< Yohana 8 >

1 (Zingatia: Angalia ufafanuzi wa Yohana 7: 53 - 8: 11 hapo juu). Yesu alienda mlima wa Mizeituni.
mais Jésus s'est rendu sur le mont des Oliviers.
2 Mapema asubuhi akaja tena hekaluni, na watu wote wakamwendea; akakaa na kuwafundisha.
Or, de grand matin, il entra de nouveau dans le temple, et tout le peuple vint à lui. Il s'assit et les enseigna.
3 Waandishi na Mafarisayo wakamletea mwanamke aliyekamatwa katika kitendo cha kuzini. Wakamweka katikati.
Les scribes et les pharisiens amenèrent une femme surprise en adultère. L'ayant placée au milieu,
4 (Zingatia: Angalia ufafanuzi wa Yohana 7: 53 - 8: 11 hapo juu). Ndipo wakamwambia Yesu, “Mwalimu, mwanamke huyu amekamatwa katika uzinzi, katika kitendo kabisa.
ils lui dirent: Maître, nous avons trouvé cette femme adultère, en flagrant délit.
5 Sasa, katika sheria, Musa ametuamuru kuwaponda mawe watu kama hawa, unasemaje juu yake?
Or, dans notre loi, Moïse nous a ordonné de lapider de telles femmes. Que dis-tu donc d'elle? »
6 Walisema haya ili kumtega ili kwamba wapate jambo la kumshitaki, lakini Yesu akainama chini akaandika katika ardhi kwa kidole chake.
Ils dirent cela pour l'éprouver, afin d'avoir quelque chose à lui reprocher. Mais Jésus se baissa et écrivit sur la terre avec son doigt.
7 (Zingatia: Angalia ufafanuzi wa Yohana 7: 53 - 8: 11 hapo juu). Walipoendelea kumwuliza, alisimama na kuwaambia, “Yeye asiyekuwa na dhambi miongoni mwenu, awe wa kwanza kumponda mawe.”
Comme ils continuaient à l'interroger, il leva les yeux et leur dit: « Que celui d'entre vous qui est sans péché lui jette la première pierre. »
8 Akainama tena chini, akaandika katika ardhi kwa kidole chake.
De nouveau, il se baissa et écrivit sur la terre avec son doigt.
9 (Zingatia: Angalia ufafanuzi wa Yohana 7: 53 - 8: 11 hapo juu). Waliposikia hayo, waliondoka mmoja baada ya mwingine, kuanzia aliye mzee. Mwishowe Yesu aliachwa peke yake, pamoja na mwanamke aliyekuwa katikati yao.
Ceux-ci, après avoir entendu cela, convaincus par leur conscience, sortirent un par un, depuis le plus âgé jusqu'au dernier. Jésus resta seul avec la femme, là où elle était, au milieu.
10 Yesu alisimama na kumwambia, “Mwanamke, waliokushitaki wako wapi? Hakuna hata mmoja aliyekuhukumu?”
Jésus, s'étant levé, la vit et dit: « Femme, où sont tes accusateurs? Personne ne t'a condamnée? »
11 Akasema, “Hakuna hata mmoja Bwana.” Yesu akasema, “Hata mimi sikuhukumu. Nenda njia yako; kuanzia sasa na kuendelea usitende dhambi tena.”
Elle a dit: « Personne, Seigneur. » Jésus a dit: « Je ne te condamne pas non plus. Va ton chemin. Désormais, ne pèche plus. »
12 Tena Yesu akazungumza na watu akisema, “Mimi ni nuru ya ulimwengu; yeye anifuataye hatatembea gizani bali atakuwa na nuru ya uzima.”
Jésus leur parla de nouveau, en disant: « Je suis la lumière du monde. Celui qui me suit ne marchera pas dans les ténèbres, mais il aura la lumière de la vie. »
13 Mafarisayo wakamwambia, “Unajishuhudia mwenyewe; ushuhuda wako siyo wa kweli.”
Les pharisiens lui dirent donc: « Tu témoignes de toi-même. Ton témoignage n'est pas valable. »
14 Yesu alijibu akawaambia, “Hata kama nitajishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu ni kweli. Ninajua mahali nilikotoka na kule ninakoenda, lakini ninyi hamjui mahali ninapotoka au kule ninakoenda.
Jésus leur répondit: « Même si je rends témoignage de moi-même, mon témoignage est vrai, car je sais d'où je viens et où je vais; mais vous, vous ne savez ni d'où je viens ni où je vais.
15 Nyinyi mnahukumu kimwili; mimi simhukumu yeyote.
Vous jugez selon la chair. Moi, je ne juge personne.
16 Mimi hata nikihukumu, hukumu yangu ni kweli kwa sababu siko peke yangu, bali niko pamoja na baba aliyenituma.
Et quand bien même je jugerais, mon jugement est vrai, car je ne suis pas seul, mais je suis avec le Père qui m'a envoyé.
17 Ndiyo, na katika sheria yenu imeandikwa kwamba ushuhuda wa watu wawili ni kweli.
Il est aussi écrit dans votre loi que le témoignage de deux personnes est valable.
18 Mimi ndiye ninayejishuhudia, na Baba aliyenituma ananishuhudia.”
Moi, je suis celui qui rend témoignage de moi-même, et le Père qui m'a envoyé rend témoignage de moi. »
19 Wakamwambia, “Baba yako yuko wapi?” Yesu akajibu, “mimi hamnijui wala Baba yangu hammjui; mngelikuwa mnanijua mimi, mngemjua na Baba yangu pia.”
Ils lui dirent donc: « Où est ton Père? » Jésus répondit: « Vous ne connaissez ni moi ni mon Père. Si vous me connaissiez, vous connaîtriez aussi mon Père. »
20 Alisema maneno haya akiwa karibu na hazina alipokuwa akifundisha hekaluni, na hakuna hata mmoja aliyemkamata kwa sababu saa yake ilikuwa bado haijafika.
Jésus prononça ces paroles dans le trésor, comme il enseignait dans le temple. Et personne ne l'arrêta, parce que son heure n'était pas encore venue.
21 Basi akawaambia tena, “Ninaenda zangu; mtanitafuta na mtakufa katika dhambi zenu. Kule niendako, hamuwezi kuja.”
Jésus leur dit donc encore: « Je m'en vais, et vous me chercherez, et vous mourrez dans vos péchés. Là où je vais, vous ne pouvez pas venir. »
22 Wayahudi wakasema, “Atajiua mwenyewe, yeye ambaye alisema, 'kule niendako hamuwezi kuja'?”
Les Juifs dirent donc: « Se tuera-t-il, parce qu'il dit: « Où je vais, vous ne pouvez pas venir »? »
23 Yesu akawaambia, “Mnatoka chini; mimi natoka juu. Ninyi ni wa Ulimwengu huu; mimi si wa ulimwengu huu.
Il leur dit: « Vous êtes d'en bas. Moi, je suis d'en haut. Vous êtes de ce monde. Je ne suis pas de ce monde.
24 Kwa hiyo, naliwaambieni kuwa mtakufa katika dhambi zenu. Vinginevyo muamini kuwa MIMI NDIYE, mtakufa katika dhambi zenu”.
Je vous ai donc dit que vous mourrez dans vos péchés; car si vous ne croyez pas que je suis lui, vous mourrez dans vos péchés. »
25 Kwa hiyo wakamwambia, “Wewe ni nani?” Yesu akawaambia, Yale niliyowaambia tangu mwanzo.
Ils lui dirent donc: « Qui es-tu? » Jésus leur dit: « Ce que je vous dis depuis le commencement.
26 Ninayo mambo mengi ya kuzungumza na kuhukumu juu yenu. Hata hivyo, yeye aliyenituma ni wa kweli; na mambo niliyoyasikia kutoka kwake, mambo haya nayasema kwa Ulimwengu.”
J'ai beaucoup de choses à dire et à juger à votre sujet. Mais celui qui m'a envoyé est vrai; et ce que j'ai entendu de lui, je le dis au monde entier. »
27 Hawakumuelewa kwamba alikuwa akiongea nao kuhusu Baba.
Ils ne comprenaient pas qu'il leur parlait du Père.
28 Yesu akasema, “Mtakapomwinua juu Mwana wa Mtu, ndipo mtakapojua kuwa MIMI NDIYE, na kwamba sifanyi lolote kwa nafsi yangu. Kama Baba alivyonifundisha, ninazungumza mambo haya.
Jésus leur dit donc: « Quand vous aurez élevé le Fils de l'homme, vous saurez que c'est moi, et je ne fais rien de moi-même; mais c'est comme mon Père me l'a enseigné que je dis ces choses.
29 Yeye aliyenituma yuko pamoja nami, na yeye hajaniacha peke yangu, kwani kila mara nafanya yale yanayompendeza.”
Celui qui m'a envoyé est avec moi. Le Père ne m'a pas laissé seul, car je fais toujours ce qui lui est agréable. »
30 Wakati Yesu akisema mambo haya, wengi walimwamini.
Comme il parlait ainsi, beaucoup crurent en lui.
31 Yesu akasema kwa wale Wayahudi waliomwamini, “Ikiwa mtakaa katika neno langu, ndipo mtakuwa wanafunzi wangu kweli,
Jésus dit donc aux Juifs qui avaient cru en lui: « Si vous demeurez dans ma parole, vous êtes vraiment mes disciples.
32 nanyi mtaijua kweli, na kweli itawaweka huru.”
Vous connaîtrez la vérité, et la vérité vous rendra libres. »
33 Walimjibu, “Sisi ni uzao wa Ibrahimu na kamwe hatujawahi kwa chini ya utumwa wa yeyote; utasemaje, “Tutawekwa huru?”
Ils lui répondirent: « Nous sommes la descendance d'Abraham, et nous n'avons jamais été asservis à personne. Comment peux-tu dire: « Vous serez libérés »? »
34 Yesu aliwajibu, “Amini, amini, nawaambia, kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi.
Jésus leur répondit: Je vous le dis en vérité, quiconque commet un péché est esclave du péché.
35 Mtumwa hakai nyumbani wakati wote; mwana hudumu siku zote. (aiōn g165)
Un esclave ne demeure pas toujours dans la maison. Un fils demeure pour toujours. (aiōn g165)
36 Kwa hiyo, ikiwa Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kabisa.”
Si donc le Fils vous rend libres, vous serez vraiment libres.
37 Ninajua kwamba ninyi ni uzao wa Ibrahimu; mnatafuta kuniua kwa sababu neno langu halina nafasi ndani yenu.
Je sais que vous êtes la postérité d'Abraham, et pourtant vous cherchez à me tuer, parce que ma parole ne trouve pas de place en vous.
38 Ninasema mambo ambayo nimeyaona pamoja na Baba yangu, na ninyi vile vile mnafanya mambo ambayo mliyasikia kutoka kwa baba yenu.”
Je dis les choses que j'ai vues avec mon Père; et vous aussi, vous faites les choses que vous avez vues avec votre père. »
39 Walijibu na kumwambia, “Baba yetu ni Abrahamu.” Yesu akawaambia, Kama mngelikuwa watoto wa Ibrahimu, mngefanya kazi za Ibrahimu.
Ils lui répondirent: « Notre père est Abraham. » Jésus leur dit: « Si vous étiez les enfants d'Abraham, vous feriez les œuvres d'Abraham.
40 Hata sasa mnatafuta kuniua, mtu aliyewaambia ukweli kwamba nilisikia kutoka kwa Mungu. Abrahamu hakufanya hivi.
Mais maintenant vous cherchez à me tuer, moi qui vous ai dit la vérité que j'ai entendue de Dieu. Ce n'est pas Abraham qui a fait cela.
41 Mnafanya kazi za baba yenu.” Wakamwambia, “Hatukuzaliwa katika uzinzi, tunaye Baba mmoja, Mungu.”
Vous faites les œuvres de votre père. » Ils lui dirent: « Nous ne sommes pas nés de l'immoralité sexuelle. Nous avons un seul Père, Dieu. »
42 Yesu akawaambia, “Ikiwa Mungu ni Baba yenu, mngenipenda mimi, kwa maana nimetoka kwa Mungu; wala sikuja kwa nafsi yangu, bali yeye alinituma.
C'est pourquoi Jésus leur dit: « Si Dieu était votre père, vous m'aimeriez, car je suis sorti et je suis venu de Dieu. Car je ne suis pas venu de moi-même, mais c'est lui qui m'a envoyé.
43 Kwa nini hamyaelewi maneno yangu? Kwa sababu hamuwezi kuvumilia kuyasikia maneno yangu.
Pourquoi ne comprenez-vous pas ma parole? Parce que vous n'entendez pas ma parole.
44 Ninyi ni wa baba yenu, shetani, na mnataka kuzitenda tamaa za baba yenu. Alikuwa mwuaji tangu mwanzo na hawezi kusimama katika kweli kwa sababu kweli haimo ndani yake. Anapoongea uongo, anaongea kutoka kwenye asili yake kwa sababu ni mwongo na baba wa uongo.
Vous êtes de votre père le diable, et vous voulez faire les désirs de votre père. Il a été meurtrier dès le commencement, et il ne tient pas dans la vérité, parce qu'il n'y a pas de vérité en lui. Quand il dit un mensonge, il parle de lui-même, car il est menteur et père du mensonge.
45 Hata sasa, kwa sababu ninasema iliyo kweli, hamniamini.
Mais parce que je dis la vérité, vous ne me croyez pas.
46 Ni nani kati yenu anayenishuhudia kuwa nina dhambi? ikiwa ninasema iliyo kweli, kwa nini hamniamini?
Lequel d'entre vous me convainc de péché? Si je dis la vérité, pourquoi ne me croyez-vous pas?
47 Yeye aliye wa Mungu huyasikia maneno ya Mungu; ninyi hamyasikii kwa sababu ninyi si wa Mungu.”
Celui qui est de Dieu entend les paroles de Dieu. C'est pourquoi vous n'entendez pas, parce que vous n'êtes pas de Dieu. »
48 Wayahudi wakamjibu na kumwambia, hatujasema kweli kuwa wewe ni Msamaria na una pepo?”
Alors les Juifs lui répondirent: « Ne disons-nous pas bien que tu es un Samaritain, et que tu as un démon? »
49 Yesu akajibu, sina pepo; lakini namheshimu Baba yangu, nanyi hamniheshimu.
Jésus répondit: « Je n'ai pas de démon, mais j'honore mon Père et vous me déshonorez.
50 Sitafuti utukufu wangu; kuna mmoja atafutaye na kuhukumu.
Mais je ne cherche pas ma propre gloire. Il y a quelqu'un qui cherche et qui juge.
51 Amini, amini, nawaambia, iwapo yeyote atalishika neno langu, hataona mauti kamwe.” (aiōn g165)
En vérité, je vous le dis, si quelqu'un garde ma parole, il ne verra jamais la mort. » (aiōn g165)
52 Wayahudi wakamwambia, “Sasa tumejua kuwa una pepo. Abrahamu na mabii walikufa; lakini unasema, 'Ikiwa mtu atalishika neno langu, hataonja mauti'. (aiōn g165)
Alors les Juifs lui dirent: « Nous savons maintenant que tu as un démon. Abraham est mort, ainsi que les prophètes; et toi, tu dis: « Si quelqu'un garde ma parole, il ne goûtera jamais à la mort. (aiōn g165)
53 Wewe si mkuu kuliko baba yetu Abrahamu aliyekufa, sivyo? Manabii pia walikufa. Wewe wajifanya kuwa nani?”
Es-tu plus grand que notre père Abraham, qui est mort? Les prophètes sont morts. Pour qui te prends-tu? »
54 Yesu akajibu, “Ikiwa nitajitukuza mwenyewe, utukufu wangu ni bure; ni Baba yangu anayenitukuza - yule mnayemsema kuwa ni Mungu wenu.
Jésus répondit: « Si je me glorifie moi-même, ma gloire n'est rien. C'est mon Père qui me glorifie, lui dont vous dites qu'il est notre Dieu.
55 Ninyi hamjamjua yeye, lakini mimi namjua yeye. Ikiwa nitasema, 'simjui,' nitakuwa kama nyinyi, muongo. Hata hivyo, ninamjua na maneno yake nimeyashika.
Vous ne l'avez pas connu, mais moi, je le connais. Si je disais: « Je ne le connais pas », je serais comme vous, un menteur. Mais moi, je le connais et je garde sa parole.
56 Baba yenu Abrahamu alishangilia atakavyoiona siku yangu; aliiona na alifurahi.”
Ton père Abraham s'est réjoui de voir mon jour. Il l'a vu et s'est réjoui. »
57 Wayahudi wakamwambia,”Haujafikisha umri wa miaka hamsini bado, nawe umemuona Ibrahimu?”
Les Juifs lui dirent donc: « Tu n'as pas encore cinquante ans! As-tu vu Abraham? »
58 Yesu akawaambia, “Amini, amini, nawaambia, kabla Abrahamu hajazaliwa, MIMI NIKO.”
Jésus leur dit: « En vérité, je vous le dis, avant qu'Abraham n'existe, JE SUIS. »
59 Ndipo waliokota mawe wapate kumpiga, lakini Yesu alijificha na akatoka nje ya hekalu.
Ils prirent donc des pierres pour les jeter contre lui, mais Jésus se cacha et sortit du temple, après avoir traversé le milieu d'eux, et il passa ainsi.

< Yohana 8 >