< Ayubu 16 >

1 Ndipo Ayubu akajibu na kusema,
Tad Ījabs atbildēja un sacīja:
2 “Mimi nimevisikia vitu hivyo vingi; ninyi nyote ni wafariji wenye kuhuzunisha.
Tādas lietas nu papilnam esmu dzirdējis, jūs visi esat nelāga iepriecinātāji.
3 Maneno yenye upuuzi daima yanaweza kuwa na mwisho? Nini kimeharibika kwenu kwamba mnajibu kama hivi?
Vai tie uzpūstie vārdi nu būs galā, vai kas tevi dzen tā atbildēt?
4 Mimi pia ningeweza kuzungumza kama ninyi mnavyofanya, kama ninyi mngekuwa katika nafasi yangu; Mimi ningekusanya na kuunganisha maneno pamoja dhidi yenu na kutikisa kichwa changu kwenu ninyi katika dhihaka.
Es gan tāpat runātu kā jūs, kad jūsu dvēsele būtu manā vietā, ar vārdiem es pret jums turētos un kratītu savu galvu pār jums.
5 Laiti, jinsi gani Mimi ningewatia moyo na midomo yangu! Jinsi gani faraja kutoka midomo yangu ingenga'risha huzuni yenu!
Es jūs stiprinātu ar savu muti, jūs iepriecinātu ar savām lūpām.
6 Ikiwa Mimi ninazungumza, kuomboleza kwangu hakujasikilizwa; Ikiwa nikiendelea katika kuzungumza, jinsi gani mimi ninaidiwa?
Kad es runāju, tad manas sāpes nerimst, un kad es klusu ciešu, vai tad tās nostājās?
7 Lakini sasa, Mungu,
Tiešām, nu Viņš mani nokausējis; Tu esi izklīdinājis visu manu saimi,
8 wewe umenifanya mimi kuchoka; wewe umeifanya familia yangu yote kuwa ukiwa. Wewe umenifanya mimi kukauka, ambayo yenyewe ni ushuhuda dhidi yangu mimi; kukonda kwa mwili wangu huinuka dhidi yangu, na kunashuhudia dhidi ya macho yangu.
Un mani darījis grumbainu, - tas ir par liecību, un mana liecība cēlās pret mani un mani apsūdzēja pašā vaigā.
9 Mungu amenirarua mimi katika ghadhabu yake na amenitesa mimi; Yeye amenisaga mimi kwa meno yake; Adui yangu amenikazia macho yake juu yangu kama yeye anavyonirarua mimi vipande.
Viņa bardzība mani saplosīja un vajāja, Viņš sakož Savus zobus par mani, mans pretinieks met briesmīgas acis uz mani.
10 Watu wameachama na midomo iliyowazi juu yangu; wamenipiga mimi katika shavu kwa kunitukana; wamekusanyika pamoja kinyume changu mimi.
Tie atplēš muti pret mani, un lādot tie mani sit vaigā, tie sapulcējās kopā pret mani.
11 Mungu amenikabidhi mimi juu ya watu wasio mcha Mungu, na kunitupa mimi ndani ya mikono ya watu waovu.
Dievs mani nodevis neliešiem un man licis nākt bezdievīgu rokā.
12 Mimi nilikuwa katika wepesi, na yeye amenivunjavunja mimi vipande. Hakika, amenichukua mimi kwa shingo na ameniponda mimi vipande vipande; yeye pia ameniweka mimi juu kama shabaha yake.
Es biju mierā, bet Viņš mani sadauzījis, Viņš mani grābis pie kakla un mani satriecis un mani licis Sev par mērķi.
13 Wapiga upinde wake wote wamenizunguka mimi; Mungu huzikata vipande vipande figo zangu, na haniokoi mimi; yeye humwaga nje nyongo yangu juu ya ardhi.
Viņa bultas ap mani skraida, Viņš sašķēlis manas īkstis un nav taupījis, Viņš manu žulti izlējis zemē.
14 yeye hukanyaga kanyaga kupitia ukuta wangu tena na tena; yeye hukimbia juu yangu mimi kama shujaa.
Plosīdams Viņš mani plosot plosījis, Viņš kā pats varenais pret mani lauzies.
15 nguo ya magunia juu ya ngozi yangu; Mimi nimeisukuma kwa nguvu pembe yangu ndani ya ardhi.
Es maisu esmu šuvis ap savu ādu un savu ragu licis pīšļos,
16 Uso wangu ni mwekundu na kuomboleza; juu ya ngozi inayofunika macho kuna kivuli cha mauti
Mans vaigs ir nosarcis no raudām, un pār maniem acu vākiem ir nāves ēna,
17 ingawa hakuna dhuluma katika mikono yangu, na kuomba kwangu ni safi.
Jebšu netaisnība nav manā rokā, un mana lūgšana ir šķīsta.
18 Nchi, haifuniki juu damu yangu mimi; acha kulia kwangu kuwe hakuna mahali pa kupumzika.
Zeme, neapklāj manas asinis, un mana saukšana lai nemitās!
19 Hata sasa, tazama, ushuhuda wangu uko mbinguni; yeye ambaye ashuhudiaye kwa ajili yangu mimi yuko juu.
Jau tagad, redzi, mans liecinieks ir debesīs, un mans liecības devējs debess augstībā.
20 Rafiki zangu wananicheka kwa dharau, lakini jicho langu linamwaga machozi kwa Mungu.
Mani draugi ir mani mēdītāji, bet no manas acs asaras pil uz Dievu,
21 Mimi ninaomba ule ushuhuda ulioko mbinguni kumtetea mtu huyu na Mungu kama mwanadamu afanyavyo na jirani yake.
Kaut Viņš tiesu nestu starp vīru un Dievu un starp cilvēka bērnu un viņa draugu!
22 Kwa maana wakati miaka michache itakapokuwa imepita, Mimi nitakwenda mahali ambapo mimi sitaweza kurudi.
Jo tie noliktie gadi ies galā, un es aiziešu ceļu, kur atpakaļ negriezīšos.

< Ayubu 16 >