< Yohana 1 >

1 Mwanzoni kulikuwako Neno, na Neno alikuwa pamoja na Mungu, na Neno alikuwa Mungu.
In the beginning the Word already was. The Word was with God, and the Word was God.
2 Huyu, Neno, Mwanzoni alikuwa pamoja na Mungu.
In the beginning he was with God.
3 Vitu vyote vilifanyika kupitia yeye, na pasipo yeye hakuna hata kitu kimoja kilichokuwa kimefanyika.
Everything came into being through him; nothing came into being without him.
4 Ndani yake kulikuwa uzima, na huo uzima ulikuwa nuru ya wanadamu wote.
In him was life, the life that was the light of everyone.
5 Nuru yang'aa gizani, wala giza halikuizimisha.
The light shines in the darkness, and the darkness has not extinguished it.
6 Palikuwa na mtu aliyetumwa kutoka kwa Mungu, ambaye jina lake alikuwa Yohana.
God sent a man named John.
7 Alikuja kama shahidi kushuhudia kuhusu ile nuru, ili kwamba wote waweze kuamini kupitia yeye.
He came as a witness to explain about the light so that everyone might believe through him.
8 Yohana hakuwa ile nuru, bali alikuja ili ashuhudie kuhusu ile nuru
He himself was not the light, but he came to witness to the light.
9 Hiyo ilikuwa nuru ya kweli ambayo ilikuwa inakuja katika dunia nayo humtia nuru kila mmoja
The true light was coming into the world to give light to everyone.
10 Alikuwa katika dunia, na dunia iliumbwa kupitia yeye, na dunia haikumjua.
He was in the world, and though the world was made through him, the world didn't know who he was.
11 Alikuja kwa vitu vyake, na watu wake hawakumpokea.
He came to his own people, but they didn't accept him.
12 Bali kwa wale wengi waliompokea, ambao waliamini jina lake, kwa hao aliwapa haki ya kuwa wana wa Mungu,
But to all those who accepted him and trusted in him, he gave the right to become God's children.
13 Ambao walizaliwa, sio kwa damu, wala kwa mapenzi ya mwili, wala kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu mwenyewe.
These are the children born not in the usual way, not as the result of human desire or a father's decision, but born of God.
14 Naye Neno alifanyika mwili na akaishi miongoni mwetu, tumeuona utukufu wake, utukufu kama wa mtu pekee wa kipekee aliyekuja kutoka kwa Baba, amejaa neema na kweli.
The Word became human and lived among us, and we saw his glory, the glory of the Father's one and only Son, full of grace and truth.
15 Yohana alishuhudia kuhusu yeye, na alipaza sauti akisema, “Huyu ndiye ambaye nilisema habari zake nikisema, “Yule ajaye baada yangu ni mkuu kuliko mimi, kwa sababu amekuwako kabla yangu.”
John gave his testimony about him, shouting out to the people, “This is the one I was telling you about when I said, ‘The one who is coming after me is more important than me, for before I ever existed he already was.’”
16 Kwa kuwa kutoka katika utimilifu wake, sisi sote tumepokea bure kipawa baada ya kipawa.
We have all been recipients of his generous nature, one gracious gift after another.
17 Kwa kuwa sheria ililetwa kupitia Musa. Neema na kweli vilikuja kupitia Yesu Kristo.
The law was given through Moses; grace and truth came through Jesus Christ.
18 Hakuna mwanadamu aliyemwona Mungu wakati wowote. Mtu pekee ambaye ni Mungu, aliye katika kifua cha Baba, amemfanya yeye ajulikane.
While no one has ever seen God, God the one and only, who is close to the Father, has shown us what God is like.
19 Na huu ndio ushuhuda wa Yohana wakati makuhani na walawi waliotumwa kwake na Wayahudi kumwuliza, “Wewe ni nani?”
This is what John publicly stated when the Jewish leaders sent priests and Levites from Jerusalem to ask him, “Who are you?”
20 Bila kusitasita na hakukana, bali alijibu, “Mimi sio Kristo.”
John declared plainly and clearly without hesitation, “I am not the Messiah.”
21 Hivyo wakamuuliza, “kwa hiyo wewe ni nani sasa?” Wewe ni Eliya? Akasema, “Mimi siye.” Wakasema, Wewe ni nabii? Akajibu,” Hapana.”
“So then, who are you?” they asked. “Elijah?” “No, I'm not,” he answered. “Are you the Prophet?” “No,” he replied.
22 Kisha wakamwambia, “Wewe ni nani, ili kwamba tuwape jibu waliotutuma”? Wajishuhudiaje wewe mwenyewe?”
“Well, who are you, then?” they asked. “We have to give an answer to those who sent us. What do you say about yourself?”
23 Akasema, “Mimi ni sauti yake aliaye nyikani: 'Inyosheni njia ya Bwana,' kama nabii Isaya alivyosema.”
“I am a voice calling in the desert, ‘Make the Lord's way straight!’” he said, using the words of the prophet Isaiah.
24 Basi kulikuwa na watu wametumwa pale kutoka kwa Mafarisayo. Wakamuuliza na kusema,
The priests and Levites sent by the Pharisees
25 “Kwa nini unabatiza basi kama wewe sio Kristo wala Eliya wala nabii?”
asked him, “Why then are you baptizing, if you're not the Messiah, or Elijah, or the Prophet?”
26 Yohana aliwajibu akisema, “Ninabatiza kwa maji. Hata hivyo, miongoni mwenu anasimama mtu msiyemtambua.
John replied, “I baptize with water, but standing among you is someone you don't know.
27 Huyu ndiye ajaye baada yangu. Mimi sisitahili kulegeza kamba za viatu vyake.”
He is coming after me, but I am not even worthy to untie his sandals.”
28 Mambo haya yalitendeka huko Bethania, ng'ambo ya Yordani, mahali ambapo Yohana alikuwa akibatiza.
This all happened in Bethany beyond the Jordan, where John was baptizing.
29 Siku iliyofuata Yohana alimwona Yesu akija kwake akasema, “Tazama mwanakondoo wa Mungu aichukuae dhambi ya ulimwengu!
The next day John saw Jesus approaching him, and said, “Look, the Lamb of God, who takes away the sin of the world!
30 huyu ndiye niliyesema habari zake nikisema, “Yeye ajaye nyuma yangu ni mkuu kuliko mimi, kwa kuwa alikuwa kabla yangu.'
This is the one I was talking about when I said, ‘A man who is coming after me is more important than me, for before I ever existed he already was.’
31 Sikumtambua yeye, lakini ilifanyika hivyo ili kwamba afunuliwe katika Israeli, kwamba nilikuja nikibatiza kwa maji.”
I didn't know myself who he was, but I came baptizing with water so that he could be revealed to Israel.”
32 Yohana alishuhudia, “Niliona Roho akishuka kutoka mbinguni mfano wa hua, na ilibaki juu yake.
John gave his evidence about him, saying, “I saw the Spirit descend from heaven like a dove and rest upon him.
33 Mimi sikumtambua lakini yeye aliyenituma ili nibatize kwa maji aliniambia, 'yule ambaye utaona Roho akishuka na kukaa juu yake, Huyo ndiye abatizaye kwa Roho Mtakatifu.'
I wouldn't have known him except he who sent me to baptize with water had told me, ‘The one you see the Spirit descend to and rest upon, he is the one who baptizes with the Holy Spirit.’
34 Nimeona na nimeshuhudia kwamba huyu ni Mwana wa Mungu.”
I saw it happen and I declare that this is the Son of God.”
35 Tena siku iliyofuata Yohana alikuwa amesimama pamoja na wanafunzi wake wawili,
The next day John was standing there with two of his disciples.
36 walimwona Yesu akitembea na Yohana akasema, “Tazama, Mwana kondoo wa Mungu!”
He saw Jesus passing by, and said, “Look! This is the Lamb of God!”
37 Wanafunzi wawili walimsikia Yohana akisema haya wakamfuata Yesu.
When the two disciples heard what he said they went and followed Jesus.
38 Tena Yesu aligeuka na kuwaona wanafunzi wale wakimfuata, na akawambia, “Mnataka nini?” Wakajibu, “Rabbi, (maana yake 'mwalimu,' unaishi wapi?”
Jesus turned round and saw them following him. “What are you looking for?” he asked them. “Rabbi (which means ‘Teacher’), where are you staying?” they asked in reply.
39 Akawambia, “Njooni na mwone.”Kisha walikwenda na kuona mahali alipokuwa akiishi; walikaa pamoja naye siku hiyo, kwa kuwa ilikuwa yapata kama saa kumi hivi.
“Come and see,” he told them. So they went with him and saw where he was staying. It was about four p.m., and they spent the rest of the day with him.
40 Mmoja wa wale wawili waliomsikia Yohana akiongea na kisha kumfuata Yesu alikuwa ni Andrea, ndugu yake Simoni Petro.
Andrew, the brother of Simon Peter, was one of these two disciples who had heard what John said and followed Jesus.
41 Akamwona ndugu yake Simoni na akamwambia, “Tumempata Masihi” (ambayo inatafsiriwa Kristo).
He went at once to find his brother Simon and told him, “We've found the Messiah!” (which means “Christ”).
42 Akamleta kwa Yesu. Yesu akamtazama na akasema, “Wewe ni Simoni mwana wa Yohana” utaitwa Kefa,” (maana yake 'Petro').
He took him to Jesus. Looking directly at Simon, Jesus said, “You are Simon, son of John. But now you will be called Cephas,” (which means “Peter”).
43 Siku iliyofuata wakati Yesu alipotaka kuondoka kwenda Galilaya, alimpata Filipo na akamwambia, “Nifuate mimi.”
The next day Jesus decided to go to Galilee. Jesus found Philip there, and told him, “Follow me.”
44 Filipo alikuwa ni mwenyeji wa Bethsaida, mji wa Andrea na Petro.
Philip was from Bethsaida, the same town that Andrew and Peter came from.
45 Filipo alimpata Nathanaeli na kumwambia, Tumempata yule ambaye Musa aliandika habari zake katika sheria na Manabii. Yesu mwana wa Yusufu, kutoka Nazareti.
Philip found Nathanael and told him, “We've found the one that Moses wrote about in the law and that the prophets did too—Jesus of Nazareth, the son of Joseph.”
46 Nathanaeli akamwambia, “Je kitu chema chaweza kutokea Nazareti?” Filipo akamwambia, Njoo na uone.”
“From Nazareth? Can anything good come from there?” Nathanael wondered. “Just come and see,” Philip replied.
47 Yesu akamwona Nathanaeli akija kwake na akasema, “Tazama, Mwisraeli kweli kweli asiye na udanganyifu ndani yake!”
As Jesus saw Nathanael approaching, he said about him, “Look, here's a true Israelite! There's nothing false about him.”
48 Nathanaeli akamwambia, “Umenifahamuje mimi?” Yesu akajibu na akamwambia, “Kabla Filipo hajakuita ulipokuwa chini ya mtini, nalikuona.”
“How do you know who I am?” Nathanael asked. “I saw you there under the fig tree, before Philip called you,” Jesus replied.
49 Nathanaeli akajibu, “Rabi wewe u Mwana wa Mungu! Wewe ni Mfalme wa Israeli”!
“Rabbi, you are the Son of God, the king of Israel!” Nathaniel exclaimed.
50 Yesu akajibu akamwambia, Kwa sababu nilikuambia 'nilikuona chini ya mtini' je waamini? utaona matendo makubwa kuliko haya.”
“You believe this just because I told you I saw you under the fig tree?” Jesus replied. “You'll get to see much more than that!”
51 Yesu akasema, “Amini amini nawambieni mtaziona mbingu zikifunguka, na kuwaona malaika wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Adamu.”
Then Jesus said, “I tell you the truth, you will all see heaven open, and the angels of God going up and down on the Son of man.”

< Yohana 1 >