< Ayubu 3 >

1 Baada ya hayo, Ayubu akafunua kinywa chake na kuilani siku aliyozaliwa.
After this opened Job his mouth, and cursed his day.
2 Akasema,
And Job spoke, and said:
3 “Na ipotelee mbali siku niliyozaliwa mimi, usiku uliosema, 'Mimba ya mtoto wa kiume imetungwa.'
Let the day perish wherein I was born, and the night wherein it was said: 'A man-child is brought forth.'
4 Siku hiyo na iwe giza; Mungu toka juu asiifikilie, wala mwanga usiiangazie.
Let that day be darkness; let not God inquire after it from above, neither let the light shine upon it.
5 Ishikwe na giza na giza la mauti liwe lake. Wingu na likae juu yake; kila kitu kiifanyacho siku kuwa giza kweli na kiitishe.
Let darkness and the shadow of death claim it for their own; let a cloud dwell upon it; let all that maketh black the day terrify it.
6 Usiku huo, na ukamatwe na giza tororo. Usihesabiwe miongoni mwa siku za mwaka; na usiwekwe katika hesabu ya miezi.
As for that night, let thick darkness seize upon it; let it not rejoice among the days of the year; let it not come into the number of the months.
7 Tazama, usiku huo na uwe tasa; na sauti ya shangwe isiwe ndani yake.
Lo, let that night be desolate; let no joyful voice come therein.
8 Na wailani siku hiyo, hao wafahamuo namna ya kumuamsha lewiathani.
Let them curse it that curse the day, who are ready to rouse up leviathan.
9 Nyota za mapambazuko yake zitiwe giza. Siku hiyo iutafute mwanga, lakini isiupate; wala makope ya mapambazuko isiyaone,
Let the stars of the twilight thereof be dark; let it look for light, but have none; neither let it behold the eyelids of the morning;
10 kwasababu haikuifunga milango ya tumbo la mama yangu, na kwasababu haikunifichia taabu machoni pangu.
Because it shut not up the doors of my mother's womb, nor hid trouble from mine eyes.
11 Kwanini si-kufa wakati lipotokeza katika tumbo la uzazi? Kwanini sikuitoa roho yangu hapo mama aliponizaa?
Why died I not from the womb? Why did I not perish at birth?
12 kwanini magoti yake yalinipokea? Kwanini maziwa yake yanipokee hata ninyonye?
Why did the knees receive me? And wherefore the breasts, that I should suck?
13 Kwa sasa ningelikuwa nimelala chini kimya kimya. Ningelala usingizi na kupata pumziko
For now should I have lain still and been quiet; I should have slept; then had I been at rest —
14 pamoja na wafalme na washauri wa dunia, ambao walijijengea makaburi ambayo sasa ni magofu.
With kings and counsellors of the earth, who built up waste places for themselves;
15 Au Ningelikuwa nimelala pamoja na wakuu wenye dhahabu, waliozijaza nyumba zao fedha.
Or with princes that had gold, who filled their houses with silver;
16 Au pengine ningekuwa sijazaliwa, kama watoto wachanga wasio uona mwanga kabisa.
Or as a hidden untimely birth I had not been; as infants that never saw light.
17 Huko waovu huacha kusumbua; huko waliochoka hupumzika.
There the wicked cease from troubling; and there the weary are at rest.
18 Huko wafungwa kwa pamoja hupata amani; hawaisikii sauti ya msimamizi wa watumwa.
There the prisoners are at ease together; they hear not the voice of the taskmaster.
19 Wote wadogo na watu maarufu wako huko; mtumishi yuko huru kwa bwana wake huko.
The small and great are there alike; and the servant is free from his master.
20 Kwa nini yeye aliye mashakani kupewa mwanga? Kwa nini hao wenye uchungu moyoni kupewa uhai,
Wherewith is light given to him that is in misery, and life unto the bitter in soul —
21 ambao hutamani mauti lakini hawapati; ambao huyachimbulia mauti zaidi ya kutafuta hazina iliyofichika?
Who long for death, but it cometh not; and dig for it more than for hid treasures;
22 Kwa nini kupewa mwanga ambao hushangilia mno na kufurahi walionapo kaburi?
Who rejoice unto exultation, and are glad, when they can find the grave? —
23 Kwanini kupewa mwanga mtu ambaye njia zake zimefichika, mtu ambaye Mungu amemzungushia uwa?
To a man whose way is hid, and whom God hath hedged in?
24 Kwa kuwa kushusha kwangu pumzi kwatokea badala ya kula; kuugua kwangu kumemiminika kama maji.
For my sighing cometh instead of my food, and my roarings are poured out like water.
25 Maana jambo lile niliogopalo limenipata; nalo linitialo hofu limenijilia.
For the thing which I did fear is come upon me, and that which I was afraid of hath overtaken me.
26 Mimi sioni raha, sipati utulivu, na sipati pumziko; badala yake huja taabu.”
I was not at ease, neither was I quiet, neither had I rest; but trouble came.

< Ayubu 3 >