< Zaburi 2 >

1 Kwa nini mataifa wanafanya dhoruba, kwa nini watu wanafanya njama ambazo zitafeli?
Why are the nations in an uproar? And why do the peoples mutter in vain?
2 Wafalme wa nchi kwa pamoja hushikilia misimamo yao na watawala kwa pamoja hufanya njama kinyume na Yahwe na kinyume na Masihi, wakisema,
The kings of the earth stand up, and the rulers take counsel together, against the LORD, and against His anointed:
3 “Ngoja tuzikate pingu walizo tufingia sisi na kuzitupa pingu zao.”
'Let us break their bands asunder, and cast away their cords from us.'
4 Yeye aketie katika mbingu atacheka kwa dharau mbele yao; Bwana atawadhihaki wao.
He that sitteth in heaven laugheth, the Lord hath them in derision.
5 Kisha ataongea nao katika hasira yake na kuwaogofya kwa gadhabu yake, akisema,
Then will He speak unto them in His wrath, and affright them in His sore displeasure:
6 “Mimi mwenyewe nilimpaka mafuta mfalme wa Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
'Truly it is I that have established My king upon Zion, My holy mountain.'
7 Nami nitatangaza amri ya Yahwe. Yeye aliniambia, “wewe ni mwanangu! Leo hii nimekuwa baba yako.
I will tell of the decree: the LORD said unto me: 'Thou art My son, this day have I begotten thee.
8 Uniombe, nami nitakupa wewe taifa kwa ajili ya urithi na mikoa ya nchi iliyo bora kwa ajili ya umiliki wako.
Ask of Me, and I will give the nations for thine inheritance, and the ends of the earth for thy possession.
9 Wewe utawavunja wao kwa fimbo ya chuma; kama vile mtungi wa mfinyanzi, wewe utawavunja wao vipande vipande.”
Thou shalt break them with a rod of iron; thou shalt dash them in pieces like a potter's vessel.'
10 Hivyo sasa, ninyi wafalme; mchukue tahadhari; mjirekebishe.
Now therefore, O ye kings, be wise; be admonished, ye judges of the earth.
11 Mwabuduni Yahwe kwa hofu na mfurahi mkitetemeka.
Serve the LORD with fear, and rejoice with trembling.
12 Mumbusu mwana vinginevyo atawakasirikia, na mtakufa pale pale hasira yake ikiwaka. Ni jinsi gani wamebarikiwa wale wote watafutao usalama ndani yake.
Do homage in purity, lest He be angry, and ye perish in the way, when suddenly His wrath is kindled. Happy are all they that take refuge in Him.

< Zaburi 2 >