< Ayubu 40 >

1 Yahweh aliendelea kuongea na Ayubu na kusema,
Moreover the LORD answered Job, and said:
2 “Je mtu yeyote anayetaka kukosoa na ajaribu kumsahihisha Mwenye enzi? Na yeye anayehojiana na Mungu, na ajibu yeye.”
Shall he that reproveth contend with the Almighty? He that argueth with God, let him answer it.
3 Ndipo Ayubu akamjibu Yahweh na kusema, “
Then Job answered the LORD, and said:
4 Tazama, mimi si mtu muhimu; je nawezaje kukujibu? Ninauweka mkono wangu juu ya mdomo wangu.
Behold, I am of small account; what shall I answer Thee? I lay my hand upon my mouth.
5 Ninazungumza mara moja, na sitakujibu; hakika, mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.”
Once have I spoken, but I will not answer again; yea, twice, but I will proceed no further.
6 Kisha Yahweh akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kusema,
Then the LORD answered Job out of the whirlwind, and said:
7 “Jifunge sasa mkanda kiunoni mwako kama mwanaume, kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
Gird up thy loins now like a man; I will demand of thee, and declare thou unto Me.
8 Je waweza kusema kwa hakika kwamba mimi si mwenye haki? Je utanihukumu mimi ili useme wewe ni mwenye haki?
Wilt thou even make void My judgment? Wilt thou condemn Me, that thou mayest be justified?
9 Je una mkono kama wa Mungu? Je waweza kutoa kishindo kwa sauti kama yeye?
Or hast thou an arm like God? And canst thou thunder with a voice like Him?
10 Jivike sasa katika utukufu na katika utu; jivalie mwenyewe heshima na enzi.
Deck thyself now with majesty and excellency, and array thyself with glory and beauty.
11 Sambaza ziada ya hasira yako; mtazame kila mmoja mwenye kiburi na umshushe chini.
Cast abroad the rage of thy wrath; and look upon every one that is proud, and abase him.
12 Mwangalie kila mmoja mwenye kiburi na umweke chini; wakanyage chini watu waovu mahali wanaposimama.
Look on every one that is proud, and bring him low; and tread down the wicked in their place.
13 Wazike ardhini pamoja; zifunge nyuso zao katika sehemu zilizositirika.
Hide them in the dust together; bind their faces in the hidden place.
14 Ndipo pia nitakapokubali ya kwamba mkono wako wa kulia waweza kukuokoa.
Then will I also confess unto thee that thine own right hand can save thee.
15 Mwangalie sasa kiboko, ambaye niliwafanya kama nilivyokufanya wewe; anakula nyasi kama ng'ombe.
Behold now behemoth, which I made with thee; he eateth grass as an ox.
16 Ona sasa, nguvu zake ziko katika viuno vyake; nguvu zake zi katika mishipa ya tumbo lake.
Lo now, his strength is in his loins, and his force is in the stays of his body.
17 Yeye huuondoa mkia wake kama mti wa mwerezi; mishipa ya paja lake imeunganishwa pamoja.
He straineth his tail like a cedar; the sinews of his thighs are knit together.
18 Mifupa yake ni kama ya mirija ya shaba; na miguu yake ni kama kipande cha chuma.
His bones are as pipes of brass; his gristles are like bars of iron.
19 Yeye ni mkuu wa viumbe vya Mungu. Ni Mungu pekee, ambaye alimwumba, anaweza kumshinda.
He is the beginning of the ways of God; He only that made him can make His sword to approach unto him.
20 Kwa kuwa milima humpatia chakula; hayawani wa mashambani hucheza karibu.
Surely the mountains bring him forth food, and all the beasts of the field play there.
21 Hujilaza chini ya mimiea ya kivuli katika makao ya mianzi, na katika bwawa la matope.
He lieth under the lotus-trees, in the covert of the reed, and fens.
22 Miti yenye vivuli humfunika katika vivuli vyake; mierebi ya kijito inamzunguka pande zote.
The lotus-trees cover him with their shadow; the willows of the brook compass him about.
23 Tazama, kama mto utazigharikisha kingo zake, hatikisiki; yeye anajiamini, hata kama Mto wa Yordani unajaa hadi katika pua yake.
Behold, if a river overflow, he trembleth not; he is confident, though the Jordan rush forth to his mouth.
24 Je mtu yeyote aweza kumnasa kwa ndoano, au kuichoma pua yake kwa mtego?
Shall any take him by his eyes, or pierce through his nose with a snare?

< Ayubu 40 >