< Yeremia 2 >

1 Neno la BWANA lilinijia likisema,
And the word of the LORD came to me, saying:
2 “Nenda ukanene katika masikio ya Yerusalemu. Useme; BWANA asema hivi: Ninakumbuka agano la uaminifu la ujana wako, upendo wako wakati tulipokuwa tumechumbiana, ulipokuwa ukinihitaji kule jangwani, katika ile nchi iliyokuwa haijapandwa.
Go, and cry in the ears of Jerusalem, saying: Thus saith the LORD: I remember for thee the affection of thy youth, the love of thine espousals; how thou wentest after Me in the wilderness, in a land that was not sown.
3 Israeli alikuwa ametengwa kwa BWANA, malimbuko yake ya mavuno yake! Wote waliokula malimbuko yake walikuwa na hatia! majanga yaliwajia—asema BWANA.'”
Israel is the LORD'S hallowed portion, His first-fruits of the increase; all that devour him shall be held guilty, evil shall come upon them, saith the LORD.
4 Sikilizeni neno la BWANA, enyi nyumba ya Yakobo na kila familia katika nyumba ya Israeli.
Hear ye the word of the LORD, O house of Jacob, and all the families of the house of Israel;
5 BWANA anasema hivi, “Ni makosa gani ambayo baba zenu waliyaona kwangu, hata wakatae kunifuata mimi? hata wazifuate sanamu ambazo hazina chochote na wao kuwa si kitu?
Thus saith the LORD: What unrighteousness have your fathers found in Me, that they are gone far from Me, and have walked after things of nought, and are become nought?
6 Wala hawakusema, BWANA yuko wapi, ambaye alitutoa katika nchi ya Misri? BWANA yuko wapi, ambaye alituongoza katika jangwa, katika nchi ya Araba na mashimo, katika nchi ya ukame na giza nene, katika nchi ambayo hakuna mtu apitaye wala hakuna mtu anayeishi humo?
Neither said they: 'Where is the LORD that brought us up out of the land of Egypt; that led us through the wilderness, through a land of deserts and of pits, through a land of drought and of the shadow of death, through a land that no man passed through, and where no man dwelt?'
7 Lakini nilwaleta katika nchi ya Kameli, ili mle matunda yake na vitu vingine vyema! Lakini mlipokuja, mliitia unajisi nchi yangu, mliufany urithi wangu kuwa chukizo!
And I brought you into a land of fruitful fields, to eat the fruit thereof and the good thereof; but when ye entered, ye defiled My land, and made My heritage an abomination.
8 Hata makuhani hawakusema, 'BWANA yuko wapi?' na watalamu wa sheria hawakunijali mimi! wachungaji wametenda dhambi dhidi yangu. Manabii wamemtolea Baali unabii na kuvitafuta vitu ambvyo havina faida.
The priests said not: 'Where is the LORD?' And they that handle the law knew Me not, and the rulers transgressed against Me; the prophets also prophesied by Baal, and walked after things that do not profit.
9 Kwa hiyo nitaendelea kuwashitaki - hili ni neno la BWANA - na nitawashitiki watoto wa watoto wenu.
Wherefore I will yet plead with you, saith the LORD, and with your children's children will I plead.
10 Kwa kuvuka kwenda hadi pwani ya Kitimu na kutazama. Tuma wajumbe kwenda Kedari na tafuta uone kama kama iliwahi kutokea hapo awali vitu kama hivi.
For pass over to the isles of the Kittites, and see, and send unto Kedar, and consider diligently, and see if there hath been such a thing.
11 Je, taifa limebadilisha miungu, hata kama haikuwa miungu? Lakini watu wangu wameubadili utukufu wao kwa kitu ambacho hakiwezi kuwasaidia.
Hath a nation changed its gods, which yet are no gods? But My people hath changed its glory for that which doth not profit.
12 Sitajabuni, enyi mbingu kwa sababu ya hili! Tetemekeni na kuogopa -asema BWANA.
Be astonished, O ye heavens, at this, and be horribly afraid, be ye exceeding amazed, saith the LORD.
13 Kwa kuwa watu wangu wametenda maovu mawili dhidi yangu: Wameziacha chemichemi za maji ya uhai kwa kuchimba mabarika kwa ajili yao, mabarika yanayovuja yasiyoweza kutunza maji!
For My people have committed two evils: they have forsaken Me, the fountain of living waters, and hewed them out cisterns, broken cisterns, that can hold no water.
14 Je, Israeli ni mtumwa? Kwani hakuzaliwa nyumbani? Kwa nini sasa amekuwa nyara?
Is Israel a servant? Is he a home-born slave? Why is he become a prey?
15 Wanasimba wameunguruma dhidi yake. Wamepiga kelele sana na kuifanya kuwa ukiwa. Miji yake imeharibiwa na kubaki bila watu.
The young lions have roared upon him, and let their voice resound; and they have made his land desolate, his cities are laid waste, without inhabitant.
16 Pia watu wa Nufu na Tahapanesi watakinyoa kichwa chako.
The children also of Noph and Tahpanhes feed upon the crown of thy head.
17 Je, hamkufanya haya kwa ajili yenu mlipomwacha BWANA, wakati Mungu wenu, alipokuwa akiwaongoza njiani?
Is it not this that doth cause it unto thee, that thou hast forsaken the LORD thy God, when He led thee by the way?
18 Kwa hiyo, kwa nini kutafuta msaada Misri na kunywa maji ya Shihori? Kwa nini kutafuta msaada Ashuru na kunywa maji ya Mto Frati?
And now what hast thou to do in the way to Egypt, to drink the waters of Shihor? Or what hast thou to do in the way to Assyria, to drink the waters of the River?
19 Uovu wako unakukemea, na maasi yako yatakuadhibu. Kwa hiyo yafikiri hayo; tambua kuwa ni uovu na uchungu kwenu ninyi kuniacha mimi, BWANA Mungu wako, na kutokuwa na hofu yangu - asema BWANA wa majeshi.
Thine own wickedness shall correct thee, and thy backslidings shall reprove thee: know therefore and see that it is an evil and a bitter thing, that thou hast forsaken the LORD thy God, neither is My fear in thee, saith the Lord GOD of hosts.
20 Kwa kuwa niliivunja nira yenu mliyokuwa nayo wakati wa kale; Nilivichana vifungo vyako kutoka kwako. Lakini bado ulisema, 'Sitamtumikia!' tangu ulipopiga magoti katika kila kilima kuusogelea kila mti wenye majani mabichhi, enyi makahaba.
For of old time I have broken thy yoke, and burst thy bands, and thou saidst: 'I will not transgress'; upon every high hill and under every leafy tree thou didst recline, playing the harlot.
21 Lakini mimi mwenyewe niliwapanda kama mzabibu niliouchagua, mbegu iliyokamilika. Lakini tazama jinsi ulivyobadilika mbele yangu, na kuwa mzabibu usiofaa na mzabibu pori!
Yet I had planted thee a noble vine, wholly a right seed; how then art thou turned into the degenerate plant of a strange vine unto Me?
22 Kwa kuwa hata kama utajisafisha mwenyewe mtoni na kuoga kwa sabuni kali, bado dhambi yako ni madoa mbele yangu - asema BWANA Mungu.
For though thou wash thee with nitre, and take thee much soap, yet thine iniquity is marked before Me, saith the Lord GOD.
23 Wawezaje kusema, 'Mimi sijanajisika! Mimi sjaenda kwa Mabaal?' Tazama tabia zako zilivyokuwa bondeni! Tambua kile ulichofanya, wewe ngamia mwepesi! akimbiaye katika njia yake!
How canst thou say: 'I am not defiled, I have not gone after the Baalim'? See thy way in the Valley, know what thou hast done; thou art a swift young camel traversing her ways;
24 Wewe ni punda wa mwitu, aliyeizoelea nyika, avutaye pumzi za upepo usiofaa katika tamaa ya kuishi! Ni nani awezaye kumgeuza anapotafuta dume la kumpanda? Na punda dume amtafutaye hajichoshi mwenyewe. Huenda kwake wakati wa mwezi wa kupandwa.
A wild ass used to the wilderness, that snuffeth up the wind in her desire; her lust, who can hinder it? All they that seek her will not weary themselves; in her month they shall find her.
25 Lazima uizuie miguu yako isikose kiatu na koo lako kuwa na kiu! Lakini umesema, 'Hakuna matumaini! Hapana! Nawapenda wageni nami huwatafuta!'
Withhold thy foot from being unshod, and thy throat from thirst; but thou saidst: 'There is no hope; no, for I have loved strangers, and after them will I go.'
26 Kama aibu ya mwizi ilivyo anapokuwa amekamatwa, ndivyo aibu ya Israeli itakavyokuwa - wao, wafalme wao, malikia wao, makuhani na manabii wao!
As the thief is ashamed when he is found, so is the house of Israel ashamed; they, their kings, their princes, and their priests, and their prophets;
27 Hawa ndio wale waiambiayo miti, 'Ninyi ndio baba zangu,' na mawe, 'Ninyi ndio mlinizaa.' Kwa kuwa migongo yao hunitazama na siyo nyuso zao. Hata hivyo, wakati wa shida husema, 'Amka utuokoe!'
Who say to a stock: 'Thou art my father', and to a stone: 'Thou hast brought us forth', for they have turned their back unto Me, and not their face; but in the time of their trouble they will say: 'Arise, and save us.'
28 Lakini iko wapi ile miungu mliyojitengenezea? Acha hao wainuke kama wanaweza kuwaokoa wakati wa shida, kwa kuwa hizo sanamu zenu zina idadi sawa na miji yenu, katika Yuda.
But where are thy gods that thou hast made thee? Let them arise, if they can save thee in the time of thy trouble; for according to the number of thy cities are thy gods, O Judah.
29 Kwa hiyo kwa nini kunituhumu kwa kufanya makosa? Ninyi nyote mmeniasi - asema BWANA wa majeshi.
Wherefore will ye contend with Me? Ye all have transgressed against Me, saith the LORD.
30 Nimewadhibu watu wenu bure. Wala hawakutaka kurudiwa. Upanga wako umewaangamiza manabii wenu kama kama simba aangamizaye!
In vain have I smitten your children — they received no correction; your sword hath devoured your prophets, like a destroying lion.
31 Enyi watu wa kizazi hiki! Sikilizeni neno langu, neno la BWANA! Je, nimekuwa jangwa kwa Israeli? Au nchi yenye giza nene? Kwa nini watu wangu husema, 'Acha tuzungukezunguke, hatutakuja kwako tena'?
O generation, see ye the word of the LORD: have I been a wilderness unto Israel? or a land of thick darkness? Wherefore say My people: 'We roam at large; we will come no more unto Thee'?
32 Je, mwanamwali anaweza kusahau mapambo yake, na bibi arusi mavazi yake? Lakini watu wngu wamenisahau mimi kwa siku nyingi!
Can a maid forget her ornaments, or a bride her attire? Yet My people have forgotten Me days without number.
33 Jinsi mlivyotengeneza njia zenu vizuri ili kutafuta mapenzi. Hata mmewafundisha njia zenu wanawake waovu.
How trimmest thou thy way to seek love! Therefore — even the wicked women hast thou taught thy ways;
34 Damu ambayo ilikuwa ndio uhai wa watu wasio na hatia, imeonekana katika mavazi yenu. Hawa watu hawajawahi kuonekana katika matendo maovu.
Also in thy skirts is found the blood of the souls of the innocent poor; thou didst not find them breaking in; yet for all these things
35 Pamoja na mambo haya yote, wewe unaeendelea kusema kuwa hauna hatia. Kwa hakika hasira ya BWANA itageuka kutoka kwangu. 'Lakini tazama! Utahukumiwa kwa sababu, 'Sikutenda dhambi.'
Thou saidst: 'I am innocent; surely His anger is turned away from me' — behold, I will enter into judgment with thee, because thou sayest: 'I have not sinned.'
36 Kwa nini mnatangatanga kwa urahisi katika njia zenu? Pia Misri itawahuzunisha sana, kama ilivyokuwa kwa Ashuru.
How greatly dost thou cheapen thyself to change thy way? Thou shalt be ashamed of Egypt also, as thou wast ashamed of Asshur.
37 Mtaondoka hapo mkiwa mmehuzunika sana, mkiwa mmeweka mikono vichwani mwenu, kwa kuwa BWANA amemkutaa yule mliyemtumainia, kwa hiyo hamtapata msaada toka kwao,”
From him also shalt thou go forth, with thy hands upon thy head; for the LORD hath rejected them in whom thou didst trust, and thou shalt not prosper in them.

< Yeremia 2 >