< Yoshua 1 >

1 Sasa ilitokea baada ya kufa kwa Musa, mtumishi wa Yahweh, Yahweh alimwambia Yoshua, mwana wa Nuni, msaidizi mkuu wa Musa, kusema,
Now it happened after the death of Moses the servant of Jehovah, that Jehovah spoke to Joshua the son of Nun, Moses' servant, saying,
2 “Musa, mtumishi wangu amekufa. Sasa basi inuka, vuka mto huu wa Yordani, wewe na watu hawa wote, kuingia katika nchi ambayo ninawapa - watu waisraeli.
Moses my servant is dead; now therefore arise, go over this Jordan, you, and all this people, to the land which I give to them, even to the children of Israel.
3 Nimewapa ninyi kila sehemu ambapo nyayo za miguu yenu itakanyaga. Nimewapa ninyi, kama nilivyomwahidi Musa.
I have given you every place that the sole of your foot will tread on, as I told Moses.
4 kuanzia jangwani na Lebanoni, hadi mto mkubwa wa Frati, nchi yote ya Wahiti, na hata Bahari kuu, ambako jua huzama, itakuwa nchi yenu.
From the wilderness, and this Lebanon, even to the great river, the river Perath, all the land of the Hittites, and to the Great Sea toward the going down of the sun, shall be your border.
5 Hakuna mtu awaye yote atakayeweza kusimama kinyume chako siku zote za maisha yako. Nitakuwa pamoja nawe kama nilivyokuwa na Musa. Sitakupungukia wala kukuacha.
No man will be able to stand before you all the days of your life. As I was with Moses, so I will be with you. I will not fail you nor forsake you.
6 Uwe hodari na jasiri. Wewe utawafanya watu hawa wairithi nchi ambayo niliwaahidi baba zao kuwa ningewapa.
Be strong and of good courage; for you shall cause this people to inherit the land which I swore to their fathers to give them.
7 Uwe hodari na jasiri sana. uwe makini kutii sheria zote ambazo Musa mtumishi wangu alikuagiza. Usikengeuke upande wa kulia au wa kushoto, ili uweze kufanikiwa kila mahali utakapoenda.
Only be strong and very courageous, to observe to do according to all the law, which Moses my servant commanded you. Do not turn from it to the right hand or to the left, that you may have good success wherever you go.
8 Siku zote uuongee juu ya kitabu hiki cha sheria. Utakitafakari mchana na usiku ili kwamba uweze kutii yote yaliyoandikwa humo. Kisha utastawi na kufanikiwa.
This book of the law shall not depart out of your mouth, but you shall meditate on it day and night, that you may observe to do according to all that is written in it: for then you shall make your way prosperous, and then you shall have good success.
9 Je si mimi niliyekuagiza? Uwe hadori na jasiri! Usiogope. Usivunjike moyo. Yahweh Mungu wako yuko pamoja nawe kila uendeko.
Haven't I commanded you? Be strong and of good courage. Do not be afraid, neither be dismayed: for Jehovah your God is with you wherever you go.
10 Kisha Yoshua akawaagiza viongozi wa watu,
Then Joshua commanded the officers of the people, saying,
11 “Nendeni katika kambi na waagizeni watu, 'andaeni chakula kwa ajili yenu. Baada ya siku tatu mtavuka mto huu wa Yordani na kuingia ndani na kuimiliki nchi ambayo Yahweh Mungu wenu awapeni ninyi ili kuimiliki.””
"Pass through the midst of the camp, and command the people, saying, 'Prepare food; for within three days you are to pass over this Jordan, to go in to possess the land, which Jehovah your God gives you to possess it.'"
12 Yoshua akawaambia Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase,
Joshua spoke to the Reubenites, and to the Gadites, and to the half-tribe of Manasseh, saying,
13 “Kumbukeni maneno ambayo Musa, mtumishi wa Yahweh, aliwaaagiza aliposema, 'Yahweh Mungu wenu awapeni ninyi pumziko, naye awapeni ninyi nchi hii.'
"Remember the word which Moses the servant of Jehovah commanded you, saying, 'Jehovah your God gives you rest, and will give you this land.
14 Wake zenu, na watoto wenu na mifugo yenu itakaa katika nchi ambayo Musa aliwapa ninyi ng'ambo ya Yordani. Lakini watu wenu wa vita wataenda pamoja na ndugu zao na kuwasaidia.
Your wives, your little ones, and your livestock, shall live in the land which Moses gave you beyond the Jordan; but you shall pass over before your brothers armed, all the mighty men of valor, and shall help them
15 Mpaka hapo Yahweh atakapowapa ndugu zenu pumziko kama alivyowapa ninyi. Na wao pia watamiliki nchi ambayo Yahweh Mungu wenu awapeni ninyi. Kisha mtarudi katika nchi yenu na kuimiliki, nchi ambayo Musa mtumishi wa Yahweh aliwapa ninyi ng'ambo ya Yordani, mahali pa mapambazuko ya jua.”
until Jehovah has given your brothers rest, as he has given you, and they have also possessed the land which Jehovah your God gives them. Then you shall return to the land of your possession, and possess it, which Moses the servant of Jehovah gave you beyond the Jordan toward the sunrise.'"
16 Nao wakamjibu Yoshua, na kusema, “Mambo yote uliyotuagiza tutayafanya, na kila mahali utakapotutuma tutaenda.
They answered Joshua, saying, "All that you have commanded us we will do, and wherever you send us we will go.
17 Tutakutii kama tulivyomtii Musa. Yahweh Mungu wako na awe pamoja nawe tu kama aliyokuwa pamoja na Musa.
Just as we listened to Moses in all things, so will we listen to you. Only may Jehovah your God be with you, as he was with Moses.
18 Yeyote anayeasi maagizo yako na kutotii maneno yako atauawa. Uwe hodari na jasiri tu.
Whoever rebels against your commandment, and doesn't listen to your words in all that you command him, he shall be put to death. Only be strong and of good courage."

< Yoshua 1 >