< Marko 2 >

1 Aliporudi Kaperinaumu baada ya siku chache, ilisikika kwamba alikuwa nyumbani.
Et il entra de nouveau dans Capernaüm, quelques jours après, et on entendit dire qu’il était à la maison.
2 Watu wengi sana walikuwa wamekusanyika pale na haikuwepo nafasi tena, hata ile ya pale mlangoni, na Yesu alisema neno kwao.
Et aussitôt beaucoup de gens s’y assemblèrent, de sorte qu’il ne se trouva plus de place, même auprès de la porte; et il leur annonçait la parole.
3 Kisha baadhi ya watu walikuja kwake waliomleta mtu aliyekuwa amepooza; watu wanne walikuwa wamembeba.
Et des gens viennent à lui, amenant un paralytique porté par quatre personnes.
4 Wakati waliposhindwa kumkaribia kwa sababu ya umati wa watu, waliondoa paa juu ya mahali pale alipokuwa. Na walipokuwa wamekwishatoboa tundu, walishusha kitanda ambacho mtu aliyepooza alikuwa amelala.
Et ne pouvant s’approcher de lui, à cause de la foule, ils découvrirent le toit [du lieu] où il était; et l’ayant percé, ils descendirent le petit lit sur lequel le paralytique était couché.
5 Alipoiona imani yao, Yesu alimwambia mtu aliyepooza, “mwanangu, dhambi zako zimesamehewa.”
Et Jésus, voyant leur foi, dit au paralytique: [Mon] enfant, tes péchés sont pardonnés.
6 Lakini baadhi ya waandishi wale waliokuwa wamekaa pale walijihoji mioyoni mwao,
Et il y avait là quelques-uns des scribes, assis et raisonnant dans leurs cœurs:
7 “Anawezaje mtu huyu kusema hivi? Anakufuru! Nani awezaye kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake?”
Pourquoi celui-ci parle-t-il ainsi? Il blasphème. Qui peut pardonner les péchés, sinon un [seul], Dieu?
8 Mara Yesu alijua rohoni mwake walichokuwa wakifikiri miongoni mwao wenyewe. Aliwaambia, “Kwa nini mnafikiri hivi mioyoni mwenu?
Et aussitôt Jésus, connaissant dans son esprit qu’ils raisonnaient ainsi en eux-mêmes, leur dit: Pourquoi faites-vous ces raisonnements dans vos cœurs?
9 Lipi ni jepesi zaidi kusema kwa mtu aliyepooza, 'Dhambi zako zimesamehewa' au kusema 'Simama, chukua kitanda chako, na utembee?'
Lequel est le plus facile, de dire au paralytique: [Tes] péchés te sont pardonnés; ou de dire: Lève-toi, prends ton petit lit, et marche?
10 Lakini ili wapate kujua ya kuwa Mwana wa Adamu ana mamlaka ya kusamehe dhambi katika dunia, alimwambia yule aliyepooza,
Or, afin que vous sachiez que le fils de l’homme a le pouvoir sur la terre de pardonner les péchés (il dit au paralytique):
11 “Nakuambia wewe, inuka, chukua mkeka wako, na uende nyumbani kwako.”
Je te dis, lève-toi, prends ton petit lit, et va dans ta maison.
12 Alisimama na mara moja akachukua mkeka wake, na alikwenda nje ya nyumba mbele ya kila mtu, hivyo wote walishangaa na walimpa Mungu utukufu, na wakasema “Kamwe, hatujawahi kuona jambo kama hili.”
Et il se leva aussitôt, et ayant pris son petit lit, il sortit en la présence de tous; de sorte qu’ils en furent tous étonnés et qu’ils glorifiaient Dieu, disant: Nous n’avons jamais vu pareille chose.
13 Alienda tena kando ya ziwa, na umati wote wa watu walikuja kwake, na akawafundisha.
Et il sortit encore et longea la mer; et toute la foule venait à lui, et il les enseignait.
14 Alipokuwa akipita alimwona Lawi mwana wa Alfayo ameketi kwenye sehemu ya kukusanyia kodi na akamwambia, “Nifuate.” Alisimama na kumfuata.
Et en passant, il vit Lévi le [fils] d’Alphée assis au bureau de recette, et il lui dit: Suis-moi. Et se levant, il le suivit.
15 Na wakati Yesu alipokuwa akipata chakula katika nyumba ya Lawi, wakusanya kodi wengi na watu wenye dhambi walikuwa wakila na Yesu na wanafunzi wake, kwa kuwa walikuwa wengi nao walimfuata.
Et il arriva, comme il était à table dans sa maison, que beaucoup de publicains et de pécheurs aussi se trouvèrent à table avec Jésus et ses disciples; car ils étaient nombreux, et ils le suivaient.
16 Wakati waandishi, ambao walikuwa Mafarisayo, walipoona kwamba Yesu alikuwa akila na watu wenye dhambi na wakusanya kodi, waliwaambia wanafunzi wake, “Kwa nini anakula na wakusanya kodi na watu wenye dhambi?”
Et les scribes et les pharisiens, le voyant manger avec les publicains et les pécheurs, dirent à ses disciples: Pourquoi mange-t-il et boit-il avec les publicains et les pécheurs?
17 Wakati Yesu aliposikia hivi aliwaambia, “Watu walio na afya katika mwili hawamhitaji tabibu; ni watu wagonjwa pekee ndio wanamhitaji. Sikuja kuwaita watu wenye haki, lakini watu wenye dhambi.”
Et Jésus, l’ayant entendu, leur dit: Ceux qui sont en bonne santé n’ont pas besoin de médecin, mais ceux qui se portent mal; je ne suis pas venu appeler des justes, mais des pécheurs.
18 Wanafunzi wa Yohana na Mafarisayo walikuwa wakifunga. Na baadhi ya watu walikuja kwake na kumwambia, “Kwa nini wanafunzi wa Yohana na mafarisayo hufunga, lakini wanafunzi wako hawafungi?
Et les disciples de Jean et les pharisiens jeûnaient; et ils viennent et lui disent: Pourquoi les disciples de Jean et ceux des pharisiens jeûnent-ils, mais tes disciples ne jeûnent pas?
19 Yesu aliwaambia, “Je waliohudhuria harusini wanaweza kufunga wakati bwana harusi bado akiwa pamoja nao? Kwa vyovyote bwana harusi akiwa bado yuko pamoja nao hawawezi kufunga.”
Et Jésus leur dit: Les fils de la chambre nuptiale peuvent-ils jeûner pendant que l’époux est avec eux? Aussi longtemps qu’ils ont l’époux avec eux, ils ne peuvent pas jeûner.
20 Lakini siku zitakuja wakati bwana harusi atakapoondolewa kwao, na katika siku hizo wao watafunga.
Mais des jours viendront, lorsque l’époux leur aura été ôté; et alors ils jeûneront en ce jour-là.
21 Hakuna mtu ashonaye kipande kipya cha nguo kwenye vazi kuukuu, vinginevyo kiraka kitabanduka kutoka katika hilo, kipya kubanduka kutoka katika kikuukuu, na kutakuwepo mpasuko mbaya.
Personne ne coud un morceau de drap neuf à un vieil habit; autrement la pièce neuve emporte [une partie] du vieil [habit], et la déchirure en devient plus mauvaise.
22 Hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba vikuukuu, vinginevyo divai itavipasua viriba na vyote viwili divai na viriba vitapotea. Badala yake, weka divai mpya katika viriba vipya.”
Et personne ne met du vin nouveau dans de vieilles outres; autrement le vin rompt les outres, et le vin se répand, et les outres sont perdues; mais le vin nouveau doit être mis dans des outres neuves.
23 Katika siku ya Sabato Yesu alipita kwenye baadhi ya mashamba, na wanafunzi wake walianza kuchukua baadhi ya masuke ya ngano.
Et il arriva qu’il passait par les blés en un jour de sabbat; et ses disciples, chemin faisant, se mirent à arracher des épis.
24 Na Mafarisayo walimwambia, “Tazama, kwa nini wanafanya kitu ambacho ni kinyume cha sheria katika siku ya Sabato?”
Et les pharisiens lui dirent: Voici, pourquoi font-ils, le jour de sabbat, ce qui n’est pas permis?
25 Aliwaambia, “Hamkusoma kile alichofanya Daudi alipokuwa katika uhitaji na njaa—yeye pamoja na watu waliokuwa pamoja naye?
Et lui leur dit: N’avez-vous jamais lu ce que fit David quand il fut dans le besoin et qu’il eut faim, lui et ceux qui étaient avec lui,
26 Jinsi alivyoenda katika nyumba ya Mungu wakati Abiathari alipokuwa kuhani mkuu na akala mkate uliowekwa mbele—ambao ilikuwa kinyume cha sheria kwa mtu yeyote kula isipokuwa makuhani—na aliwapa hata baadhi ya wale waliokuwa pamoja naye?”
comment, au [titre] “Abiathar, souverain sacrificateur”, il entra dans la maison de Dieu, et mangea les pains de proposition, qu’il n’est pas permis de manger, sinon aux sacrificateurs, et en donna aussi à ceux qui étaient avec lui?
27 Yesu alisema, “Sabato ilifanywa kwa ajili ya mwanadamu, siyo mwanadamu kwa ajili ya Sabato.
Et il leur dit: Le sabbat a été fait pour l’homme, non pas l’homme pour le sabbat;
28 Kwa hiyo, Mwana wa Adamu ni Bwana, hata kwa Sabato.”
de sorte que le fils de l’homme est seigneur aussi du sabbat.

< Marko 2 >