< Torati 33 >

1 Hii ni baraka ambayo Musa mtu wa Mungu aliwabariki watu wa Israeli kabla ya kifo chake.
This is the blessing, with which Moses the man of God blessed the children of Israel before his death.
2 Alisema: Yahwe alikuja kutoka Sinai na akainuka kutoka Seiri juu yao. Aling'ara kutoka mlima wa Paramu, na akaja na elfu kumi ya watakatifu. Katika mkono wake wa kuume radi zilimulika.
He said, "Jehovah came from Sinai, and dawned from Seir upon us. He shone forth from Mount Paran. He came from the ten thousands of holy ones. At his right hand was a fiery law for them.
3 Kweli, anawapenda watu; watakatifu wake wote wapo mikononi mwako, na walimsujudu mguuni mwake; walipokea maneno yako.
Yes, he loves the people. All his holy ones are in your hand. They sat down at your feet; each receives your words.
4 Musa alituamuru sheria, urithi kwa kusanyiko la Yakobo.
Moses commanded us a law, an inheritance for the assembly of Jacob.
5 Kisha pakawa na mfalme Yeshurumu, pale ambapo wakuu wa watu walipokusanyika, makabila yote ya Israeli pamoja.
He was king in Jeshurun, when the heads of the people were gathered, all the tribes of Israel together.
6 Acha Rubeni aishi na asife, lakini wanaume wake wawe wachache.
"Let Reuben live, and not die; Nor let his men be few."
7 Hii ni baraka ya Yuda. Musa akasema: Sikiliza sauti ya Yuda, Yahwe, na umlete kwa watu wake tena. Mpiganie; kuwa msaada dhidi ya maadui wake.
This is for Judah. He said, "Hear, Jehovah, the voice of Judah. Bring him in to his people. With his hands he contended for himself. You shall be a help against his adversaries."
8 Kuhusu Lawi, Musa akasema: Thumimu yako na Urimu yako ni ya mtakatifu wako, yule uliyemjaribu kule Masa, ambaye ulishindana naye katika maji ya Meriba.
Of Levi he said, "Give to Levi your Thummim and your Urim to your faithful one, whom you proved at Massah, with whom you strove at the waters of Meribah;
9 Mtu aliyesema juu ya baba na mama yake, “Sijawaona.” Wala hakuwatambua kaka zake, wala hakuzingatia juu ya watoto wake wenyewe. Kwa maana alilinda neno lako na kushika agano lako.
who said of his father, and of his mother, 'I have not seen him;' Neither did he acknowledge his brothers, Nor did he know his own children: For they have observed your word, and keep your covenant.
10 Anafundisha Yakobo maagizo yako na Israeli sheria yako. Ataweka ubani mbele yako na sadaka kamili ya kuteketezwa juu ya dhabahu lako.
They shall teach Jacob your ordinances, and Israel your law. They shall put incense before you, and whole burnt offering on your altar.
11 Bariki mali zake, Yahwe, na kubali kazi ya mikono yake. Vunja viuno vya wale wanaoinuka dhidi yake, na wale watu wanaomchukia, ili wasiinuke tena.
Jehovah, bless his substance. Accept the work of his hands. Strike the loins of those who rise against him, of those who hate him, that they not rise again."
12 Kuhusu Benyamini, Musa akasema: Yule anayependwa na Yahwe anaishi kwa usalama kando yake; Yahwe anamkinga siku nzima, naye huishi katikati ya mikono ya Yahwe.
Of Benjamin he said, "The beloved of Jehovah shall dwell in safety by him. He covers him all the day long. He dwells between his shoulders."
13 Kuhusu Yusufu, Musa akasema: Nchi yake na ibarikiwe na Yahwe na vitu vya thamani vya mbinguni, na umande, na kina kilalacho chini.
Of Joseph he said, "His land is blessed by Jehovah, for the precious things of the heavens, for the dew, for the deep that couches beneath,
14 Nchi yake na ibarikiwe na vitu vya thamani mavuno ya jua, na vitu vya thamani mazao ya miezi,
with the choices fruits of the sun, and the bounteous yield of the months,
15 kwa vitu vizuri vya milima ya zamani, na kwa vitu vya thamani vya milima ya milele.
with the finest produce of the ancient mountains, and the abundance of the everlasting hills,
16 Nchi yake ibarikiwe na vitu vya thamani vya ardhi na wingi wake, na kwa mapenzi mema ya yule aliyekuwa kichakani. Baraka na ifike juu ya kichwa cha Yusufu, na juu ya kichwa cha yule aliyekuwa mwana wa mfalme kwa kaka zake.
with the choice things of the earth and its fullness, the good will of him who lived in the bush. Let this come on the head of Joseph, on the crown of the head of him who was separate from his brothers.
17 Mzawa wa kwanza wa ng’ombe, katika utukufu wake, na pembe zake ni pembe za ng’ombe mwitu. Kwa hawa atawasukuma watu, wote, hadi mwisho wa ulimwengu. Hawa ni maelfu makumi ya Efraimu; hawa ni maelfu wa Manase.
A firstborn bull, majesty is his. His horns are the horns of the wild ox. With them he shall push all of the peoples, to the farthest parts of the earth. They are the ten thousands of Ephraim. They are the thousands of Manasseh."
18 Kuhusu Zabuloni, Musa alisema: Furahi, Zabuloni, katika kutoka kwako, na wewe, Isakari, katika mahema yako.
Of Zebulun he said, "Rejoice, Zebulun, in your going out; and Issachar, in your tents.
19 Watawaita watu hadi milimani. Huko watatoa sadaka za utakatifu. Maana watanyonya wingi wa bahari, na mchanga wa ufukweni.
They shall call the peoples to the mountain. There they will offer sacrifices of righteousness, for they shall draw out the abundance of the seas, the hidden treasures of the sand."
20 Kuhusu Gadi, Musa alisema: Abarikiwe yule amkuzaye Gadi. Ataishi pale kama simba jike, naye atanyakua mkono au kichwa.
Of Gad he said, "He who enlarges Gad is blessed. He dwells as a lioness, and tears the arm, yes, the crown of the head.
21 Alitoa sehemu nzuri kwake mwenyewe, maana kulikuwa na fungu la ardhi la kiongozi lililohifadhiwa. Alikuja na vichwa vya watu. Alitekeleza haki ya Yahwe na maagizo yake pamoja na Israeli.
He provided the first part for himself, for there was the lawgiver's portion reserved. He came with the heads of the people. He executed the righteousness of Jehovah, his ordinances with Israel."
22 Kuhusu Dani, Musa alisema: Dani ni mwana wa simba arukaye kutoka Bashani.
Of Dan he said, "Dan is a lion's cub that leaps out of Bashan."
23 Kuhusu Naftali, Musa alisema: Naftali, aliyeridhika na fadhila, na kujaa kwa baraka za Yahwe, miliki nchi iliyopo magharibi na kusini.
Of Naphtali he said, "Naphtali, satisfied with favor, full of the blessing of Jehovah, Possess the west and the south."
24 Kuhusu Asheri, Musa alisema: Abarakiwe Asheri Zaidi ya watoto wengine wa kiume; naye akubalike kwa kaka zake, na achovye mguu wake ndani ya mafuta ya zeituni.
Of Asher he said, "Asher is blessed with children. Let him be acceptable to his brothers. Let him dip his foot in oil.
25 Vyuma vya mji wako na viwe chuma na shaba; kama vile siku zako zitakavyokuwa, ndivyo usalama wako utakavyokuwa.
Your bars shall be iron and bronze. As your days, so your strength will be.
26 Hakuna aliye kama Mungu, Yeshurumu – aliyekamili, anayeendesha katika mbingu kukusaidia, na katika utukufu wake juu ya mawingu.
"There is none like God, Jeshurun, who rides on the heavens for your help, In his majesty through the skies.
27 Mungu wa milele ni kimbilio, na chini yake kuna mikono ya milele. Husukuma adui mbele yako, naye alisema, “Angamiza!”
The God of old is a dwelling place. Underneath are the everlasting arms. He thrust out the enemy from before you, and said, 'Destroy.'
28 Israeli waliishi katika usalama. Wana wa Yakobo walikuwa salama katika nchi ya nafaka na divai mpya; hakika, mbingu na idondoshe umande juu yake.
Israel dwells in safety; the fountain of Jacob alone, In a land of grain and new wine. Yes, his heavens drop down dew.
29 Baraka zako ni nyingi, Israeli! Nani kama wewe, watu waliokombolewa na Yahwe, ngao ya msaada wako, na upanga wa utukufu wako? Maadui zako watakuja kwako kwa kutetemeka; utakanyanga sehemu zao zilizoinuka.
You are happy, Israel. Who is like you, a people saved by Jehovah, the shield of your help, the sword of your excellency. Your enemies shall submit themselves to you. You shall tread on their high places."

< Torati 33 >