< Yoshua 23 >

1 Na baada ya siku nyingi, kipindi ambacho Yahweh alikuwa ameipa Israeli pumziko kutoka maadui zao waliowazunguka,
And it came to pass after many days, when the LORD had given rest unto Israel from all their enemies round about, and Joshua was old and well stricken in years;
2 Joshua alikuwa mzee sana. Yoshua aliwaita Waisraeli wote, na wazee wao, na viongozi, na waamuzi, na kwa maafisa, na kisha akawaambia, “Mimi nimezeeka sana.
that Joshua called for all Israel, for their elders and for their heads, and for their judges and for their officers, and said unto them: 'I am old and well stricken in years.
3 Mmeshaona kila kitu ambacho Yahweh Mungu wenu ameshafanya kwa mataifa haya yote kwa ajili yenu, kwa kuwa ni Yahweh Mungu wenu ambaye amewapigania ninyi.
And ye have seen all that the LORD your God hath done unto all these nations because of you; for the LORD your God, He it is that hath fought for you.
4 Tazama! Nimeshawakabidhi kwenu mataifa yaliyosalia ili kuyateka kwa ajili ya kupata urithi ya makabila yenu, sambasamba na mataifa yote ambayo tayari nimeshayaangamiza, tangu Yordani hadi Bahari kuu katika upande wa magharibi.
Behold, I have allotted unto you for an inheritance, according to your tribes, these nations that remain, from the Jordan, with all the nations that I have cut off, even unto the Great Sea toward the going down of the sun.
5 Yahweh Mungu wenu atayaondoa. Atayafukuzia mbali kutoka kwenu. Ataiteka nchi yao, nanyi mtaimiliki nchi yao, kama vile Yahweh Mungu wenu alivyowaahidi ninyi.
And the LORD your God, He shall thrust them out from before you, and drive them from out of your sight; and ye shall possess their land, as the LORD your God spoke unto you.
6 Hivyo, iweni jasiri, ili kwamba mtunze na kuyafanya yale yote yaliyoandikwa katika kitabu cha sheria ya Musa, msikengeuke upande wa kulia wala upande wa kushoto,
Therefore be ye very courageous to keep and to do all that is written in the book of the law of Moses, that ye turn not aside therefrom to the right hand or to the left;
7 basi msichanganyikane na mataifa haya ambayo yamesalia miongoni mwenu, wala msiyataje majina ya miungu yao, wala msiape kwayo, wala msiiabudu, wala msiipigie magoti.
that ye come not among these nations, these that remain among you; neither make mention of the name of their gods, nor cause to swear by them, neither serve them, nor worship them;
8 Badala yake, mnatakiwa kumshika sana Yahweh Mungu wenu kama vile mlivyofanya siku hii ya leo.
but cleave unto the LORD your God, as ye have done unto this day;
9 Kwa kuwa Yahweh ameyafukuzia mbali mbele yenu mataifa makubwa yenye nguvu. Hakuna hata mmoja aliyeweza kusimama mbele yenu hata siku hii ya leo.
wherefore the LORD hath driven out from before you great nations and mighty; but as for you, no man hath stood against you unto this day.
10 Mtu yeyote mmoja wa kwenu atawafanya watu elfu wakimbie mbali, kwa kuwa Yahweh Mungu wenu, ndiye anayepigania ninyi, kama vile alivyowaahidi.
One man of you hath chased a thousand; for the LORD your God, He it is that fought for you, as He spoke unto you.
11 Zingatieni kwa uangalifu ili mmpende Yahweh Mungu wenu.
Take good heed therefore unto yourselves, that ye love the LORD your God.
12 Lakini kama mkiegeuka na kushikamana na watu walioalia wa mataifa haya waliobaki miongoni mwenu, au kuoana nao, au kama mkishirikiana pamoja nao, na wao pamoja nanyi,
Else if ye do in any wise go back, and cleave unto the remnant of these nations, even these that remain among you, and make marriages with them, and go in unto them, and they to you;
13 jueni kwa hakika kwamba Yahweh Mungu wenu hatayafukuzia mbali mataifa haya yatoke kati yenu. Badala yake, watakuwa kitanzi na mtego kwenu, viboko migongoni mwenu na miiba machoni mwenu, mpaka pale mtakapoangamia katika nchi hii nzuri ambayo Yahweh Mungu wenu amewapeni ninyi.
know for a certainty that the LORD your God will no more drive these nations from out of your sight; but they shall be a snare and a trap unto you, and a scourge in your sides, and pricks in your eyes, until ye perish from off this good land which the LORD your God hath given you.
14 Na sasa ninaenda katika njia ya dunia yote, na mnajua kwa moyo na roho zenu zote kwamba hakuna hata neno moja ambalo halijatimia kati ya mambo yote mazuri ambayo Yahweh Mungu wenu aliyaahidi juu yenu. Vitu hivi vyote vimetokea kwa ajili yenu. Hakuna hata moja lililoshindikana.
And, behold, this day I am going the way of all the earth; consider ye therefore in all your heart and in all your soul, that not one thing hath failed of all the good things which the LORD your God spoke concerning you; all are come to pass unto you, not one thing hath failed thereof.
15 Lakini kama kila neno ambalo Yahweh Mungu wenu alilowaahidi limekwisha kutimia, hivyo Yahweh atawaletea juu yenu mabaya yote mpaka pale atakapokuwa amewaangamiza katika nchi hii nzuri ambayo Yahweh Mungu wenu amewapeni ninyi.
And it shall come to pass, that as all the good things are come upon you of which the LORD your God spoke unto you, so shall the LORD bring upon you all the evil things, until He have destroyed you from off this good land which the LORD your God hath given you.
16 Atafanya hivi kama mtalivunja agano la Yahweh Mungu wenu, ambalo aliwaagizeni kulitunza. Kama mtaenda na kuiabudu miungu mingine na kuiinamia, ndipo hasira ya Yahweh itawaka kinyume nanyi, na ninyi mtaangamia upesi katika nchi nzuri ambayo amekwisha kuwapeni ninyi.”
When ye transgress the covenant of the LORD your God, which He commanded you, and go and serve other gods, and worship them; then shall the anger of the LORD be kindled against you, and ye shall perish quickly from off the good land which He hath given unto you.'

< Yoshua 23 >