele”. (aiōn g165, aiōnios g166)
mais quiconque proférera des paroles injurieuses contre l’Esprit Saint n’aura jamais de pardon; mais il est passible du jugement éternel. (aiōn g165, aiōnios g166)
30 Yesu alilisema hili kwa sababu walikuwa wakisema, “Ana roho chafu”.
C’était parce qu’ils disaient: Il a un esprit immonde.
31 Kisha mama yake na ndugu zake walikuja na kusimama nje. Wakamtuma mtu, kumwita.
Ses frères et sa mère donc viennent; et se tenant dehors, ils l’envoyèrent appeler;
32 Na umati wa watu uliokuwa umekaa karibu naye wakamwambia, “mama yako na ndugu zako wako nje, na wanakutafuta wewe”.
et la foule était assise autour de lui. Et on lui dit: Voici, ta mère et tes frères, là dehors, te cherchent.
33 Aliwajibu, “Ni nani mama yangu na ndugu zangu?”
Et il leur répondit, disant: Qui est ma mère, ou [qui sont] mes frères?
34 Aliwaangalia waliokuwa wamekaa wamemzunguka, na akasema, “Tazama, hawa ni mama zangu na ndugu zangu!
Et regardant tout à l’entour ceux qui étaient assis autour de lui, il dit: Voici ma mère et mes frères;
35 Yeyote afanyaye mapenzi ya Mungu, mtu huyo ni ndugu yangu, na dada yangu, na mama yangu”.
car quiconque fera la volonté de Dieu, celui-là est mon frère, et ma sœur, et ma mère.

< Marko 3 >