< Luka 4 >

1 Kisha, Yesu akiwa amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Mto Jordani, na aliongozwa na Roho jangwani
Jésus, rempli de l'Esprit Saint, revint du Jourdain et fut conduit par l'Esprit dans le désert
2 kwa siku arobaini, na huko alijaribiwa na Ibilisi. Wakati huo hakula chochote, na mwisho wa wakati huo alihisi njaa.
pendant quarante jours, pour être tenté par le diable. Il ne mangea rien pendant ces jours-là. Ensuite, quand ils furent terminés, il eut faim.
3 Ibilisi akamwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, liamru jiwe hili kuwa mkate.”
Le diable lui dit: « Si tu es le Fils de Dieu, ordonne à cette pierre de devenir du pain. »
4 Yesu akamjibu, “Imeandikwa; 'mtu hataishi kwa mkate pekee.”
Jésus lui répondit: « Il est écrit: L'homme ne vivra pas de pain seulement, mais de toute parole de Dieu. »
5 Kisha Ibilisi alimwongoza juu kwenye kilele cha mlima, na akamwonyesha falme zote za dunia kwa muda mfupi.
Le diable, le conduisant sur une haute montagne, lui montra en un instant tous les royaumes du monde.
6 Ibilisi akamwambia, “Nitakupa mamlaka ya kutawala falme hizi zote pamoja na fahari zake. Naweza kufanya hivyo kwa sababu vyote vimekabidhiwa kwangu nivitawale, na ninaweza kumpa yeyote nitakaye kumpa.
Le diable lui dit: « Je te donnerai toute cette autorité et leur gloire, car elles m'ont été remises, et je les donne à qui je veux.
7 Kwahiyo, kama utaniinamia na kuniabudu, vitu hivi vyote vitakuwa vyako.”
Si donc tu te prosternes devant moi, tout cela sera à toi. »
8 Lakini Yesu alijibu na kumwambia, “Imeandikwa, “lazima umwabudu Bwana Mungu wako, na lazima umtumikie Yeye peke yake.”
Jésus lui répondit: « Va derrière moi, Satan! Car il est écrit: « Tu adoreras le Seigneur ton Dieu, et tu ne serviras que lui. »
9 Baadaye Ibilisi alimwongoza Yesu hadi Yerusalemu na kumweka sehemu ya juu kabisa ya jengo la hekalu na kumwambia, “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe chini kutoka hapa.
Il le conduisit à Jérusalem, le plaça sur le pinacle du temple et lui dit: « Si tu es le Fils de Dieu, jette-toi en bas d'ici,
10 Kwa sababu imeandikwa, “Atawaagiza malaika zake wakutunze na kukulinda,
car il est écrit, Il mettra ses anges à votre tête, pour vous protéger.
11 na watakuinua juu mikononi mwao ili kwamba usiumize miguu yako juu ya jiwe.”
et, C'est sur leurs mains qu'ils te porteront, de peur que tu ne heurtes ton pied contre une pierre. »
12 Yesu akijibu alimwambia, “Imenenwa, “usimjaribu Bwana Mungu wako.”
Jésus, prenant la parole, lui dit: « Il a été dit: Tu ne tenteras pas le Seigneur ton Dieu. »
13 Ibilisi alipomaliza kumjaribu Yesu, alienda zake na kumwacha hadi wakati mwingine.
Lorsque le diable eut achevé toutes les tentations, il s'éloigna de lui jusqu'à une autre époque.
14 Kisha Yesu alirudi Galilaya kwa nguvu za Roho, na habari kumhusu yeye zikaenea na kusambaa katika mikoa jirani yote.
Jésus revint en Galilée dans la puissance de l'Esprit, et la nouvelle de sa venue se répandit dans toute la région environnante.
15 Alifundisha katika masinagogi yao, na kila mmoja alimsifu.
Il enseignait dans leurs synagogues, et était glorifié par tous.
16 Siku moja alikwenda Nazareti, mji ambao alilelewa na kukulia. Kama ilivyokuwa desturi yake aliingia kwenye sinagogi siku ya sabato, na alisimama kusoma maandiko.
Il se rendit à Nazareth, où il avait été élevé. Il entra, selon sa coutume, dans la synagogue, le jour du sabbat, et se leva pour lire.
17 Alikabidhiwa gombo la nabii Isaya, hivyo, alilifungua gombo na akatafuta sehemu iliyoandikwa,
On lui remit le livre du prophète Ésaïe. Il ouvrit le livre, et trouva l'endroit où il était écrit,
18 “Roho wa Bwana yuu juu yangu, kwa sababu alinitia mafuta kuhubiri habari njema kwa maskini. Amenituma kutangaza uhuru kwa wafungwa, na kuwafanya wasioona waweze kuona tena. Kuwaweka huru wale wanaogandamizwa,
« L'Esprit du Seigneur est sur moi, car il m'a oint pour annoncer la bonne nouvelle aux pauvres. Il m'a envoyé pour guérir les cœurs brisés, pour proclamer la libération des captifs, le recouvrement de la vue pour les aveugles, pour délivrer ceux qui sont écrasés,
19 kuutangaza mwaka ambao Bwana ataonesha wema wake.”
et de proclamer l'année de grâce du Seigneur. »
20 Kisha akalifunga gombo, akamrudishia kiongozi wa sinagogi, na akaketi chini. Macho ya watu wote waliokuwa katika sinagogi yalimwangalia yeye.
Il ferma le livre, le rendit au gardien et s'assit. Les yeux de tous ceux qui étaient dans la synagogue étaient fixés sur lui.
21 Alianza kuzungumza nao akisema, “Leo andiko hili limetimizwa masikioni mwenu.”
Il se mit à leur dire: « Aujourd'hui, cette Écriture s'est accomplie pour vous. »
22 Kila mmoja pale alishuhudia kile alichokisema Yesu, na wengi miongoni mwao walishangazwa na maneno ya hekima yaliyokuwa yakitoka katika kinywa chake. Walikuwa wakisema, “huyu ni kijana tu wa Yusufu, siyo hivyo?”
Tous témoignaient de lui et s'étonnaient des paroles gracieuses qui sortaient de sa bouche; et ils disaient: « N'est-ce pas le fils de Joseph? »
23 Yesu akawaambia, “hakika mtasema methali hii kwangu, “Tabibu, jiponye mwenyewe. Chochote tulichosikia ukifanya Kapernaumu, kifanye hapa pia kijijini kwako.”
Il leur dit: « Vous me direz sans doute ce proverbe: « Médecin, guéris-toi toi-même! Tout ce que nous avons entendu faire à Capharnaüm, fais-le aussi ici, dans ta ville natale. »
24 Pia alisema, “hakika nawaambia ninyi, hakuna nabii anayekubalika katika nchi yake.”
Il répondit: « En vérité, je vous le dis, aucun prophète n'est accepté dans sa ville natale.
25 Lakini nawaambia ninyi kweli kwamba kulikuwa na wajane wengi Israel katika kipindi cha Eliya, wakati mbingu ilipofungwa kusiwe na nvua kwa miaka mitatu na nusu, wakati kulipokuwa na njaa kubwa katika nchi yote.
Mais en vérité, je vous le dis, il y avait beaucoup de veuves en Israël au temps d'Elie, lorsque le ciel fut fermé pendant trois ans et six mois et qu'une grande famine s'abattit sur tout le pays.
26 Lakini Eliya hakutumwa kwa yeyote mmoja wao, lakini kwa mjane mmoja tu aliyeishi Sarepta karibu na mji wa Sidoni.
Élie ne fut envoyé vers aucune d'elles, si ce n'est à Sarepta, dans le pays de Sidon, vers une femme qui était veuve.
27 Pia, kulikuwa na wakoma wengi Israel katika kipindi cha Elisha nabii, lakini hakuna hatammoja wao aliyeponywa isipokuwa Naamani mtu wa Siria.
Il y avait beaucoup de lépreux en Israël au temps du prophète Élisée, et aucun d'eux ne fut purifié, si ce n'est Naaman, le Syrien. »
28 Watu wote ndani ya sinagogi walijawa na gadhabu walipoyasikia haya yote.
Ils furent tous remplis de fureur dans la synagogue en entendant ces choses.
29 Walisimama na kumsukumizia nje ya mji, na kumwongoza mpaka kwenye ukingo wa mlima wa mji ambapo mji wao ulijengwa juu yake, ili waweze kumtupa chini.
Ils se levèrent, le jetèrent hors de la ville, et le conduisirent au sommet de la colline sur laquelle leur ville était bâtie, afin de le précipiter du haut de la falaise.
30 Lakini alipita salama katikati yao na akaenda zake.
Mais lui, passant au milieu d'eux, s'en alla.
31 Kisha alitelemkia Kapernaumu, katika mji wa Galilaya. Sabato moja alikuwa akifundisha watu ndani ya sinagogi.
Il descendit à Capernaüm, ville de Galilée. Il les enseignait le jour du sabbat,
32 Walishangazwa na mafundisho yake, kwasababu alifundisha kwa mamlaka.
et ils étaient étonnés de son enseignement, car sa parole avait de l'autorité.
33 Sasa siku hiyo ndani ya sinagogi, kulikuwa na mtu aliyekuwa na roho ya pepo mchafu, na alilia kwa sauti ya juu,
Il y avait dans la synagogue un homme possédé d'un esprit de démon impur. Il poussa un grand cri,
34 “Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Umekuja kutuangamiza? Ninajua wewe ni nani! Wewe ni mtakatifu wa Mungu!”
disant: « Ah! qu'avons-nous à faire avec toi, Jésus de Nazareth? Es-tu venu pour nous détruire? Je sais qui tu es: le Saint de Dieu! »
35 Yesu alimkemea pepo akisema, “Nyamaza kimya, na umtoke mtu huyu!” Pepo yule alipomtupa mtu yule chini katikati yao, alimtoka yule mtu bila ya kumsababishia maumivu yoyote.
Jésus le réprimanda en disant: « Tais-toi et sors de lui! » Quand le démon l'eut jeté au milieu d'eux, il sortit de lui, sans lui avoir fait aucun mal.
36 Watu wote walishangaa, na waliendelea kuzungumzia jambo hilo kila mmoja na mwenzake. Wakasema, “Ni maneno ya aina gani haya?” Anawaamuru roho wachafu kwa mamlaka na nguvu na watondoka.”
La stupeur s'empara de tous, et ils parlaient ensemble, les uns avec les autres, en disant: « Quelle est cette parole? Car c'est avec autorité et puissance qu'il commande aux esprits impurs, et ils sortent! »
37 Hivyo, habari juu ya Yesu zilienea kila sehemu katika maeneo yanayozunguka mkoa huo.
La nouvelle de sa venue se répandit dans tous les lieux de la région environnante.
38 Kisha Yesu aliondoka katika mji huo na akaingia katika nyumba ya Simoni. Sasa, mama mkwe wake na Simoni alikuwa anaumwa homa kali, na wakamsihi kwa niaba yake.
Il se leva de la synagogue et entra dans la maison de Simon. La belle-mère de Simon était atteinte d'une forte fièvre, et ils le supplièrent de la secourir.
39 Hivyo, Yesu alimsogelea, akaikemea ile homa na ikamwachia. Ghafla alisimama na akaanza kuwatumikia.
Il se tint au-dessus d'elle et menaça la fièvre, qui la quitta. Aussitôt, elle se leva et les servit.
40 Jua lilipokuwa likizama, watu walimletea Yesu kila mmoja aliyekuwa mgonjwa wa maradhi ya aina mbalimbali. Aliweka mikono yake juu ya kila mgonjwa na akawaponya wote.
Au coucher du soleil, tous ceux qui avaient des malades atteints de diverses maladies les lui amenèrent; il imposa les mains à chacun d'eux et les guérit.
41 Mapepo pia yaliwatoka wengi wao yakilia kwa sauti na kusema, “Wewe ni mwana wa Mungu!” Yesu aliwakemea mapepo na hakuwaruhusu waongee, kwa sababu walijua kwamba yeye alikuwa ni Kristo.
Des démons sortaient aussi de plusieurs, criant et disant: « Tu es le Christ, le Fils de Dieu! » Les réprimandant, il ne leur permettait pas de parler, car ils savaient qu'il était le Christ.
42 Wakati kulipopambazuka, alienda eneo lisilokuwa na watu. Makutano ya watu walikuwa wakimtafuta na wakaja katika eneo alilokuwapo. Walijaribu kumzuia asiende mbali na wao.
Le jour venu, il partit et s'en alla dans un lieu inhabité. La foule le cherchait, s'approchait de lui et le retenait, afin qu'il ne s'éloigne pas d'elle.
43 Lakini akawaambia, “Lazima pia nihubiri habari njema za ufalme wa Mungu katika miji mingine mingi, kwa kuwa hii ndiyo sababu nilitumwa hapa.”
Mais il leur dit: « Il faut que j'annonce aussi la bonne nouvelle du Royaume de Dieu dans les autres villes. C'est pour cela que j'ai été envoyé. »
44 Kisha aliendelea kuhubiri ndani ya masinagogi katika uyahudi wote.
Il prêchait dans les synagogues de Galilée.

< Luka 4 >