< Yeremia 28 >

1 Ilitokea katika mwaka ule, mwanzoni mwa utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda, katika mwaka wa nne na mwezi wa tano, Hanania mwana wa Azuri nabii, alikuwa wa Gibeoni, alisema kwangu katika nyumba ya Yahwe mbele za makuhani na watu wote. Alisema,
And it came to pass the same year, in the beginning of the reign of Zedekiah king of Judah, in the fourth year, in the fifth month, that Hananiah the son of Azzur the prophet, who was of Gibeon, spoke unto me in the house of the LORD, in the presence of the priests and of all the people, saying:
2 “Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nimeivunja nira iliyowekwa na mfalme wa Babeli.
'Thus speaketh the LORD of hosts, the God of Israel, saying: I have broken the yoke of the king of Babylon.
3 Ndani ya miaka miwili nitavirudisha katika sehemu hii vyombo vyote vya nyumba ya Yahwe ambavyo Nebukadreza mfalme wa Babeli livichukua kutoka sehemu hii na kuvisafirisha hadi Babeli.
Within two full years will I bring back into this place all the vessels of the LORD'S house, that Nebuchadnezzar king of Babylon took away from this place, and carried them to Babylon;
4 Kisha nitawarudisha katika sehemu hii Yekonia mwana wa Yehotakimu, mfalme wa Yuda, na mateka wote wa Yuda ambao walipelekwa Babeli—hili ni tangazo la Yahwe—kwa maana nitaivunja nira ya mfalme wa Babeli.”
and I will bring back to this place Jeconiah the son of Jehoiakim, king of Judah, with all the captives of Judah, that went to Babylon, saith the LORD; for I will break the yoke of the king of Babylon.'
5 Kwa hiyo Yeremia nabii akasema kwa Hanania nabii mbele ya makuhani na kwa watu wote waliosimama katika nyumba ya Yahwe.
Then the prophet Jeremiah said unto the prophet Hananiah in the presence of the priests, and in the presence of all the people that stood in the house of the LORD,
6 Yeremia nabii akasema, “Yahwe afanye hivi! Yahwe ayathibitishe maneno ambayao ulitabiri na kuvirudisha katika sehemsu hii vyombo vya nyumb a ya Yahwe, na mateka wote kutoka Babeli.
even the prophet Jeremiah said: 'Amen! the LORD do so! the LORD perform thy words which thou hast prophesied, to bring back the vessels of the LORD'S house, and all them that are carried away captive, from Babylon unto this place!
7 Vile vile, sikilizeni neno ambaloo ninalitangaza katika masikio yenu na katika masikio ya watu wote.
Nevertheless hear thou now this word that I speak in thine ears, and in the ears of all the people:
8 Manabii ambao walikuwepo mbele yangu na na mbele yenu muda mrefu uliopita pia walitabiri kuhusu mataifa mengi na juu ya falme kuu, kuhusu vita, njaa, na mapigo.
The prophets that have been before me and before thee of old prophesied against many countries, and against great kingdoms, of war, and of evil, and of pestilence.
9 Kwa hiyo nabii anayetabiri kwamba kutakuwa na amani—kama neno lake litatimia, basi itajulikana kwamba yeye ni nabii kweli aliyetumwa na Yahwe.”
The prophet that prophesieth of peace, when the word of the prophet shall come to pass, then shall the prophet be known, that the LORD hath truly sent him.'
10 Lakini Hanania nabii akaichukua nira kutoka kwenye shingo ya Yeremia na kuivunja.
Then Hananiah the prophet took the bar from off the prophet Jeremiah's neck, and broke it.
11 Kisha Hanania akanena mbele ya watu wote na kusema, “Yahwe anasema hivi: Kama hivi tu, ndani ya miaka miwili nitaivunja nira iliyowekwa na Nebukadreza mfalme wa Babeli kutoka kwenye shingo ya kila taifa.” Kisha Yeremia nabii akaenda njia yake.
And Hananiah spoke in the presence of all the people, saying: 'Thus saith the LORD: Even so will I break the yoke of Nebuchadnezzar king of Babylon from off the neck of all the nations within two full years.' And the prophet Jeremiah went his way.
12 Baada ya Hanania nabii kuivunja nira kutoka kwenye shingo ya Yeremia nabii, neno la Yahwe likamjia Yeremia. likisema,
Then the word of the LORD came unto Jeremiah, after that Hananiah the prophet had broken the bar from off the neck of the prophet Jeremiah, saying:
13 Nenda na ukaseme kwa Hanania na useme, Yahwe anasema hivi: Uliivunja nira ya mbao, lakini badala yake nitafanya nira ya chuma.'
'Go, and tell Hananiah, saying: Thus saith the LORD: Thou hast broken the bars of wood; but thou shalt make in their stead bars of iron.
14 Kwa maana Yahwe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nimeweka nira ya chuma shingoni mwa mataifa haya yote ili wamtumikea Nebukadreza mfalme wa Babeli, na watamtumikia. Pia nimempa wanyama wa mashambani awatawale.”
For thus saith the LORD of hosts, the God of Israel: I have put a yoke of iron upon the neck of all these nations, that they may serve Nebuchadnezzar king of Babylon; and they shall serve him; and I have given him the beasts of the field also.'
15 Kisha nabii Yeremia akamwambia Hanania nabii, “Sikiliza Hanania! Yahwe hajakutuma, bali wewe mwenyewe umewasababisha watu hawa kuamini katika uongo.
Then said the prophet Jeremiah unto Hananiah the prophet: 'Hear now, Hananiah; the LORD hath not sent thee; but thou makest this people to trust in a lie.
16 Kwa hiyo Yahwe anasema hivi: Angalia, niko karibu kukutuma nje ya dunia. Mwaka huu utakufa.”
'Therefore thus saith the LORD: Behold, I will send thee away from off the face of the earth; this year thou shalt die, because thou hast spoken perversion against the LORD.'
17 Katika mwezi wa saba wa mwaka ule ule, Hanania nabii akafa.
So Hananiah the prophet died the same year in the seventh month.

< Yeremia 28 >