< Ayubu 41 >

1 Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
But will you catch the serpent with a hook, and put a halter about his nose?
2 Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
Or will you fasten a ring in his nostril, and bore his lip with a clasp?
3 Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
Will he address you with a petition? softly, with the voice of a suppliant?
4 Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
And will he make a covenant with you? and will you take him for a perpetual servant?
5 Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
And will you play with him as with a bird? or bind him as a sparrow for a child?
6 Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
And do the nations feed upon him, and the nations of the Phoenicians share him?
7 Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
And all the ships come together would not be able to bear the mere skin of his tail; neither [shall they carry] his head in fishing vessels.
8 Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
But you shall lay your hand upon him [once], remembering the war that is waged by his mouth; and let it not be done any more.
9 Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
Hast you not seen him? and have you not wondered at the things said [of him]?
10 Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
Do you not fear because preparation has been made by me? for who is there that resists me?
11 Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
Or who will resist me, and abide, since the whole [world] under heaven is mine?
12 Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
I will not be silent because of him: though because of his power [one] shall pity his antagonist.
13 Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
Who will open the face of his garment? and who can enter within the fold of his breastplate?
14 Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
Who will open the doors of his face? terror is round about his teeth.
15 Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
His inwards are as brazen plates, and the texture of his [skin] as a smyrite stone.
16 Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
One [part] cleaves fast to another, and the air can’t come between them.
17 Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
They will remain united each to the other: they are closely joined, and can’t be separated.
18 Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
At his sneezing a light shines, and his eyes are [as] the appearance of the morning star.
19 Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
Out of his mouth proceed as it were burning lamps, and as it were hearths of fire are cast abroad.
20 Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
Out of his nostrils proceeds smoke of a furnace burning with fire of coals.
21 Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
His breath is [as] live coals, and a flame goes out of his mouth.
22 Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
And power is lodged in his neck, before him destruction runs.
23 Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
The flesh also of his body is joined together: [if one] pours [violence] upon him, he shall not be moved.
24 Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
His heart is firm as a stone, and it stands like an unyielding anvil.
25 Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
And when he turns, [he is] a terror to the four-footed wild beasts which leap upon the earth.
26 Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
If spears should come against him, [men] will effect nothing, [either with] the spear or the breast-plate.
27 Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
For he considers iron as chaff, and brass as rotten wood.
28 Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
The bow of brass shall not would him, he deems a slinger as grass.
29 Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
Mauls are counted as stubble; and he laughs to scorn the waving of the firebrand.
30 Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
His lair is [formed of] sharp points; and all the gold of the sea under him is an immense [quantity of] clay.
31 Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
He makes the deep boil like a brazen cauldron; and he regards the sea as a pot of ointment,
32 Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
and the lowest part of the deep as a captive: he reckons the deep as [his] range.
33 Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
There is nothing upon the earth like to him, formed to be sported with by my angels.
34 Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”
He beholds every high thing: and he is king of all that are in the waters.

< Ayubu 41 >