< Waamuzi 19 >

1 Katika siku hizo, wakati hakuna mfalme katika Israeli, kulikuwa na mtu, Mlawi, aliyekuwa akiishi kwa muda kidogo katika eneo la mbali zaidi ya nchi ya Efraimu. Alijichukulia mwanamke, masuria kutoka Bethlehemu huko Yuda.
It happened in those days, when there was no king in Israel, that there was a certain Levite sojourning on the farther side of the hill country of Ephraim, who took for himself a secondary wife from Bethlehem Judah.
2 Lakini mkewe hakuwa mwaminifu kwake; akaondoka na kurudi nyumbani kwa baba yake huko Bethlehemu ya Yuda. Alikaa huko kwa muda wa miezi minne.
His secondary wife was angry with him and went away from him to her father's house in Bethlehem of Judah, and was there about four months.
3 Kisha mumewe akaondoka na kumfuata ili kumshawishi arudi. Mtumishi wake alikuwa pamoja naye, na punda wawili. Akamleta nyumbani kwa baba yake. Baba wa msichana alipomwona, alifurahi.
Her husband arose, and went after her, to speak kindly to her, to bring her again, having his servant with him, and a couple of donkeys. And she brought him into her father's house; and when the father of the young woman saw him, he rejoiced to meet him.
4 Baba mkwe wake, baba wa msichana, alimshawishi kukaa siku tatu. Walikula na kunywa, na walikaa usiku huko.
His father-in-law, the young woman's father, welcomed him; and he stayed with him three days. So they ate and drank and stayed there.
5 Siku ya nne waliamka mapema na alijiandaa kuondoka, lakini baba wa msichana akamwambia mkwewe, “Jipe nguvu na mkate kidogo, kisha unaweza kwenda.”
It happened on the fourth day, that they arose early in the morning, and he rose up to depart: and the young woman's father said to his son-in-law, "Refresh yourself with a piece of bread, and after that you may go."
6 Basi hao wawili wakaketi kula na kunywa pamoja. Kisha baba ya msichana akasema, “Tafadhali uwe tayari kukaa usiku huu na kuwa na wakati mzuri.'
So they sat down, ate, and drank, both of them together. Then the young woman's father said to the man, "Please agree to stay the night, and enjoy yourself."
7 Mlawi alipoinuka ili aondoke, baba wa mwanamke huyo alimwomba akae, hivyo alibadili mpango wake na akalala usiku tena.
The man rose up to depart; but his father-in-law urged him, and he stayed there again.
8 Siku ya tano aliamka mapema kuondoka, lakini baba wa msichana akasema, 'Jitie nguvu mwenyewe, na kusubiri mpaka alasiri.' Kwa hiyo hao wawili wakala chakula.
He arose early in the morning on the fifth day to depart; and the young woman's father said, "Please refresh yourself and stay until the day declines." And the two of them ate and drank.
9 Mlawi na suria wake na mtumishi wake wakainuka ili kuondoka, baba mkwe wake, baba wa msichana akamwambia, “Angalia, sasa mchana unaelekea jioni. Tafadhali kaa usiku mwingine, na uwe na wakati mzuri. Unaweza kuamka kesho mapema na kurudi nyumbani.”
When the man rose up with his secondary wife and his servant to leave, his father-in-law, the young woman's father, said to him, "Look, now the day draws toward evening, please stay the night. Look, the day grows to an end, stay here, and enjoy yourself; and tomorrow you can get up early for your journey so that you may go home."
10 Lakini Mlawi hakuwa tayari kukaa usiku. Aliamka na kuondoka. Akaenda kuelekea Yebusi (hiyo ni Yerusalemu). Alikuwa na pande mbili za punda-na masuria wake alikuwa pamoja naye.
But the man wouldn't stay that night, but he rose up and departed, and went toward Jebus (that is, Jerusalem). And there were with him a couple of saddled donkeys, and his secondary wife and his servant were with him.
11 Walipokuwa karibu na Yebusi, siku hiyo ilikuwa imeenda mno, na mtumishi akamwambia bwana wake, Haya, tupate kwenda kwa mji wa Wayebusi, tukakae ndani yake usiku huu.
When they were by Jebus, the day was almost gone, and the servant said to his master, "Please come and let us stop at this city of the Jebusites, and spend the night in it."
12 Bwana wake akamwambia, “Hatuwezi kwenda katika mji wa wageni ambao si wa wana wa Israeli.” Tutakwenda Gibea.
His master said to him, "We won't go into the city of a foreigner that is not of the children of Israel, but we will pass over to Gibeah."
13 Mlawi akamwambia yule kijana, “Njoo, twende sehemu moja wapo, na tukae usiku huko Gibea au Rama.”
He said to his servant, "Come and let us try to reach one of those places and we will spend the night in Gibeah or Ramah."
14 Basi, wakaenda, na jua likachwea wakiwa karibu na Gibea, katika eneo la Benyamini.
So they passed on and went their way; and the sun set on them near Gibeah, which belongs to Benjamin.
15 Wakageuka huko ili wawezenkukaa usiku huko Gibea. Naye akaingia na kukaa katika njia kuu ya jiji, maana hakuna mtu aliyewaingiza nyumbani kwake usiku.
They turned that way to go in to spend the night in Gibeah. And he went in and they sat down in the street of the city; for there was no one who would take them into their house to spend the night.
16 Lakini mtu mzee alikuwa akija kutoka kazini kwake katika shamba jioni hiyo. Alikuwa kutoka mlima wa Efraimu, naye alikuwa akikaa kwa muda huko Gibea. Lakini watu wanaoishi mahali hapo walikuwa Wabenyamini.
Look, there came an old man from his work out in the field at evening. Now the man was of the hill country of Ephraim, and he was residing in Gibeah; but the men of the place were Benjamites.
17 Aliinua macho na kumwona msafiri katika njia kuu ya jiji. Huyo mzee akasema, “Unakwenda wapi? Unatoka wapi?”
He lifted up his eyes, and saw the traveler in the street of the city. And the old man said, "Where are you going, and where did you come from?"
18 Mlawi akamwambia, “Tunaenda kutoka Betelehemu ya Yuda mpaka sehemu ya mbali zaidi ya nchi ya kilima ya Efraimu, ambako mimi hutoka. Nilikwenda Bethlehemu huko Yuda, nami nenda nyumbani mwa Bwana; lakini hakuna mtu atakayenichukua nyumbani kwake.
He said to him, "We are passing from Bethlehem in Judah to the farther side of the hill country of Ephraim. I am from there, and I went to Bethlehem in Judah. And I am going to my home, and there is no one who will take me into his home.
19 Tuna nyasi za kulisha punda zetu, na kuna mkate na divai kwa ajili yangu na mtumishi wako mwanamke hapa, na kwa kijana huyu pamoja na watumishi wako. Hatujapungukiwa chochote. '
Yet there is both straw and feed for our donkeys, and there is bread and wine also for me, and for your female servant, and for the young man who is with your servants. There is no lack of anything."
20 Huyo mzee akawasalimu, “Amani iwe na wewe! Nitakupatia mahitaji yako yote. Usikae usiku tu katika njia kuu.”
And the old man said, "Peace be to you. I will take care of all your needs; however, do not spend the night in the square."
21 Basi huyo mtu akamleta Mlawi nyumbani kwake, akawalisha punda. Wakaosha miguu yao na kula na kunywa.
So he brought him into his house, and fed the donkeys. And they washed their feet, and ate and drank.
22 Walipokuwa wakifurahisha mioyo yao, watu wengine wa jiji, watu wasiokuwa na maana, walizunguka nyumba, wakipiga mlango. Wakamwambia yule mzee, mwenye nyumba, wakisema, “Mtoe mtu aliyeingia nyumbani kwako, ili tuweze kufanya mapenzi naye.”
As they were enjoying themselves, look, the men of the city, some wicked men of the city surrounded the house, beating at the door. And they spoke to the master of the house, the old man, saying, "Bring out the man who came into your house, that we may have sex with him."
23 Yule mtu, mwenye nyumba, akawajia, akawaambia, “Hapana, ndugu zangu, tafadhali msifanye jambo baya! Kwa kuwa mtu huyu ni mgeni nyumbani kwangu, musifanye jambo hili baya!”
The man, the master of the house, went out to them, and said to them, "No, my brothers, please do not act so wickedly; since this man has come into my house. Do not do this disgraceful thing.
24 Angalia, binti yangu bikira na masuria wake hawa hapa. Ngoja niwalete sasa. Wapuuze na kufanya nao chochote mnachopenda. Lakini msifanyie jambo hili mbaya kwa mtu huyu!”
Look, here is my virgin daughter and his secondary wife. I will bring them out now. Ravish them and do with them what seems good to you; but do not do any such a disgraceful thing to this man."
25 Lakini watu hawakumsikiliza, kwa hiyo huyo mwanamume akamshika yule mwanamke, akamleta nje. Walimkamata, wakambaka, na kumtendea uovu usiku mzima, na asubuhi wakamruhusu aende.
But the men wouldn't listen to him: so the man laid hold of his secondary wife, and brought her out to them. And they raped her and abused her all night until the morning, and when the day began to dawn they let her go.
26 Asubuhi mwanamke alikuja akaanguka chini ya mlango wa nyumba ya mtu ambapo bwana wake alikuwa, na yeye akalala pale mpaka kulipokucha.
Then at daybreak the woman arrived and fell down at the door of the man's house where her lord was, until daylight.
27 Bwana wake akaondoka asubuhi na kufungua milango ya nyumba, akatoka kwenda njiani. Aliweza kumwona mwanamke wake amelala pale mlangoni, mikono yake ikiwa juu ya kizingiti.
Her lord rose up in the morning, and opened the doors of the house, and went out to go his way; and look, the woman his secondary wife was fallen down at the door of the house, with her hands on the threshold.
28 Mlawi akamwambia, “Simama twende.” Lakini hakujibiwa. Alimuweka juu ya punda, na huyo mtu akaondoka nyumbani.
And he said to her, "Get up, and let us go." But there was no answer, for she was dead. So he placed her on the donkey, and the man rose up and went to his home.
29 Mlawi alipofika nyumbani kwake, akachukua kisu, naye akamshika suria wake, akamkataa, mguu kwa mguu, akafanya vipande kumi na viwili, akapeleka vipande kila mahali katika Israeli.
When he had come into his house, he took a knife, and took hold of his secondary wife and divided her, limb by limb, into twelve pieces, and sent her throughout all the territory of Israel.
30 Wote waliona hili wakasema, “Kitu hicho hakijawahi kufanyika au kuonekana tangu siku ambayo watu wa Israeli walikuja kutoka nchi ya Misri mpaka leo. Fikiria juu ya hili! Tupe ushauri! Tuambie nini cha kufanya!”
And it was so, that all who saw it said, "Nothing like this has been done or seen since the day that the children of Israel came up out of the land of Egypt until this day." And he commanded the men whom he sent, saying, "This is what you will say to all the men of Israel, 'Has anything like this happened since the day that the children of Israel came up out of the land of Egypt until this day? Consider it, take counsel, and speak.'"

< Waamuzi 19 >