< Yohana 12 >

1 Siku sita kabla ya Pasaka, Yesu alienda Bethania, alipokuwapo Lazaro, yeye ambaye alimfufua kutoka katika wafu.
Six jours avant la Pâque, Jésus se rendit à Béthanie, où était Lazare, qui était mort, et qu'il avait ressuscité des morts.
2 Basi wakamwandalia chakula cha jioni huko, na Martha akamtumikia, wakati huo Lazaro alikuwa mmoja wapo wa wale walioketi chakulani pamoja na Yesu.
Là, on lui fit un souper. Marthe servait, mais Lazare était du nombre de ceux qui étaient à table avec lui.
3 Kisha Mariamu akachukua ratli ya manukato yaliyotengenezwa kwa nardo safi, yenye thamani kubwa, akampaka Yesu miguuni, na kumfuta miguu kwa nywele zake; nyumba yote ilijaa harufu ya manukato.
Marie prit une livre d'onguent de nard pur, très précieux, et elle oignit les pieds de Jésus; elle lui essuya les pieds avec ses cheveux. La maison fut remplie de l'odeur du parfum.
4 Yuda Iskariote, mmoja wa wale wanafunzi wake, ambaye ndiye atakayemsaliti Yesu, akasema,
Alors Judas Iscariote, fils de Simon, l'un de ses disciples, qui allait le trahir, dit:
5 “Kwanini manukato haya yasingeuzwa kwa dinari mia tatu na wakapewa maskini?”
« Pourquoi ce parfum n'a-t-il pas été vendu trois cents deniers et donné aux pauvres? »
6 Naye aliyasema hayo, si kwa kuwahurumia maskini, bali kwa sababu alikuwa mwizi: yeye ndiye aliyeshika mfuko wa fedha na alikuwa anachukua baadhi ya vilivyowekwa humo kwa ajili yake mwenyewe.
Il disait cela, non qu'il se souciât des pauvres, mais parce qu'il était voleur et qu'ayant la tirelire, il avait l'habitude de voler ce qu'on y mettait.
7 Yesu alisema, “Mwache aweke alicho nacho kwa ajili ya siku ya maziko yangu.
Mais Jésus dit: « Laisse-la tranquille. Elle a gardé cela pour le jour de ma sépulture.
8 Maskini mtakuwa nao siku zote; lakini hamtakuwa nami siku zote.”
Car vous avez toujours les pauvres avec vous, mais vous ne m'avez pas toujours, moi. »
9 Basi umati mkubwa wa Wayahudi walipata kujua ya kuwa Yesu yuko huko, nao wakaja, si kwa ajili ya Yesu tu, ila wamwone na Lazaro ambaye Yesu alimfufua kutoka katika wafu.
Une grande foule de Juifs apprit donc qu'il était là, et ils vinrent, non seulement à cause de Jésus, mais aussi pour voir Lazare, qu'il avait ressuscité des morts.
10 Nao wakuu wa makuhani wakafanya shauri ili wamue Lazaro;
Mais les principaux sacrificateurs complotèrent de faire mourir aussi Lazare,
11 maana kwa ajili yake wengi katika Wayahudi walienda zao na wakamwamini Yesu.
parce que, à cause de lui, beaucoup de Juifs s'en allèrent et crurent en Jésus.
12 Na siku ya pili yake umati mkubwa walikuja kwenye sikukuu. Waliposikia ya kuwa Yesu anakuja Yerusalemu,
Le lendemain, une grande foule était venue à la fête. Lorsqu'ils apprirent que Jésus venait à Jérusalem,
13 walichukua matawi ya miti ya mitende na kutoka nje kwenda kumlaki na wakapiga kelele, “Hosana! Amebarikiwa yeye ajaye kwa jina la Bwana, Mfalme wa Israeli.”
ils prirent les branches des palmiers, sortirent à sa rencontre et s'écrièrent: « Hosanna! Béni soit celui qui vient au nom du Seigneur, le roi d'Israël! »
14 Yesu alimpata mwana-punda akampanda; kama vile ilivyoandikwa,
Jésus, ayant trouvé un jeune âne, s'assit dessus. Selon qu'il est écrit:
15 “Usiogope, binti Sayuni; tazama, Mfalme wako anakuja, amepanda mwana-punda.”
« Ne crains pas, fille de Sion. Voici que ton Roi vient, assis sur un ânon. »
16 Wanafunzi wake hawakuyaelewa mambo haya hapo kwanza; lakini Yesu alipotukuzwa, ndipo walipokumbuka ya kuwa mambo haya aliandikiwa yeye na ya kwamba wametenda mambo haya kwake.
Ses disciples ne comprirent pas d'abord ces choses; mais, lorsque Jésus fut glorifié, ils se souvinrent que ces choses étaient écrites de lui, et qu'ils les avaient faites pour lui.
17 Basi lile kundi la watu waliokuwepo pamoja na Yesu wakati alipomwita Lazaro kutoka kaburini, wakashuhudia kwa wengine.
La foule qui était avec lui, lorsqu'il appela Lazare hors du sépulcre et le ressuscita des morts, rendait donc témoignage à ce sujet.
18 Na ilikuwa kwa sababu hii pia kwamba kundi la watu walikwenda kumlaki kwasababu walisikia ya kwamba ameifanya ishara hiyo.
C'est pourquoi aussi la foule alla au-devant de lui, parce qu'elle avait appris qu'il avait fait ce miracle.
19 Mafarisayo wakasemezana wao kwa wao, “Tazama, sasa hamwezi kufanya lolote; tazama, ulimwengu umekwenda kwake.”
Les pharisiens se dirent alors entre eux: « Voyez comme vous ne faites rien. Voici que le monde est allé après lui. »
20 Sasa baadhi ya Wayunani walikuwa miongoni mwa wale waliokuwa wakienda kuabudu kwenye sikukuu.
Or, il y avait quelques Grecs parmi ceux qui montaient se prosterner à la fête.
21 Hawa walimwendea Filipo, ambaye alitoka Bethsaida ya Galilaya, wakamwomba wakisema, “Bwana, sisi tunatamani kumwona Yesu.”
Ils vinrent donc trouver Philippe, qui était de Bethsaïda en Galilée, et lui demandèrent: « Seigneur, nous voulons voir Jésus. »
22 Filipo akaenda akamwambia Andrea; Andrea na Filipo wakaenda na kumwambia Yesu.
Philippe vint le dire à André; et André vint à son tour avec Philippe, et ils le dirent à Jésus.
23 Yesu akawajibu akasema, “Saa imefika kwa ajili ya Mwana wa Adamu kutukuzwa.
Jésus leur répondit: « Le temps est venu où le Fils de l'homme sera glorifié.
24 Amini, amini, nawaambia, chembe ya ngano isipoanguka katika nchi ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, itazaa matunda mengi.
Je vous le dis en vérité, si le grain de blé ne tombe en terre et ne meurt, il reste seul. Mais s'il meurt, il porte beaucoup de fruit.
25 Yeye apendaye uhai wake ataupoteza; bali yeye auchukiaye uhai wake katika ulimemngu huu atausalimisha hata uzima wa milele. (aiōnios g166)
Celui qui aime sa vie la perdra. Celui qui hait sa vie dans ce monde la gardera pour la vie éternelle. (aiōnios g166)
26 Mtu yeyote akinitumikia mimi, na anifuate; nami nilipo, ndipo na mtumishi wangu atakapokuwapo. Mtu yeyote akinitumikia, Baba atamheshimu.
Si quelqu'un me sert, qu'il me suive. Là où je suis, là aussi sera mon serviteur. Si quelqu'un me sert, le Père l'honorera.
27 Sasa roho yangu imefadhaika: nami nisemeje? 'Baba, uniokoe katika saa hii'? Lakini ni kwa kusudi hii nimeifikia saa hii.
« Maintenant mon âme est troublée. Que dirai-je? « Père, sauve-moi de ce temps »? Mais c'est pour cette cause que je suis arrivé à ce moment.
28 Baba, ulitukuze jina lako.” Kisha sauti ikaja kutoka mbinguni na kusema, “Nimelitukuza nami nitalitukuza tena.”
Père, glorifie ton nom! » Alors une voix sortit du ciel, disant: « Je l'ai glorifié et je le glorifierai encore. »
29 Basi mkutano uliosimama karibu naye wakasikia, wakasema ya kwamba kumekuwa ngurumo. Wengine walisema, “Malaika amesema naye.”
C'est pourquoi la foule qui se tenait là et qui l'entendait disait que c'était un tonnerre. D'autres disaient: « Un ange lui a parlé. »
30 Yesu akajibu na kusema, “Sauti hii haikuja kwa ajili yangu, bali kwa ajili yenu.
Jésus répondit: « Cette voix n'est pas venue à cause de moi, mais à cause de vous.
31 Sasa hukumu ya ulimwengu huu ipo: Sasa mkuu wa ulimwngu huu atatupwa nje.
Maintenant, c'est le jugement de ce monde. Maintenant, le prince de ce monde sera chassé.
32 Nami nikiinuliwa juu ya nchi, nitawavuta wote kwangu.”
Et moi, si je suis élevé de la terre, j'attirerai à moi tous les peuples. »
33 Aliyanena hayo akionesha ni mauti gani atakayokufa.
Mais il disait cela en indiquant par quel genre de mort il devait mourir.
34 Mkutano wakamjibu, “Sisi tumesikia katika sheria ya kwamba Kristo atadumu hata milele. Nawe wasemaje, 'Mwana Adamu lazima ainuliwe juu'? Huyu Mwana wa Mtu ni nani?” (aiōn g165)
La foule lui répondit: « Nous avons appris par la loi que le Christ demeure éternellement. Comment dis-tu: « Il faut que le Fils de l'homme soit élevé »? Qui est ce Fils de l'homme? » (aiōn g165)
35 Basi Yesu akawaambia, “Nuru ingalipo pamoja nanyi muda kidogo. Enendeni maadamu mnayo nuru, ili kwamba giza lisije likawaweza. Yeye aendaye gizani hajui aendako.
Jésus leur dit donc: « La lumière est encore pour un peu de temps avec vous. Marchez pendant que vous avez la lumière, afin que les ténèbres ne vous surprennent pas. Celui qui marche dans les ténèbres ne sait pas où il va.
36 Mngali mnayo nuru, iaminini nuru hiyo ili mpate kuwa wana wa nuru.” Yesu aliyasema haya na kisha akaenda zake akajificha wasimwone.
Pendant que vous avez la lumière, croyez en la lumière, afin de devenir des enfants de lumière. » Jésus dit ces choses, puis il s'en alla et se cacha d'eux.
37 Ingawa Yesu alifanya ishara nyingi namna hiyo mbele yao, bado hawakumwamini
Mais, bien qu'il eût fait devant eux tant de miracles, ils ne crurent pas en lui,
38 ili litimie neno la nabii Isaya, alilosema: “Bwana, ni nani aliyezisadiki habari zetu? Na mkono wa Bwana amefunuliwa nani?”
afin que s'accomplît la parole qu'Ésaïe, le prophète, avait prononcée: « Seigneur, qui a cru à notre rapport? A qui le bras du Seigneur a-t-il été révélé? »
39 Ndio sababu wao hawakuamini, maana Isaya alisema tena,
C'est pour cela qu'ils ne pouvaient pas croire, car Ésaïe a encore dit:
40 “Amewapofusha macho, na ameifanya migumu mioyo yao; wasije wakaona kwa macho yao na wakafahamu kwa mioyo yao, na wakaongoka nami nikawaponya.”
« Il a aveuglé leurs yeux et il a endurci leur cœur, de peur qu'ils ne voient avec leurs yeux, et perçoivent avec leur cœur, et tournerait, et je les guérirais. »
41 Isaya alisema maneno hayo kwa kuwa aliuona utukufu wa Yesu na akanena habari zake.
Ésaïe a dit ces choses en voyant sa gloire, et il a parlé de lui.
42 Walakini, hata wakuu wengi walimwamini Yesu; lakini kwa sababu ya Mafarisayo, hawakukiri ili wasije wakatengwa na sinagogi.
Cependant, beaucoup de chefs croyaient en lui; mais, à cause des pharisiens, ils ne le confessaient pas, afin de ne pas être exclus de la synagogue,
43 Walipenda sifa za wanadamu kuliko sifa zitokazo kwa Mungu.
car ils aimaient mieux les louanges des hommes que celles de Dieu.
44 Yesu akapaza sauti na kusema, “Yeye aniaminiye mimi, haniamini mimi tu bali na yeye aliyenituma mimi,
Jésus s'écria: « Celui qui croit en moi ne croit pas en moi, mais en celui qui m'a envoyé.
45 naye anionaye mimi anamuona yeye aliyenituma.
Celui qui me voit voit celui qui m'a envoyé.
46 Mimi nimekuja kama nuru ulimwenguni ili kila mtu aniaminiye mimi asikae gizani.
Je suis venu comme une lumière dans le monde, afin que quiconque croit en moi ne demeure pas dans les ténèbres.
47 Ikiwa mtu yeyote atayasikia maneno yangu lakini asiyashike, mimi simhukumu; maana sikuja ili niuhukumu ulimwengu, bali niuokoe ulimwengu.
Si quelqu'un écoute mes paroles et ne croit pas, je ne le juge pas. Car je suis venu non pas pour juger le monde, mais pour sauver le monde.
48 Yeye anikataye mimi na asiyeyakubali maneno yangu, anaye amhukumuye: neno hilo nililolinena ndilo litakalomhukumu siku ya mwisho.
Celui qui me rejette, et qui ne reçoit pas mes paroles, a quelqu'un qui le juge. La parole que j'ai prononcée le jugera au dernier jour.
49 Maana mimi sikunena kwa nafsi yangu tu. Bali ni Baba aliyenipeleka, yeye mwenyewe ameniagiza nitakayonena na nitakayosema.
Car je n'ai pas parlé de moi-même, mais le Père qui m'a envoyé m'a donné un commandement, celui de savoir ce que je dois dire et ce que je dois dire.
50 Nami najua ya kuwa agizo lake ni uzima wa milele; basi hayo ninenayo mimi - kama Baba alivyoniambia, ndivyo ninenavyo kwao.” (aiōnios g166)
Je sais que son commandement est la vie éternelle. Les choses donc que je dis, je les dis comme le Père me les a dites. » (aiōnios g166)

< Yohana 12 >