< Ayubu 40 >

1 Yahweh aliendelea kuongea na Ayubu na kusema,
And the Lord God answered Job, and said,
2 “Je mtu yeyote anayetaka kukosoa na ajaribu kumsahihisha Mwenye enzi? Na yeye anayehojiana na Mungu, na ajibu yeye.”
Will [any one] pervert judgement with the Mighty One? and he that reproves God, let him return it for answer.
3 Ndipo Ayubu akamjibu Yahweh na kusema, “
And Job answered and said to the Lord,
4 Tazama, mimi si mtu muhimu; je nawezaje kukujibu? Ninauweka mkono wangu juu ya mdomo wangu.
Why do I yet plead? being rebuked even while reproving the Lord: hearing such things, whereas I am nothing: and what shall I answer to these [arguments]? I will lay my hand upon my mouth.
5 Ninazungumza mara moja, na sitakujibu; hakika, mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.”
I have spoken once; but I will not do so a second time.
6 Kisha Yahweh akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kusema,
And the Lord yet again answered and spoke to Job out of the cloud, [saying],
7 “Jifunge sasa mkanda kiunoni mwako kama mwanaume, kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
Nay, gird up now your loins like a man; and I will ask you, and do you answer me.
8 Je waweza kusema kwa hakika kwamba mimi si mwenye haki? Je utanihukumu mimi ili useme wewe ni mwenye haki?
Do not set aside my judgement: and do you think that I have dealt with you in any other way, than that you might appear to be righteous?
9 Je una mkono kama wa Mungu? Je waweza kutoa kishindo kwa sauti kama yeye?
Hast you an arm like the Lord's? or do you thunder with a voice like his?
10 Jivike sasa katika utukufu na katika utu; jivalie mwenyewe heshima na enzi.
Assume now a lofty bearing and power; and clothe yourself with glory and honour.
11 Sambaza ziada ya hasira yako; mtazame kila mmoja mwenye kiburi na umshushe chini.
And send forth messengers with wrath; and lay low every haughty one.
12 Mwangalie kila mmoja mwenye kiburi na umweke chini; wakanyage chini watu waovu mahali wanaposimama.
Bring down also the proud man; and consume at once the ungodly.
13 Wazike ardhini pamoja; zifunge nyuso zao katika sehemu zilizositirika.
And hide them together in the earth; and fill their faces with shame.
14 Ndipo pia nitakapokubali ya kwamba mkono wako wa kulia waweza kukuokoa.
[Then] will I confess that your right hand can save [you].
15 Mwangalie sasa kiboko, ambaye niliwafanya kama nilivyokufanya wewe; anakula nyasi kama ng'ombe.
But now look at the wild beasts with you; they eat grass like oxen.
16 Ona sasa, nguvu zake ziko katika viuno vyake; nguvu zake zi katika mishipa ya tumbo lake.
Behold now, his strength is in his loins, and his force is in the navel of his belly.
17 Yeye huuondoa mkia wake kama mti wa mwerezi; mishipa ya paja lake imeunganishwa pamoja.
He sets up his tail like a cypress; and his nerves are wrapped together.
18 Mifupa yake ni kama ya mirija ya shaba; na miguu yake ni kama kipande cha chuma.
His sides are sides of brass; and his backbone is [as] cast iron.
19 Yeye ni mkuu wa viumbe vya Mungu. Ni Mungu pekee, ambaye alimwumba, anaweza kumshinda.
This is the chief of the creation of the Lord; made to be played with by his angels.
20 Kwa kuwa milima humpatia chakula; hayawani wa mashambani hucheza karibu.
And when he has gone up to a steep mountain, he causes joy to the quadrupeds in the deep.
21 Hujilaza chini ya mimiea ya kivuli katika makao ya mianzi, na katika bwawa la matope.
He lies under trees of every kind, by the papyrus, and reed, and bulrush.
22 Miti yenye vivuli humfunika katika vivuli vyake; mierebi ya kijito inamzunguka pande zote.
And the great trees make a shadow over him with their branches, and [so do] the bushes of the field.
23 Tazama, kama mto utazigharikisha kingo zake, hatikisiki; yeye anajiamini, hata kama Mto wa Yordani unajaa hadi katika pua yake.
If there should be a flood, he will not perceive it; he trust that Jordan will rush up into his mouth.
24 Je mtu yeyote aweza kumnasa kwa ndoano, au kuichoma pua yake kwa mtego?
[Yet one] shall take him in his sight; [one] shall catch [him] with a cord, and pierce his nose.

< Ayubu 40 >