< Luka 20 >

1 Ikawa siku moja, Yesu alipokuwa akiwafundisha watu Hekaluni na kuhubiri injili, makuhani wakuu na walimu wa Sheria walimwendea pamoja na wazee.
On one of those days, as he was teaching the people in the temple and preaching the Good News, the priests and scribes came to him with the elders.
2 Walizungumza, wakimwambia, 'Tuambie ni kwa mamlaka gani unafanya mambo haya? Au ni nani huyo ambaye amekupa mamlaka haya? “
They asked him, “Tell us: by what authority do you do these things? Or who is giving you this authority?”
3 Naye akajibu, akawaambia, 'Nami pia nitawauliza swali. Niambieni
He answered them, “I also will ask you one question. Tell me:
4 ubatizo wa Yohana. Je, ulitoka mbinguni ama kwa watu? '
the baptism of John, was it from heaven, or from men?”
5 Lakini wakajadiliana wao kwa wao, wakisema, 'Tukisema, `litoka mbinguni, atatuuliza, ` Basi, mbona hamkumwamini?'
They reasoned with themselves, saying, “If we say, ‘From heaven,’ he will say, ‘Why didn’t you believe him?’
6 Na tukisema; ilitoka kwa wanadamu; watu wote hapa watatupiga mawe, maana wote wanaamini kwamba Yohana alikuwa nabii. '
But if we say, ‘From men,’ all the people will stone us, for they are persuaded that John was a prophet.”
7 Basi, wakamjibu ya kwamba hawakujua ilikotoka.
They answered that they didn’t know where it was from.
8 Yesu akawaambia, '“Wala mimi siwaambii ninyi ni kwa mamlaka gani ninafanya mambo haya.”
Jesus said to them, “Neither will I tell you by what authority I do these things.”
9 Aliwaambia watu mfano huu, “Mtu mmoja alipanda shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima wa mizabibu, na akaenda nchi nyingine kwa muda mrefu.
He began to tell the people this parable: “A man planted a vineyard and rented it out to some farmers, and went into another country for a long time.
10 Kwa muda uliopangwa, alimtuma mtumishi kwa wakulima mizabibu, kwamba wampe sehemu ya matunda ya shamba la mizabibu. Lakini wakulima wa mzabibu wakampiga, wakamrudisha mikono- mitupu.
At the proper season, he sent a servant to the farmers to collect his share of the fruit of the vineyard. But the farmers beat him and sent him away empty.
11 Kisha akamtuma tena mtumishi mwingine na nao wakampiga, kumtendea vibaya, na wakamrudisha mikono- mitupu.
He sent yet another servant, and they also beat him and treated him shamefully, and sent him away empty.
12 Alimtuma tena wa tatu na nao wakamjeruhi na kumtupa nje.
He sent yet a third, and they also wounded him and threw him out.
13 Hivyo bwana wa shamba akasema, 'Nitafanya nini? Nitamtuma mwanangu mpendwa. Labda watamheshimu. '
The lord of the vineyard said, ‘What shall I do? I will send my beloved son. It may be that seeing him, they will respect him.’
14 Lakini wakulima wa mzabibu walipomwona, walijadili wao kwa wao wakisema, `Huyu ndiye mrithi. Tumuue, ili urithi wake uwe wetu. '
“But when the farmers saw him, they reasoned amongst themselves, saying, ‘This is the heir. Come, let’s kill him, that the inheritance may be ours.’
15 Wakamtoa nje ya shamba la mizabibu na kumuua. Je bwana shamba atawafanya nini?
Then they threw him out of the vineyard and killed him. What therefore will the lord of the vineyard do to them?
16 Atakuja kuwaangamiza wakulima wa mzabibu, na atawapa shamba hilo wengine”. 'Nao waliposikia hayo, wakasema, 'Mungu amekataa'
He will come and destroy these farmers, and will give the vineyard to others.” When they heard that, they said, “May that never be!”
17 Lakini Yesu akawatazama, akasema, “Je andiko hili lina maana gani? 'Jiwe walilolikataa wajenzi, limekuwa jiwe la pembeni'?
But he looked at them and said, “Then what is this that is written, ‘The stone which the builders rejected was made the chief cornerstone’?
18 Kila mtu aangukaye juu ya jiwe hilo, atavunjika vipande vipande. Lakini yule ambaye litamwangukia, litamponda. '
Everyone who falls on that stone will be broken to pieces, but it will crush whomever it falls on to dust.”
19 Hivyo waandishi na wakuu wa makuhani walitafuta njia ya kumkamata wakati huohuo, walijua kwamba alikuwa amesema mfano huu dhidi yao. Lakini waliwaogopa watu.
The chief priests and the scribes sought to lay hands on him that very hour, but they feared the people—for they knew he had spoken this parable against them.
20 Walimuangalia kwa makini, wakatuma wapelelezi waliojifanya kuwa watu wa haki, ili wapate kupata kosa kwa hotuba yake, ili kumpelekakwa watawala na wenye mamlaka.
They watched him and sent out spies, who pretended to be righteous, that they might trap him in something he said, so as to deliver him up to the power and authority of the governor.
21 Nao wakamwuliza, wakisema, “Mwalimu, tunajua kwamba unasema na kufundisha mambo ya kweli na si kushawishiwa na mtu yeyote, lakini wewe hufundisha ukweli kuhusu njia ya Mungu.
They asked him, “Teacher, we know that you say and teach what is right, and aren’t partial to anyone, but truly teach the way of God.
22 Je, ni halali kwetu kulipa kodi kwa Kaisari, au la?”
Is it lawful for us to pay taxes to Caesar, or not?”
23 Lakini Yesu alitambua mtego wao, akawaambia,
But he perceived their craftiness, and said to them, “Why do you test me?
24 “Nionyesheni dinari. Sura na chapa ya nani ipo juu yake?” Walisema, '“Ya Kaisari.”
Show me a denarius. Whose image and inscription are on it?” They answered, “Caesar’s.”
25 Naye akawaambia, 'Basi, mpeni Kaisari yaliyo yake Kaisari, na Mungu yaliyo yake Mungu.'
He said to them, “Then give to Caesar the things that are Caesar’s, and to God the things that are God’s.”
26 Waandishi na wakuu wa makuhani hawakuwa na uwezo wa kukosoa kile alichosema mbele ya watu. Wakastaajabia majibu yake na hawakusema chochote.
They weren’t able to trap him in his words before the people. They marvelled at his answer and were silent.
27 Baadhi ya Masadukayo wakamwendea, wale ambao wanasema kwamba hakuna ufufuo,
Some of the Sadducees came to him, those who deny that there is a resurrection.
28 wakamwuliza, wakisema, “Mwalimu, Musa alituandikia kwamba kama mtu akifiwa na ndugu mwenye mke ambaye hana mtoto basi anapaswa kumchukuna mke wa ndugu yake na kuzaa nae kwa ajili ya kaka yake.
They asked him, “Teacher, Moses wrote to us that if a man’s brother dies having a wife, and he is childless, his brother should take the wife and raise up children for his brother.
29 Kulikuwa na ndugu saba Wa kwanza alioa, akafa bila kuacha mtoto,
There were therefore seven brothers. The first took a wife, and died childless.
30 na wa pili pia.
The second took her as wife, and he died childless.
31 Wa tatu akamchukua vilevile, vivyo hivyo wa saba hakuacha watoto na akafa.
The third took her, and likewise the seven all left no children, and died.
32 Baadaye yule mwanamke pia akafa.
Afterward the woman also died.
33 Katika ufufuo atakuwa mke wa nani? Maana wote saba walikuwa wamemwoa. '
Therefore in the resurrection whose wife of them will she be? For the seven had her as a wife.”
34 Yesu akawaambia, “Wana wa ulimwengu huu huoa na kuolewa. (aiōn g165)
Jesus said to them, “The children of this age marry and are given in marriage. (aiōn g165)
35 Lakini wale wanastaohili kupokea ufufuo wa wafu na kuingia uzima wa milele hawaoi wala hawaolewi. (aiōn g165)
But those who are considered worthy to attain to that age and the resurrection from the dead neither marry nor are given in marriage. (aiōn g165)
36 Wala hawawezi kufa tena, kwa sababu huwa sawasawa na malaika na ni watoto wa Mungu, wana wa ufufuo.
For they can’t die any more, for they are like the angels and are children of God, being children of the resurrection.
37 Lakini hiyo wafu wanafufuliwa, hata Musa alionyesha mahali katika habari za kichaka, pale alimwita Bwana kama Mungu wa Ibrahimu na Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo.
But that the dead are raised, even Moses showed at the bush, when he called the Lord ‘The God of Abraham, the God of Isaac, and the God of Jacob.’
38 Sasa, yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai, kwa sababu wote huishi kwake. “
Now he is not the God of the dead, but of the living, for all are alive to him.”
39 Baadhi ya walimu wa Sheria wakamjibu, 'Mwalimu, umejibu vema. '
Some of the scribes answered, “Teacher, you speak well.”
40 Hawakuthubutu kumwuliza maswali mengine zaidi.
They didn’t dare to ask him any more questions.
41 Yesu akawaambia, “Ki vipi watu wanasema kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?
He said to them, “Why do they say that the Christ is David’s son?
42 Maana Daudi mwenyewe anasema katika Zaburi: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti mkono wa kulia,
David himself says in the book of Psalms, ‘The Lord said to my Lord, “Sit at my right hand,
43 mpaka niwaweke adui zako chini ya miguu yako. '
until I make your enemies the footstool of your feet.”’
44 Daudi anamwita Kristo 'Bwana', basi atakuwaje mwana wa Daudi?”
“David therefore calls him Lord, so how is he his son?”
45 Watu wote walipokuwa wakimsikiliza akawaambia wanafunzi wake,
In the hearing of all the people, he said to his disciples,
46 'Jihadharini na waandishi, wapendao kutembea wamevaa mavazi marefu, na wapenda salamu maalum sokoni na viti vya heshima katika masinagogi, na maeneo ya heshima karamuni.
“Beware of those scribes who like to walk in long robes, and love greetings in the marketplaces, the best seats in the synagogues, and the best places at feasts;
47 Wao pia hula nyumba za wajane, na wanajifanya wanasali sala ndefu. Hawa watapokea hukumu kubwa zaidi. '
who devour widows’ houses, and for a pretence make long prayers. These will receive greater condemnation.”

< Luka 20 >