< Luka 21 >

1 Yesu alitazama akawaona wanaume matajiri waliokuwa wanaweka zawadi zao kwenye hazina.
Il leva les yeux et vit les riches qui mettaient leurs dons dans le trésor.
2 Akamuona mjane mmoja masikini akiweka senti zake mbili.
Il vit une pauvre veuve qui jetait deux petites pièces d'airain.
3 Hivyo akasema, “Kweli nawaambieni, huyu Mjane maskini ameweka nyingi kuliko wengine wote.
Il dit: « Je vous le dis en vérité, cette pauvre veuve a mis plus qu'eux tous,
4 Hawa wote wametoa hizi zawadi kutoka katika vingi walivyonavyo. Lakini huyu mjane, katika umaskini wake, ametoa fedha zote alizokuwa nazo kwa ajili ya kuishi kwake.”
car tous ceux-là ont fait des dons à Dieu de leur superflu, mais elle, de sa pauvreté, a mis tout ce qu'elle avait pour vivre. »
5 Wakati wengine walipokuwa wakisema juu ya hekalu, namna lilivyokuwa limepambwa na mawe mazuri na matoleo, alisema,
Comme certains parlaient du temple et de la façon dont il était décoré de belles pierres et de cadeaux, il dit:
6 “Kwa habari ya mambo haya mnayoyaona, siku zitakuja ambazo hakuna jiwe moja ambalo litaachwa juu ya jiwe jingine ambalo halitabomolewa.”
« Quant à ces choses que vous voyez, les jours viendront où il ne restera pas ici une pierre sur une autre qui ne soit pas renversée. »
7 Hivyo wakamuuliza, wakasema, “Mwalimu, mambo haya yatatokea lini? Na nini ni itakuwa ishara kwamba haya mambo yako karibu kutokea?”
Ils lui demandèrent: « Maître, quand donc ces choses arriveront-elles? Quel est le signe que ces choses vont arriver? »
8 Yesu akajibu, “Muwe waangalifu kwamba msidanganywe. Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, 'Mimi ndiye, 'na 'Muda umekaribia'. Msiwafuate.
Il dit: « Prenez garde de ne pas vous laisser égarer, car plusieurs viendront en mon nom, disant: « C'est moi", et « Le temps est proche ». Ne les suivez donc pas.
9 Mkisikia vita na vuruguvurugu msiogope, kwa sababu haya mambo lazima yatokee kwanza, lakini mwisho hautatokea upesi.”
Quand vous entendrez parler de guerres et de troubles, ne soyez pas terrifiés, car il faut que ces choses arrivent d'abord, mais la fin ne viendra pas immédiatement. »
10 Kisha akawaambia, “Taifa litainuka kupigana na taifa jingine, na ufalme juu ya ufalme mwingine.
Puis il leur dit: « Une nation s'élèvera contre une nation, et un royaume contre un royaume.
11 Kutakuwa na matetemeko makubwa, na njaa na tauni katika maeneo mbalimbali. Kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara za kutisha kutoka mbinguni.
Il y aura de grands tremblements de terre, des famines et des pestes en divers lieux. Il y aura des terreurs et de grands signes venant du ciel.
12 Lakini kabla ya mambo haya yote, wataweka mikono yao juu yenu na kuwatesa, kuwapeleka kwenye masinagogi na magereza, kuwaleta mbele za wafalme na wenye mamlaka kwa sababu ya jina langu.
Mais avant tout cela, on mettra la main sur vous, on vous persécutera, on vous livrera aux synagogues et aux prisons, on vous fera comparaître devant des rois et des gouverneurs, à cause de mon nom.
13 Hii itawafungulia fursa kwa ushuhuda wenu.
Il en résultera pour vous un témoignage.
14 Kwahiyo amueni mioyoni mwenu kutoandaa utetezi wenu mapema,
Mettez-vous donc dans la tête de ne pas réfléchir d'avance à la manière de répondre,
15 kwa sababu nitawapa maneno na hekima, ambayo adui zenu wote hawataweza kuipinga au kuikana.
car je vous donnerai une bouche et une sagesse auxquelles tous vos adversaires ne pourront résister ni contredire.
16 Lakini mtakataliwa pia na wazazi wenu, ndugu zenu, jamaa zenu na rafiki zenu, na watawaua baadhi yenu.
Vous serez livrés même par vos parents, vos frères, vos proches et vos amis. Ils feront mettre à mort certains d'entre vous.
17 Mtachukiwa na kila mmoja kwa sababu ya jina langu.
Vous serez haïs de tous les hommes à cause de mon nom.
18 Lakini hakuna hata unywele mmoja wa vichwa vyenu utakaopotea.
Et pas un cheveu de votre tête ne périra.
19 Katika kuvumilia mtaziponya nafsi zenu.
« C'est par votre endurance que vous gagnerez vos vies.
20 Mtakapoona Yerusalemu imezungukwa na majeshi, basi jueni kwamba uharibifu wake umekaribia.
« Mais quand vous verrez Jérusalem entourée d'armées, sachez que sa désolation est proche.
21 Hapo wale walioko Yudea wakimbilie milimani, na wale walioko katikati ya jiji waondoke, na msiwaache walioko vijijini kuingia.
Alors, que ceux qui sont en Judée fuient vers les montagnes. Que ceux qui sont au milieu d'elle s'en aillent. Que ceux qui sont dans la campagne n'y entrent pas.
22 Maana hizi ni siku za kisasi, ili kwamba mambo yote yaliyoandikwa yapate kutimilika.
Car ce sont des jours de vengeance, afin que s'accomplisse tout ce qui est écrit.
23 Ole ni kwa wale walio na mimba na kwa wale wanyonyeshao katika siku hizo! Kwa maana kutakuwa na adha kuu juu ya nchi, na ghadhabu kwa watu hawa.
Malheur aux femmes enceintes et à celles qui allaitent en ces jours-là! Car il y aura une grande détresse dans le pays et une grande colère pour ce peuple.
24 Na wataanguka kwa ncha ya upanga na watachukuliwa mateka kwa mataifa yote, na Yerusalem itakanyagwa na watu wa mataifa, mpaka wakati wa watu wa mataifa utakapotimilika.
Ils tomberont sous le tranchant de l'épée, et ils seront emmenés captifs dans toutes les nations. Jérusalem sera foulée aux pieds par les païens, jusqu'à ce que les temps des païens soient accomplis.
25 Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Na katika nchi kutakuwa na dhiki ya mataifa, katika kukata tamaa kutokana na mlio wa bahari na mawimbi.
Il y aura des signes dans le soleil, la lune et les étoiles; et sur la terre, l'angoisse des nations, dans la perplexité à cause du mugissement de la mer et des flots;
26 Kutakuwa na watu wakizimia kwa hofu na katika kutarajia mambo yatakoyo tokea juu ya dunia. Kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
les hommes seront saisis de crainte et d'attente des choses qui vont arriver au monde, car les puissances des cieux seront ébranlées.
27 Kisha watamwona Mwana wa Adamu akija mawinguni katika nguvu na utukufu mkuu.
Alors ils verront le Fils de l'homme venant sur une nuée avec puissance et grande gloire.
28 Lakini mambo haya yatakapoanza kutokea, simameni, inueni vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umesogea karibu.”
Mais quand ces choses commenceront à arriver, regardez en haut et levez vos têtes, car votre rédemption est proche. »
29 Yesu akawaambia kwa mfano, “Uangalieni mtini, na miti yote.
Il leur raconta une parabole. « Regardez le figuier et tous les arbres.
30 Inapotoa machipukizi, mnajionea wenyewe na kutambua kwamba kiangazi tayari kiko karibu.
Quand ils bourgeonnent déjà, vous le voyez et vous savez par vous-mêmes que l'été est déjà proche.
31 Vivyo hivyo, mnapoona mambo haya yanatokea, ninyi tambueni ya kwamba ufalme wa Mungu umekaribia.
De même, vous aussi, quand vous voyez ces choses arriver, vous savez que le Royaume de Dieu est proche.
32 Kweli, nawaambieni, kizazi hiki hakitapita, mpaka mambo haya yote yatakapotokea.
En vérité, je vous le dis, cette génération ne passera pas que tout ne soit accompli.
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
Le ciel et la terre passeront, mais mes paroles ne passeront pas.
34 Lakini jiangalieni wenyewe, ili kwamba mioyo yenu isije ikalemewa na ufisadi, ulevi, na mahangaiko ya maisha haya. Kwa sababu ile siku itawajia ghafla
« Prenez donc garde que vos cœurs ne s'appesantissent sous le poids des plaisirs de la fête, de l'ivresse et des soucis de la vie présente, et que ce jour ne vienne sur vous à l'improviste.
35 kama mtego. Kwasababu itakuwa juu ya kila mmoja aishiye katika uso wa dunia nzima.
Car il viendra comme un piège pour tous ceux qui habitent à la surface de toute la terre.
36 Lakini mwe tayari wakati wote, mwombe kwamba mtakuwa imara vya kutosha kuyaepuka haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.”
Veillez donc en permanence, en priant pour que vous soyez jugés dignes d'échapper à toutes ces choses qui arriveront, et de vous présenter devant le Fils de l'homme. »
37 Hivyo wakati wa mchana alikuwa akifundisha hekaluni na usiku alitoka nje, na kwenda kukesha katika mlima unaoitwa wa Mzeituni.
Chaque jour, Jésus enseignait dans le temple, et chaque soir, il sortait et passait la nuit sur la montagne qu'on appelle le mont Olivet.
38 Watu wote walimjia asubuhi na mapemaili kumsikiliza ndani ya hekalu.
Tout le peuple venait de bon matin le trouver dans le temple pour l'écouter.

< Luka 21 >