< Yeremia 5 >

1 Kimbieni mkapite katika mitaa ya Yerusalemu, Tafuteni katika viwanja vyake. Kama mtaweza kumpata hata mtu mmoja anayetenda kwa haki na kufanya kwa uaminifu, basi nitaisamehe Yerusalemu.
Run ye to and fro through the streets of Jerusalem, and see now, and know, and seek in the broad places thereof, if ye can find a man, if there be any that doeth justly, that seeketh truth; and I will pardon her.
2 Hata kama wanasema, 'Kama BWANA aishivyo,' wanaapa uongo.”
And though they say: 'As the LORD liveth', surely they swear falsely.
3 BWANA, macho yako hayatazami uaminifu? Unawapiga watu, lakini hawasikii maumivu. Umewaangsmiza kabisa, lakini bado wanakataa kuwa waadilifu. Wanafanya nyuso zao kuwa ngumu kama mwamba. kwa kuwa wanakataa kutubu.
O LORD, are not Thine eyes upon truth? Thou hast stricken them, but they were not affected; Thou hast consumed them, but they have refused to receive correction; they have made their faces harder than a rock; they have refused to return.
4 Kwa hiyo nilisema, “Hakika hawa ni watu masikini, Ni wapumbavu, Kwa kuwa hawazijui njia za BWANA, wala maagizo ya Mungu wao.
And I said: 'Surely these are poor, they are foolish, for they know not the way of the LORD, nor the ordinance of their God;
5 Nitaenda kwa watu wa muhimu na kutangaza ujumbe wa Mungu kwao, kwa kuwa angalau wanazijua njia za BWANA, maagizo ya Mungu wao. Lakini wote wanavunja nira yao pamoja; wote wanaivunja ile minyororo inayowafunga kwa ajili ya Mungu.
I will get me unto the great men, and will speak unto them; for they know the way of the LORD, and the ordinance of their God.' But these had altogether broken the yoke, and burst the bands.
6 Kwa hiyo simba kutoka mwituni atawavamia. Mbweha kutoka Arabaha atawaangamiza. Chui ataivunja miji yao. Mtu yeyota anayeenda nje ya mji wake atavunjwavunjwa. Kwa kuwa maovu yao yameongezeka. Matendo yao ya uasi hayana ukomo.
Wherefore a lion out of the forest doth slay them, a wolf of the deserts doth spoil them, a leopard watcheth over their cities, every one that goeth out thence is torn in pieces; because their transgressions are many, their backslidings are increased.
7 Kwa nini niwasamehe hawa watu? Wana wenu wameniacha na wamefanya viapo na wale ambao si miungu. Niliwalisha vya kutosha, lakini wamefanya uasherati na kuchukua alama za nyumba ya uzinzi.
Wherefore should I pardon thee? The children have forsaken Me, and sworn by no-gods; and when I had fed them to the full, they committed adultery, and assembled themselves in troops at the harlots' houses.
8 Walikuwa farasi wanaotafuta kupandwa. Walitembea huku na huku wakitafutwa kupandwa. Kila mwanamume alimkaribia mke wa jirani yake.
They are become as well-fed horses, lusty stallions; every one neigheth after his neighbour's wife.
9 Kwa hiyo kwa nini nisiwaadhibu - asema BWANA - na kwa nini nisijilipizie kisasi juu ya taifa kama hili?
Shall I not punish for these things? saith the LORD; and shall not My soul be avenged on such a nation as this?
10 Nenda hadi kwenye kuta za shamba lake la mizabibu na zihariibuni. Lakini wao msiwaharibu kabisa. Ondoeni matawi kwa sababu hayatoki kwa BWANA.
Go ye up into her rows, and destroy, but make not a full end; take away her shoots; for they are not the LORD'S.
11 Kwa sababu nyumba ya Yuda na Israeli wamenisaliti kabisa - asema BWANA -
For the house of Israel and the house of Judah have dealt very treacherously against Me, saith the LORD.
12 na wamenikataa. Wanasema, ''Yeye si halisi. Maovu hayawezi kutupata, wala hatutaona upanga wala njaa.
They have belied the LORD, and said: 'It is not He, neither shall evil come upon us; neither shall we see sword nor famine;
13 Kwa kuwa manabii wamekuwa si kitu kama upepo na hakuna mtu mwiingine wa kunena ujumbe wa BWANA kwetu. Vitisho vyao na viwjie wao wenyewe.”'
And the prophets shall become wind, and the word is not in them; thus be it done unto them.'
14 Kwa hiyo BWANA, Mungu wa majeshi asema hivi, tazama nataka kuweka maneno yangu katika kinywa chako. Yatakuwa kama moto na watu hawa watakuwa kama kuni! Kwa kuwa utawaramba.
Wherefore thus saith the LORD, the God of hosts: Because ye speak this word, behold, I will make My words in thy mouth fire, and this people wood, and it shall devour them.
15 Tazama nataka kuleta taifa dhidi yenu kutoka mbali, enyi nyumba ya Israeli - asema BWANA - ni taifa linalodumu, taifa la kale! Ni taifa ambalo lugha yake hamuijui, wala hamtaelewa wasemacho.
Lo, I will bring a nation upon you from far, O house of Israel, saith the LORD; it is an enduring nation, it is an ancient nation, a nation whose language thou knowest not, neither understandest what they say.
16 Podo lao ni kaburi wazi. Wote ni wanajeshi.
Their quiver is an open sepulchre, they are all mighty men.
17 Kwa hiyo mavuno yako yataliwa, wana wako na binti zako pia, na chakula chako. Watakula kondoo wako na ng'ombe wako, watakula matunda ya zabibu zako na ya mitiini. Wataiangusha chini miji yenu na boma zake ambazo mnazitumainia.
And they shall eat up thy harvest, and thy bread, they shall eat up thy sons and thy daughters, they shall eat up thy flocks and thy herds, they shall eat up thy vines and thy fig-trees; they shall batter thy fortified cities, wherein thou trusteth, with the sword.
18 Lakini hata katika siku hizo - asema BWANA - sikusudii kuwaharibu kabisa.
But even in those days, saith the LORD, I will not make a full end with you.
19 Itatokea kwenu, ninyi Yuda na Israeli, mkisema, 'Kwa nini BWANA, Mungu wetu ametufanyia haya yote?' kwamba wewe Yeremia, utawaambia, 'Kama vile mlivyomwacha BWANA na kuabudu miungu mingine katika nchi yenu, vivyo hivyo mtawatumikia wageni katika nchi ambayo si yenu.'
And it shall come to pass, when ye shall say: 'Wherefore hath the LORD our God done all these things unto us?' then shalt Thou say unto them: 'Like as ye have forsaken Me, and served strange gods in your land, so shall ye serve strangers in a land that is not yours.'
20 Waambia haya watu wa nyumba ya Yakobo na yasikike katika Yuda. Waambie,
Declare ye this in the house of Jacob, and announce it in Judah, saying:
21 'Sikilizeni hili, eny watu wapumbavu! Sanamu hazina matakwa; zina masikio lakini haziwawezi kusikia.
Hear now this, O foolish people, and without understanding, that have eyes, and see not, that have ears, and hear not:
22 Je, hamnihofu mimi - asema BWANA - au kutetemeka mbele ya uso wangu? Nimeweka mpaka wa mchanga kwenye bahari, ambao ni agizo la kudumu ambalo halibomoki - hata kama bahari ina kupwa na kujaa, bado hauwenzi kubomoka. Hata kama mawimbi yake yanaunguruma, hayawezi kuvuka.
Fear ye not Me? saith the LORD; Will ye not tremble at My presence? Who have placed the sand for the bound of the sea, an everlasting ordinance, which it cannot pass; and though the waves thereof toss themselves, yet can they not prevail; though they roar, yet can they not pass over it.
23 Lakini hawa watu wana mioyo ya usumbufu. Hugeuka kuwa wapinzani na kuondoka.
But this people hath a revolting and a rebellious heart; they are revolted, and gone.
24 Kwa kuwa hawasemi mioyoni mwao, “basi na tumche BWANA, Mungu wetu, yeye aletaye mvua za awali na mvua za vuli - kwa wakati wake, ambaye hutuzna majuma ya mavuno kwa ajili yetu.”
Neither say they in their heart: 'Let us now fear the LORD our God, that giveth the former rain, and the latter in due season; that keepeth for us the appointed weeks of the harvest.'
25 uovu wako umezuia haya yasitokee. Dhambi zako zimeyazuia mambo mema yasitokee.
Your iniquities have turned away these things, and your sins have withholden good from you.
26 Kwa watu waovu wamo kati ya watu wangu. Wanatazama kama mtu anayenyatia ili kukamata ndege; wanaweka mitego na kukamata watu;
For among My people are found wicked men; they pry, as fowlers lie in wait; they set a trap, they catch men.
27 Kama tundu la mtego lijaavyo ndege, nyumba zao zimejaa uongo. Kwa hiyo wanakua na kutajirika.
As a cage is full of birds, so are their houses full of deceit; therefore they are become great, and waxen rich;
28 Wamenenepa; wanang'aa na kupendeza. Wamepitiliza hata mipika ya maovu. Wala hawajali sababu ya kuwepo kwa watu na wala uwepo wa yatima. Wanafanikiwa hata kama hawatoi hukumu ya haki kwa yatima.
They are waxen fat, they are become sleek; yea, they overpass in deeds of wickedness; they plead not the cause, the cause of the fatherless, that they might make it to prosper; and the right of the needy do they not judge.
29 Kwa nini nisiwadhibu kwa sababu ya haya - asema BWANA - sitajilipizia kisasi juu ya taifa la namna hii?
Shall I not punish for these things? saith the LORD; Shall not My soul be avenged on such a nation as this?
30 Jambo la ajabu na la kuchukiza limetokea katika nchi hii.
An appalling and horrible thing is come to pass in the land:
31 Mananbii wanatabiri kwa uongo, na makuhani wanatwala kwa msaada wa wa hao. Watu wangu wanapenda mambo ya hivyo, lakini mwisho kitatokea nini?
The prophets prophesy in the service of falsehood, and the priests bear rule at their beck; and My people love to have it so; What then will ye do in the end thereof?

< Yeremia 5 >