< Ayubu 33 >

1 Kwahiyo sasa, nakuomba wewe, Ayubu, usikilize hotuba yangu; sikiliza maneno yangu yote.
Sin embargo, Job, escucha ahora mis razones y atiende todas mis palabras.
2 Tazama sasa, nimeufumbua mdomo wangu; ulimi wangu umesema maneno ndani ya mdomo wangu.
Ciertamente ahora abro mi boca. Mi lengua habla en mi paladar.
3 Maneno yangu yatasema uadilifu wa moyo wangu; yatasema kwa unyofu yale ambayo mdomo wangu unayajua.
Mis palabras declararán la rectitud de mi corazón y lo que saben mis labios lo dicen con sinceridad:
4 Roho ya Mungu imeniumba; pumzi ya Mwenye nguvu imenipatia uhai.
El Espíritu de ʼElohim me hizo y el soplo de ʼEL-Shadday me dio vida.
5 Kama unaweza, nijibu; weka maneno yako katika mpangilio mbele yangu na kisha usimame.
Respóndeme si puedes. Alístate y ponte en pie ante mí.
6 Tazama, niko kama wewe ulivyo mbele za Mungu; nimeumbwa pia kutoka katika udongo.
Ciertamente pertenezco a ʼEL, como tú. Del barro también fui formado.
7 Ona, tishio langu halitakufanya wewe uogope; wala mzigo wangu hautakuwa mzito kwako.
Ciertamente mi terror no te espantará, ni mi mano será demasiado pesada sobre ti.
8 Umesema kwa hakika katika masikio yangu; nimeisikia sauti ya maneno yakeo yakisema,
En verdad tú dijiste a oídos míos. Yo oí el sonido de tus palabras:
9 'Mimi ni safi na bila hila; sina hatia, na hakuna dhambi ndani yangu.
Limpio soy, sin transgresión. Soy inocente y no hay culpa en mí.
10 Tazama, Mungu huona nafasi za kunishambulia mimi; huniangalia mimi kama adui yake.
Ciertamente Él inventa pretextos contra mí y me considera su enemigo.
11 Huweka miguu yangu akiba; naye huangalia njia zangu zote.'
Puso mis pies en el cepo y vigila todos mis pasos.
12 Tazama, katika hili hauko sawa, nitakujibu, kwa kuwa Mungu ni mkuu kuliko mtu.
Ciertamente yo te respondo: En esto no eres justo, porque ʼElohim es mayor que el hombre.
13 Kwanini unashindana naye? Huwa hahesabu matendo yake yoyote.
¿Por qué contiendes con ʼEL? Pues Él no da cuenta de ninguna de sus obras.
14 Kwa kuwa Mungu huzungumza mara moja, naam, mara mbili, ingawa mwanadamu hawezi kutambua.
Porque ʼElohim habla de una manera o de otra, pero nadie lo percibe:
15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito unapowapata watu, katika usingizi kitandani -
En sueño, en visión nocturna, cuando el sopor cae sobre los hombres, mientras se adormecen en la cama,
16 basi Mungu hufungua masikio ya watu, na kuwatisha kwa vitisho,
Él abre el oído de los hombres y sella su instrucción para ellos,
17 kwa kusudi la kumvuta mtu atoke katika makusudio yake maovu, na kuyaweka majivuno mbali naye.
a fin de apartar al hombre de su obra y destruir la soberbia del varón,
18 Mungu huyaokoa maisha ya mwanadamu kutoka katika shimo, na uhai wake dhidi ya kifo.
para librar su alma del sepulcro y que su vida no perezca a filo de espada.
19 Mtu huadhidibiwa pia na maumivu kitandani mwake, na maumivu makali yanayodumu katika mifupa yake,
También sobre su cama es reprendido con dolores, con el dolor incesante de sus huesos,
20 ili kwamba maisha yake yachukie chakula, na roho yake ichukie vyakula vizuri.
lo cual hace que le repugne el pan, y aun el manjar más delicado.
21 Nyama yake imeharibiwa ili kwamba usionekane; mifupa yake, mara moja isionekane, sasa basi ng'ang'ania.
Su carne se consume hasta que no se ve, y sus huesos, que no se veían, aparecen.
22 Hakika, roho yake inasogea shimoni, na uhai wake unasogea kwa wale wanaotaka kuuharibu.
Su alma se acerca al sepulcro y su vida a los que causan la muerte.
23 Lakini kama kuna malaika anayeweza kuwa mpatanishi kwa ajili yake, mpatanishi mmoja miongoni mwa maelfu ya malaika, kumwonesha kile kilicho cha haki ili atende haki,
Si hay un ángel que sea mediador para él, muy escogido entre 1.000, que recuerda al hombre lo correcto para él,
24 na kama malaika ni mpole kwake na kumwambia Mungu, 'Mwokoe mtu huyu ili asishuke chini shimoni; nimepata fidia kwa ajili yake,'
tenga compasión de él y diga: Líbrenlo de bajar al sepulcro, pues le hallé un rescate.
25 kisha mwili wake utakuwa mororo kuliko mwili wa mtoto, atazirudia siku za nguvu za ujana wake.
Entonces su carne sería más tierna que la de un joven que vuelve al vigor de los días de su juventud.
26 Atamwomba Mungu, na Mungu atakuwa mwema kwake, ili kwamba auone uso wa Mungu akiwa mwenye furaha. Mungu atampa mtu ushindi wake.
Invocaría a ʼEloha. Él le haría sacrificio que apacigua, para que vea el semblante de ʼEL con gozo y Él le restaure su justicia al hombre.
27 Ndipo mtu huyo ataimba mbele ya watu wengine na kusema, 'Nilitenda dhambi na kuasi kile kilichokuwa cha haki, lakini dhambi yangu haikuadhibiwa.
Él mira a los hombres y al que dice: Pequé y pervertí lo recto, pero nada me aprovechó,
28 Mungu ameiokoa roho yangu isiende chini shimoni; maisha yangu yataendelea kuuona mwanga.'
Él le redimirá su alma para que no baje al sepulcro, y su vida verá la luz.
29 Tazama, Mungu hufanya mambo haya yote pamoja na mwanadamu, mara mbili, naam, hata mara tatu,
En verdad ʼEL hace todas estas cosas con el hombre dos veces, y aun tres,
30 kuirudisha roho yake kutoka shimoni, ili kwamba aweze kumlikwa na mwanga wa maisha.
para rescatar su alma del sepulcro e iluminarlo con la luz de la vida.
31 Ayubu, zingatia na unisikilize mimi; nyamaza nami nitasema.
Presta atención, Job, escúchame. Calla, y permíteme hablar.
32 Ikiwa una kitu cha kusema, na unijibu; sema, maana nataka kuhakikisha kwamba wewe uko katika haki.
Si tienes palabras, respóndeme. Habla, porque yo quiero declararte justo.
33 Kama sivyo, basi nisikilize, ubaki kimya, nami nitakufundisha wewe hekima.”
Si no, escúchame. Calla, y yo te enseñaré sabiduría.

< Ayubu 33 >