< Ayubu 32 >

1 Hivyo hawa watu watatu walikoma kumjibu Ayubu kwasababu alikuwa ni mwenye haki katika macho yake mwenyewe.
Aquellos tres hombres cesaron de replicar a Job, porque él era justo ante sus propios ojos.
2 Ndipo iliwaka hasira ya Elihu mwana wa Barakeli Mbuzi, wa familia ya Ramu, iliwaka dhidi ya Ayubu kwa kuwa alijihesabia haki mwenyewe kuliko Mungu.
Entonces Eliú, hijo de Baraquel, buzita, de la familia de Ram, se encendió en ira contra Job, porque él se justificaba a sí mismo delante de ʼElohim.
3 Hasira ya Elihu iliwaka pia kinyume cha marafiki zake watatu kwasababu hawakupata jibu kwa ajili ya Ayubu, na bado walimhukumu Ayubu.
También se enardeció contra sus tres amigos, porque no hallaron respuesta, sin embargo condenaron a Job.
4 Sasa Elihu alikuwa amemsubiri Ayubu ili aweze kuzungumza naye kwa kuwa watu wengine walikuwa wakubwa kuliko yeye.
Eliú esperó en la disputa con Job, porque ellos eran mayores que él.
5 Hata hivyo, wakati Elihu alipoona ya kuwa hapakuwa na jibu katika midomo ya watu hawa watatu, hasira yake iliwaka.
Pero al ver Eliú que no había respuesta en la boca de aquellos tres hombres, se encendió en ira.
6 Ndipo Elihu mwana wa Barakeli Mbuzi alinena na kusema, “Mimi ni mdogo, na ninyi ni wazee. Hii ndio sababu nilijizuia na sikuthubutu kuzungumza mawazo yangu mwenyewe.
Eliú tomó la palabra, hijo de Baraquel, buzita: Yo soy menor y ustedes son ancianos. Por eso me abstuve y temí declararles mi opinión.
7 Nilisema, “Urefu wa siku utazungumza; na wingi wa miaka utatufundisha hekima.
Yo pensé: La edad debe hablar. El número de años debe enseñar sabiduría.
8 Lakini kuna roho ndani ya mtu; pumzi ya Mwenye nguvu humpa yeye ufahamu.
Pero el que le da entendimiento es el espíritu en el hombre, el soplo del ʼEL-Shadday.
9 Si tu watu wakubwa ndio wenye hekima, wala watu wazee pekee ambao hufahamu haki.
No son sabios los de mucha edad, ni los ancianos entienden justicia.
10 Hivyo basi nakwambia wewe, “Nisikilizeni mimi; Nitakwambia pia uelewa wangu.'
Por eso digo: ¡Escúchenme! También yo declararé lo que pienso.
11 Tazama, niliyasubiria maneno yenu; nilisikiliza hoja zenu wakati mlipokuwa mnafikiri juu ya kile cha kusema.
Ciertamente esperé sus palabras, escuché sus razones mientras buscaban qué decir.
12 Hakika, niliwajali sana ninyi, lakini, tazama, hakuna hata mmoja wenu aliyeweza kumshawishi Ayubu wala ambaye aliweza kumjibu maneno yake.
Les presté atención. Ciertamente no hay alguno de ustedes que redarguya a Job y responda sus razonamientos.
13 Iweni waangalifu msije mkasema, 'Tumepata hekima!' Mungu atakuwa amemshinda Ayubu; mtu wa kawaida hawezi akafanya hivyo.
No digan: Hallamos la sabiduría. ʼElohim lo derrotará de manera aplastante, no el hombre.
14 Kwa kuwa Ayubu hajasema mojamoja maneno yake juu yangu, basi sitamjibu kwa maneno yenu.
Él no dirigió sus palabras contra mí, ni yo le responderé con las palabras de ustedes.
15 Hawa watu watatu wamep igwa bumbuwazi; hawawezi kuendelea kumjibu Ayubu; hawana neno zaidi la kusema.
Se desconcertaron, ya no responden. Sus palabras los abandonaron.
16 Je ninapaswa kusubiria kwasababu hawazungumzi, kwa kuwa wamesimama pale kimya na wala hawajibu zaidi?
¿Debo esperar porque no hablan, porque cesaron y ya no responden?
17 La, nitajibu pia upande wangu; Nitawaambia pia ufahamu wangu.
Yo también responderé mi parte. Yo también expresaré mi opinión,
18 Kwa kuwa nimejawa na maneno mengi, roho ndani yangu inanisukuma.
porque estoy lleno de palabras, y el espíritu me obliga dentro de mí.
19 Tazama, kifua changu ni kama divai yenye chachu ambayo haina tundu; kama viriba vipya, kiko tayari kupasuka.
Ciertamente mis órganos internos son como vino sin respiradero y están a punto de reventar como odres nuevos.
20 Nitazungumza ili kwamba niweze kuburudishwa; nitafungua kimya changu na kusema.
Hablaré y me desahogaré. Abriré mi boca y responderé.
21 Sitaonesha upendeleo; wala sitatoa sifa za majina kwa mtu yeyote.
No haré ahora acepción de personas, ni me permitiré adular a algún hombre,
22 Kwa kuwa sijui namna ya kutoa sifa; kama nitafanya hivyo, Muumba wangu atanikatilia mimi mbali.
porque nunca supe adular. De otra manera, mi Hacedor pronto me consumiría.

< Ayubu 32 >