< Luka 19 >

1 Yesu aliingia na kupita katikati ya Yeriko.
He entered and was passing through Jericho.
2 Na hapo palikuwa na mtu mmoja aitwaye Zakayo. Ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
There was a man named Zacchaeus. He was a chief tax collector, and he was rich.
3 Alikuwa anajaribu kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, lakini hakuweza kuona kwa sababu ya umati wa watu, kwa kuwa alikuwa mfupi wa kimo.
He was trying to see who Jesus was, and couldn’t because of the crowd, because he was short.
4 Hivyo, alitangulia mbio mbele za watu, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona, kwa sababu Yesu alikaribia kupita njia hiyo.
He ran on ahead and climbed up into a sycamore tree to see him, for he was going to pass that way.
5 Wakati Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, 'Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.'
When Jesus came to the place, he looked up and saw him, and said to him, “Zacchaeus, hurry and come down, for today I must stay at your house.”
6 Akafanya haraka, akashuka na kumkaribisha kwa furaha.
He hurried, came down, and received him joyfully.
7 Watu wote walipoona hayo, wakalalamika, wakisema, 'Amekwenda kumtembelea mtu mwenye dhambi.'
When they saw it, they all murmured, saying, “He has gone in to lodge with a man who is a sinner.”
8 Zakayo akasimama akamwambia Bwana, Tazama Bwana nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimemnyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne. '
Zacchaeus stood and said to the Lord, “Behold, Lord, half of my goods I give to the poor. If I have wrongfully exacted anything of anyone, I restore four times as much.”
9 Yesu akamwambia, 'Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa sababu yeye pia ni mwana wa Ibrahimu.
Jesus said to him, “Today, salvation has come to this house, because he also is a son of Abraham.
10 Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa watu waliopotea. '
For the Son of Man came to seek and to save that which was lost.”
11 Waliposikia hayo, aliendelea kuongea na alitoa mfano, kwa sababu alikuwa karibu na Yerusalemu, na wao walidhani ya kuwa ufalme wa Mungu ulikuwa karibu kuonekana mara moja.
As they heard these things, he went on and told a parable, because he was near Jerusalem, and they supposed that God’s Kingdom would be revealed immediately.
12 Hivyo akawaambia, 'Ofisa mmoja alikwenda nchi ya mbali ili apokee ufalme na kisha aurudi.
He said therefore, “A certain nobleman went into a far country to receive for himself a kingdom and to return.
13 Aliwaita watumishi wake kumi, akawapa mafungu kumi, akawaambia, 'fanyeni biashara mpaka nitakaporudi.'
He called ten servants of his and gave them ten mina coins, and told them, ‘Conduct business until I come.’
14 Lakini wananchi wake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende kumfuata na kusema, 'Hatutaki mtu huyu atutawale.'
But his citizens hated him, and sent an envoy after him, saying, ‘We don’t want this man to reign over us.’
15 Ikawa aliporudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, akaamuru wale watumishi aliokuwa amewaachia fedha waitwe kwake, apate kujua faida gani waliyoipata kwa kufanya biashara.
“When he had come back again, having received the kingdom, he commanded these servants, to whom he had given the money, to be called to him, that he might know what they had gained by conducting business.
16 Wa kwanza akaja, akasema, `Bwana, fungu lako limefanya mafungu kumi zaidi. '
The first came before him, saying, ‘Lord, your mina has made ten more minas.’
17 Huyo Ofisa akamwambia, Vema, mtumishi mwema. Kwa sababu ulikuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi. '
“He said to him, ‘Well done, you good servant! Because you were found faithful with very little, you shall have authority over ten cities.’
18 Wa pili akaja, akasema, 'Bwana, fungu lako limefanya mafungu matano.'
“The second came, saying, ‘Your mina, Lord, has made five minas.’
19 Huyo Afisa akamwambia, 'Chukua mamlaka juu ya miji mitano.'
“So he said to him, ‘And you are to be over five cities.’
20 Na mwingine akaja, akasema, `Bwana hii hapa fedha yako, ambayo niliihifadhi salama katika kitambaa,
Another came, saying, ‘Lord, behold, your mina, which I kept laid away in a handkerchief,
21 kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Unaondoa kile usichokiweka na kuvuna usichopanda. '
for I feared you, because you are an exacting man. You take up that which you didn’t lay down, and reap that which you didn’t sow.’
22 Huyo Ofisa akamwambia, 'Kwa maneno yako mwenyewe, nitakuhukumu, ewe mtumishi mbaya. Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, nachukua nisichokiweka na kuvuna ambacho sikupanda.
“He said to him, ‘Out of your own mouth I will judge you, you wicked servant! You knew that I am an exacting man, taking up that which I didn’t lay down and reaping that which I didn’t sow.
23 Basi, mbona hukuweka fedha yangu katika benki, ili nikirudi niichukue pamoja na faida?
Then why didn’t you deposit my money in the bank, and at my coming, I might have earned interest on it?’
24 Ofisa akawaambia watu waliokuwa wamesimama hapo, 'Mnyang'anyeni hilo fungu na kumpa yule mwenye mafungu kumi.'
He said to those who stood by, ‘Take the mina away from him and give it to him who has the ten minas.’
25 Wakamwambia, `Bwana, yeye ana mafungu kumi. '
“They said to him, ‘Lord, he has ten minas!’
26 'Nawaambia, kila mtu ambaye anacho atapewa zaidi, lakini ambaye hana, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
‘For I tell you that to everyone who has, will more be given; but from him who doesn’t have, even that which he has will be taken away from him.
27 Lakini hawa maadui zangu, ambao hawakutaka niwe Mfalme wao, waleteni hapa na kuwaua mbele yangu. ''
But bring those enemies of mine who didn’t want me to reign over them here, and kill them before me.’”
28 Baada ya kusema hayo, aliendelea mbele akipanda kwenda Yerusalemu.
Having said these things, he went on ahead, going up to Jerusalem.
29 Ikawa alipokaribia Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
When he came near to Bethsphage and Bethany, at the mountain that is called Olivet, he sent two of his disciples,
30 akisema: `Nendeni katika kijiji cha jirani. Mkiingia, mtakuta mwana-punda hajapandwa bado. Mfungueni, mkamlete kwangu.
saying, “Go your way into the village on the other side, in which, as you enter, you will find a colt tied, which no man has ever sat upon. Untie it and bring it.
31 Kama mtu akiwauliza, `Mbona mnamfungua? ' Semeni, “Bwana anamhitaji. ''
If anyone asks you, ‘Why are you untying it?’ say to him: ‘The Lord needs it.’”
32 Wale waliotumwa wakaenda wakamwona mwana-punda kama Yesu alivyokuwa amewaambia.
Those who were sent went away and found things just as he had told them.
33 Walipokuwa wanamfungua mwana punda wamiliki wakawaambia, 'Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?'
As they were untying the colt, its owners said to them, “Why are you untying the colt?”
34 Wakasema, `Bwana anamhitaji. '
They said, “The Lord needs it.”
35 Basi, wakampelekea Yesu, wakatandika nguo zao juu ya mwana punda na wakampandisha Yesu juu yake.
Then they brought it to Jesus. They threw their cloaks on the colt and sat Jesus on them.
36 Alipokuwa akienda watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
As he went, they spread their cloaks on the road.
37 Alipokuwa anateremka mlima wa Mizeituni, jumuiya yote ya wanafunzi wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona,
As he was now getting near, at the descent of the Mount of Olives, the whole multitude of the disciples began to rejoice and praise God with a loud voice for all the mighty works which they had seen,
38 wakisema, 'Ndiye mbarikiwa Mfalme ajaye kwa jina la Bwana! Amani mbinguni, na utukufu juu!'
saying, “Blessed is the King who comes in the name of the Lord! Peace in heaven, and glory in the highest!”
39 Baadhi ya Mafarisayo katika mkutano wakamwambia, Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako. '
Some of the Pharisees from the multitude said to him, “Teacher, rebuke your disciples!”
40 Yesu akajibu, akasema, `Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, mawe yatapaza sauti. '
He answered them, “I tell you that if these were silent, the stones would cry out.”
41 Yesu alipoukaribia mji aliulilia,
When he came near, he saw the city and wept over it,
42 akisema, laiti ungelijua hata wewe, katika siku hii mambo ambayo yanayokuletea amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
saying, “If you, even you, had known today the things which belong to your peace! But now, they are hidden from your eyes.
43 Kwa kuwa siku zinakuja ambapo adui zako watajenga boma karibu na wewe, na kukuzunguka na kukukandamiza kutoka kila upande.
For the days will come on you when your enemies will throw up a barricade against you, surround you, hem you in on every side,
44 Watakuangusha chini wewe na watoto wako. Hawatakuachia hata jiwe moja juu ya jingine, kwa sababu haukutambua wakati Mungu alipokuwa anajaribu kukuokoa'.
and will dash you and your children within you to the ground. They will not leave in you one stone on another, because you didn’t know the time of your visitation.”
45 Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza,
He entered into the temple and began to drive out those who bought and sold in it,
46 akiwaambia, “Imeandikwa, 'Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala,' lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi”.
saying to them, “It is written, ‘My house is a house of prayer,’ but you have made it a ‘den of robbers’!”
47 Kwa hiyo, Yesu alikuwa akifundisha kila siku hekaluni. Makuhani wakuu na walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumuua,
He was teaching daily in the temple, but the chief priests, the scribes, and the leading men amongst the people sought to destroy him.
48 lakini hawakuweza kupata njia ya kufanya hivyo, kwa sababu watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini.
They couldn’t find what they might do, for all the people hung on to every word that he said.

< Luka 19 >