< Marko 12 >

1 Kisha Yesu alianza kuwafundisha kwa mifano. Akasema, “Mtu alipanda shamba la mizabibu, akalizungushia uzio, na akachimba shimo la kusindika mvinyo. Akajenga mnara na kisha akalipangisha shamba la mizabibu kwa wakulima wa mizabibu. Kisha alisafiri safari ya mbali.
Il se mit à leur parler en paraboles. « Un homme planta une vigne, l'entoura d'une haie, creusa une fosse pour le pressoir, construisit une tour, la loua à un fermier et s'en alla dans un autre pays.
2 Wakati ulipofika, alimtuma mtumishi kwa wakulima wa mizabibu kupokea kutoka kwao baadhi ya matunda ya shamba la mizabibu.
Le moment venu, il envoya un serviteur chez le fermier pour lui demander sa part du fruit de la vigne.
3 Lakini walimkamata, wakampiga, na wakamfukuza bila chochote.
On le prit, on le battit et on le renvoya à vide.
4 Akamtuma kwao mtumishi mwingine, wakamjeruhi kichwani na kumtendea mambo ya aibu.
Il leur envoya de nouveau un autre serviteur; ils lui jetèrent des pierres, le blessèrent à la tête et le renvoyèrent honteusement traité.
5 Bado alimtuma mwingine, na huyu mmoja walimwua. Waliwatendea wengine wengi mambo kama hayo hayo, wakiwapiga na wengine kuwaua.
Il en envoya encore un autre, et ils le tuèrent, ainsi que beaucoup d'autres, battant les uns et tuant les autres.
6 Alikuwa bado na mtu mmoja zaidi wa kumtuma, mwana mpendwa. Naye alikuwa wa mwisho aliyetumwa kwao. Akisema, “Watamheshimu mwanangu”.
Il lui restait un fils bien-aimé, qu'il envoya le dernier, en disant: « Ils respecteront mon fils ».
7 Lakini wapangaji walisemezana wao kwa wao, “Huyu ndiye mrithi. Njoni, hebu na tumwue, na urithi utakuwa wetu.”
Mais les paysans dirent entre eux: « C'est lui l'héritier. Venez, tuons-le, et l'héritage sera à nous.
8 Walimvamia, wakamuua na kumtupa nje ya shamba la mizabibu.
Ils le prirent, le tuèrent, et le chassèrent de la vigne.
9 Kwa hiyo, Je! Atafanya nini mmiliki wa shamba la mizabibu? Atakuja na kuwaangamiza wakulima wa mizabibu na atalikabidhi shamba la mizabibu kwa wengine.
Que fera donc le maître de la vigne? Il viendra faire périr les vignerons, et il donnera la vigne à d'autres.
10 Hamjapata kusoma andiko hili? “Jiwe ambalo wajenzi walilikataa, limekuwa jiwe la pembeni.
N'avez-vous même pas lu cette Écriture? « La pierre que les bâtisseurs ont rejetée a été nommé à la tête du coin.
11 Hili lilitoka kwa Bwana, na ni la ajabu machoni petu.”
Cela vient de l'Éternel. C'est merveilleux à nos yeux »?
12 Walitafuta kumkamata Yesu, Lakini waliwaogopa makutano, kwani walijua kuwa alikuwa amenena mfano huo dhidi yao. Hivyo walimwacha na wakaenda zao.
Ils cherchaient à s'emparer de lui, mais ils craignaient la foule, car ils savaient qu'il avait prononcé la parabole contre eux. Ils le laissèrent et s'en allèrent.
13 Kisha wakawatuma baadhi ya mafarisayo na maherodia kwake ili kumtega kwa maneno.
Ils envoyèrent vers lui quelques-uns des pharisiens et des hérodiens, afin qu'ils le piègent par des paroles.
14 Walipofika, wakamwambia, “Mwalimu, tunajua kwamba hujali maoni ya yeyote na huonyeshi upendeleo kati ya watu. Unafundisha njia ya Mungu katika ukweli. Je! Ni haki kulipa kodi kwa Kaisari au la? Je! Twaweza kulipa au la?
Lorsqu'ils furent arrivés, ils lui posèrent cette question: « Maître, nous savons que tu es honnête et que tu ne t'inclines devant personne; car tu n'as de parti pris pour personne, mais tu enseignes vraiment la voie de Dieu. Est-il licite de payer l'impôt à César, ou non?
15 Lakini Yesu alijua unafiki wao na kuwaambia, “Kwa nini mnanijaribu? Nipeni dinari niweze kuitazama.”
Doit-on donner, ou ne pas donner? » Mais lui, connaissant leur hypocrisie, leur dit: « Pourquoi m'éprouvez-vous? Apportez-moi un denier, que je le voie. »
16 Wakaleta moja kwa Yesu, Akawaambia, “Je! ni sura ya nani na maandishi yaliyopo hapa ni ya nani? Wakasema, “Ya Kaisari.”
Ils l'ont apporté. Il leur dit: « A qui appartient cette image et cette inscription? » Ils lui ont dit: « C'est à César. »
17 Yesu akawaambia, “Mpeni Kaisari vitu vya Kaisari na Mungu vitu vya Mungu.” Wakamstaajabia.
Jésus leur répondit: « Rendez à César ce qui est à César, et à Dieu ce qui est à Dieu. » Ils s'émerveillaient beaucoup devant lui.
18 Kisha Masadukayo, wasemao hakuna ufufuo, walimwendea. Wakamuwuliza, wakisema,
Des sadducéens, qui disent qu'il n'y a pas de résurrection, vinrent le trouver. Ils l'interrogèrent en disant:
19 “Mwalimu, Musa alituandikia kuwa, 'Ikiwa ndugu ya mtu akifa na kumwacha mke nyuma yake, lakini hakuacha mtoto, mtu atamchukua mke wa ndugu yake, na kujipatia watoto kwa ajili ya ndugu yake.'
« Maître, Moïse nous a écrit: 'Si le frère d'un homme meurt et laisse une femme derrière lui, sans laisser d'enfants, que son frère prenne sa femme et engendre une descendance pour son frère'.
20 Kulikuwa na ndugu saba, wa kwanza alitwaa mke na kisha akafa, hakuacha watoto.
Il y avait sept frères. Le premier prit une femme, et mourut sans laisser de descendance.
21 Kisha wa pili alimchukua naye akafa, hakuacha watoto. Na wa tatu hali kadhalika.
Le second la prit, et mourut, ne laissant aucun enfant derrière lui. Le troisième fit de même;
22 Na wa saba alikufa bila kuacha watoto. Mwishowe na mwanamke pia akafa.
et les sept autres la prirent et ne laissèrent pas d'enfants. La dernière de toutes les femmes mourut aussi.
23 Wakati wa ufufuo, watakapofufuka tena, Je! Atakuwa mke wa nani? Kwani wale ndugu wote saba walikuwa waume wake.”
A la résurrection, quand ils ressusciteront, de qui sera-t-elle la femme? Car les sept l'ont eue pour femme. »
24 Yesu aliwaambia, “Je! Hii si sababu kuwa mmepotoshwa, kwa sababu hamjui maandiko wala nguvu za Mungu?”
Jésus leur répondit: « N'est-ce pas parce que vous êtes dans l'erreur, ne connaissant ni les Écritures ni la puissance de Dieu?
25 Wakati wa kufufuka toka kwa wafu, hawataoa wala kuingia katika ndoa, bali watakuwa kama malaika wa mbinguni.
Car, lorsqu'ils ressusciteront d'entre les morts, ils ne se marieront pas et ne seront pas donnés en mariage, mais ils seront comme des anges dans le ciel.
26 Lakini, kuhusu wafu ambao wanafufuliwa, Je! Hamkusoma kutoka katika kitabu cha Musa, katika habari za kichaka, jinsi Mungu alivyosema na kumwambia, 'Mimi ni Mungu wa Abrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo?'
Mais pour ce qui est de la résurrection des morts, n'avez-vous pas lu dans le livre de Moïse, au sujet du buisson, comment Dieu lui a parlé en disant: « Je suis le Dieu d'Abraham, le Dieu d'Isaac et le Dieu de Jacob »?
27 Yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai. Ni dhahiri mmepotoka.”
Il n'est pas le Dieu des morts, mais des vivants. Vous vous trompez donc lourdement. »
28 Mmoja wa waandishi alikuja na kuyasikia mazungumzo yao; aliona kwamba Yesu aliwajibu vema. Alimwuliza, “Je! ni amri ipi iliyo ya muhimu zaidi katika zote?”
Un des scribes, qui les entendait discuter ensemble, sachant qu'il leur avait bien répondu, lui demanda: « Quel est le plus grand de tous les commandements? »
29 Yesu alimjibu, “Iliyo ya muhimu ni hii, “Sikia, Israeli, Bwana Mungu wetu, Bwana ni mmoja.
Jésus répondit: « La plus grande est: Écoute, Israël, le Seigneur notre Dieu, le Seigneur est unique.
30 Lazima umpende Bwana Mungu wako, kwa moyo wako yote, kwa roho yako yote, kwa akili yako yote, na kwa nguvu zako zote.'
Tu aimeras le Seigneur ton Dieu de tout ton cœur, de toute ton âme, de toute ta pensée et de toute ta force.' Tel est le premier commandement.
31 Amri ya pili ni hii, 'Lazima umpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.' Hakuna amri nyingine kuu zaidi ya hizi.”
Le second est ainsi conçu: « Tu aimeras ton prochain comme toi-même ». Il n'y a pas d'autre commandement plus grand que ceux-là. »
32 Mwandishi akasema, “Vema Mwalimu! Umesema kweli kwamba Mungu ni mmoja, na kwamba hakuna mwingine zaidi yake.
Le scribe lui dit: « En vérité, maître, tu as bien dit qu'il est unique et qu'il n'y en a pas d'autre que lui;
33 Kumpenda yeye kwa moyo wote, na kwa ufahamu wote na kwa nguvu zote, na kumpenda jirani kama mwenyewe, ni muhimu mno kuliko matoleo na dhabihu za kuteketeza.”
et l'aimer de tout son cœur, de toute son intelligence, de toute son âme et de toute sa force, et aimer son prochain comme soi-même, est plus important que tous les holocaustes et tous les sacrifices. »
34 Wakati Yesu alipoona ametoa jibu la busara, alimwambia, “Wewe hauko mbali na ufalme wa Mungu.” Baada ya hapo hakuna hata mmoja aliye thubutu kumwuliza Yesu maswali yoyote.
Voyant qu'il répondait avec sagesse, Jésus lui dit: « Tu n'es pas loin du Royaume de Dieu. » Après cela, personne n'osa plus lui poser de questions.
35 Na Yesu alijibu, wakati alipokuwa akifundisha katika hekalu, akasema, “Je! waandishi husemaje kuwa Kristo ni mwana wa Daudi?
Jésus répondit, comme il enseignait dans le temple: Comment se fait-il que les scribes disent que le Christ est le fils de David?
36 Daudi mwenyewe katika Roho Mtakatifu, alisema, 'Bwana alisema kwa Bwana wangu, keti katika mkono wangu wa kuume, mpaka niwafanye maadui wako kuwa chini ya miguu yako.'
Car David lui-même a dit dans l'Esprit Saint, Le Seigneur a dit à mon Seigneur, « Assieds-toi à ma droite, jusqu'à ce que je fasse de vos ennemis le marchepied de vos pieds. »
37 Daudi mwenyewe humwita Kristo, 'Bwana' Je! ni mwana wa Daudi kwa jinsi gani?” Na kusanyiko kuu lilimsikiliza kwa furaha.
C'est pourquoi David lui-même l'appelle Seigneur, comment pourrait-il être son fils? » Les gens du peuple l'écoutaient avec plaisir.
38 Katika mafundisho yake Yesu alisema, “Jihadharini na waandishi, wanaotamani kutembea na kanzu ndefu na kusalimiwa kwenye masoko
Dans son enseignement, il leur disait: « Méfiez-vous des scribes, qui aiment à se promener en longues robes, à se faire saluer sur les places publiques,
39 na kuketi kwenye viti vya wakuu katika masinagogi na katika sikukuu kwa maeneo ya wakuu.
à avoir les meilleurs sièges dans les synagogues et les meilleures places dans les fêtes,
40 Pia wanakula nyumba za wajane na wanaomba maombi marefu ili watu wawaone. Hawa watu watapokea hukumu iliyo kuu.”
ceux qui dévorent les maisons des veuves, et qui, pour faire semblant, font de longues prières. Ceux-là recevront une plus grande condamnation. »
41 Kisha Yesu aliketi chini karibu na sanduku la sadaka ndani ya eneo la hekalu; alikuwa akitazama watu waliokuwa wakitia pesa zao ndani ya sanduku. Watu wengi matajiri waliweka kiasi kikubwa cha pesa.
Jésus s'assit en face du trésor et vit comment la foule jetait de l'argent dans le trésor. Beaucoup de riches en jetaient beaucoup.
42 Kisha mwanamke mjane maskini alikuja na kutia vipande viwili, thamani ya senti.
Une pauvre veuve vint, et elle jeta deux petites pièces d'airain, qui équivalent à une pièce de quadrans.
43 Kisha akawaita wanafunzi wake na kuwaambia, “Amini nawaambia, mwanamke huyu mjane ametia kiasi kikubwa zaidi ya wote ambao wameshatoa katika sanduku la sadaka.
Il appela ses disciples et leur dit: « Je vous le dis en vérité, cette pauvre veuve a donné plus que tous ceux qui donnent au trésor,
44 Kwani wote wametoa kutokana na wingi wa mapato yao. Lakini mwanamke mjane huyu, kutoka katika umaskini wake, katia pesa yote ambayo alipaswa kuitumia kwa maisha yake.”
car tous ont donné de leur superflu, mais elle, de sa pauvreté, a donné tout ce qu'elle avait pour vivre. »

< Marko 12 >