< Yeremia 22 >

1 Bwana asema hivi, “Nenda kwenye nyumba ya mfalme wa Yuda, utangaze neno hili huko.
Thus said the LORD: Go down to the house of the king of Judah, and speak there this word,
2 Ukaseme, 'Ewe Mfalme wa Yuda, wewe aliyeketi kiti cha Daudi, usikilize neno la Bwana. Nisikilizeni, enyi watumishi wake, na ninyi, watu wake mnaokuja kwa malango haya.
and say: Hear the word of the LORD, O king of Judah, that sittest upon the throne of David, thou, and thy servants, and thy people that enter in by these gates.
3 Bwana asema hivi, “Fanya haki na uadilifu, na mtu yeyote ambaye ameibiwa-muokoeni kutoka mkononi mwa mshindani. Usimtendee mabaya mgeni yeyote katika nchi yako, au yatima au mjane. Usifanye vurugu au kumwaga damu isiyo na hatia mahali hapa.
Thus saith the LORD: Execute ye justice and righteousness, and deliver the spoiled out of the hand of the oppressor; and do no wrong, do no violence, to the stranger, the fatherless, nor the widow, neither shed innocent blood in this place.
4 Kwa kuwa mkifanya mambo hayo, basi wafalme wanaoketi kiti cha Daudi wataingia milango ya nyumba hii wakiendesha gari na farasi, yeye, watumishi wake, na watu wake!
For if ye do this thing indeed, then shall there enter in by the gates of this house kings sitting upon the throne of David, riding in chariots and on horses, he, and his servants, and his people.
5 Lakini ikiwa hamsikilizi maneno haya kutoka kwangu ambayo nimeyasema-hili ndilo tamko la Bwana-basi nyumba hii ya kifalme itaharibiwa.'”
But if ye will not hear these words, I swear by Myself, saith the LORD, that this house shall become a desolation.
6 Kwa maana Bwana asema hivi juu ya nyumba ya mfalme wa Yuda, “Wewe uko kama Gileadi, au kama kilele cha Lebanoni kwangu. Hata hivyo nitakugeuza kuwa jangwa, katika miji isiyo na wenyeji.
For thus saith the LORD concerning the house of the king of Judah: Thou art Gilead unto Me, the head of Lebanon; yet surely I will make thee a wilderness, cities which are not inhabited.
7 Kwa kuwa nimewaagiza waharibifu kuja juu yenu! Watu wenye silaha zao watakata mierezi yako iliyo bora na kuiacha kuanguka kwenye moto.
And I will prepare destroyers against thee, every one with his weapons; and they shall cut down thy choice cedars, and cast them into the fire.
8 Kisha mataifa mengi yatapita kwenye mji huu. Kila mtu atamwambia yule anayefuata, “Mbona Bwana amefanya hivi kwa jiji hili kuu?”
And many nations shall pass by this city, and they shall say every man to his neighbour: 'Wherefore hath the LORD done thus unto this great city?'
9 Na mwingine atajibu, “Kwa sababu waliiacha agano la Bwana, Mungu wao, wakainama kwa miungu mingine, wakaiabudu.”
Then they shall answer: 'Because they forsook the covenant of the LORD their God, and worshipped other gods, and served them.'
10 Usilie kwa ajili ya aliyekufa. Usiomboleze kwa ajili yake. Lakini mlilie mtu yeyote anayeingia kifungoni, kwa maana hatarudi tena kuiona nchi aliyozaliwa.'
Weep ye not for the dead, neither bemoan him; but weep sore for him that goeth away, for he shall return no more, nor see his native country.
11 Maana Bwana asema hivi juu ya Yehoahazi, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, aliyekuwa mfalme badala ya Yosia babaye, 'ametoka mahali hapa, wala hatarudi.
For thus saith the LORD touching Shallum the son of Josiah, king of Judah, who reigned instead of Josiah his father, and who went forth out of this place: He shall not return thither any more;
12 Atakufa huko mahali ambapo walimchukua mateka, na hataiona tena nchi hii.'
but in the place whither they have led him captive, there shall he die, and he shall see this land no more.
13 Ole mtu yeyote anayejenga nyumba yake kwa uovu na vyumba vyake vya juu katika udhalimu; ambao wengine hufanya kazi, lakini hawalipwi.
Woe unto him that buildeth his house by unrighteousness, and his chambers by injustice; that useth his neighbour's service without wages, and giveth him not his hire;
14 Ole mtu yeyote atakayesema, 'Nitajenga nyumba ndefu na vyumba vya juu vipana, na hujenga madirisha mapana, na kuta zenye mwerezi, na huipaka rangi nyekundu.'
That saith: 'I will build me a wide house and spacious chambers', and cutteth him out windows, and it is ceiled with cedar, and painted with vermilion.
15 Je, hii ndiyo inakufanya uwe mfalme mzuri, kwamba unataka kuwa na mbao za mwerezi? Je baba yako hakula na kunywa, lakini lakini alifanya hukumu na haki? Kisha mambo yakawa mazuri kwa ajili yake.
Shalt thou reign, because thou strivest to excel in cedar? Did not thy father eat and drink, and do justice and righteousness? Then it was well with him.
16 Alihukumu maneno ya masikini na mhitaji. Ilikuwa vizuri. Je, huku siko kunijua mimi? - hili ni tamko la Bwana.
He judged the cause of the poor and needy; then it was well. Is not this to know Me? saith the LORD.
17 Lakini hakuna kitu machoni na moyoni mwako isipokuwa wasiwasi kwa faida yako isiyo ya haki na kwa kumwaga damu isiyo na hatia, kwa ukandamizaji kuwatendea jeuri wengine.
But thine eyes and thy heart are not but for thy covetousness, and for shedding innocent blood, and for oppression, and for violence, to do it.
18 Kwa hiyo Bwana asema hivi juu ya Yehoyakimu, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda. Hawatamwomboleza wakisema 'ole, ndugu yangu! au 'Ole, dada yangu!' Hawataomboleza kwa kusema 'Ole, bwana! ' au 'ole, utukufu!'
Therefore thus saith the LORD concerning Jehoiakim the son of Josiah, king of Judah: They shall not lament for him: 'Ah my brother!' or: 'Ah sister!' They shall not lament for him: 'Ah lord!' or: 'Ah his glory!'
19 Atazikwa maziko ya punda, ataburuzwa mbali na kutupwa nje ya milango ya Yerusalemu.
He shall be buried with the burial of an ass, drawn and cast forth beyond the gates of Jerusalem.
20 Panda milima ya Lebanoni piga kelele. Paza sauti yako Bashani. Piga kelele kutoka kwenye milima ya Abarimu, kwa maana marafiki zako wote wataharibiwa.
Go up to Lebanon, and cry, and lift up thy voice in Bashan; and cry from Abarim, for all thy lovers are destroyed.
21 Nilinena nawe wakati ulioko salama, lakini ukasema, 'Sitasikia.' Hii ilikuwa desturi yako tangu ujana wako, kwani hukusikiliza sauti yangu.
I spoke unto thee in thy prosperity, but thou saidst: 'I will not hear.' This hath been thy manner from thy youth, that thou hearkenedst not to My voice.
22 Upepo utawalisha wachungaji wako wote, na marafiki zako watakwenda kufungwa. Hakika wewe utakuwa na aibu na kufadhaika kwa matendo yako yote mabaya.
The wind shall feed upon all thy shepherds, and thy lovers shall go into captivity; surely then shalt thou be ashamed and confounded for all thy wickedness.
23 Wewe mfalme, wewe ambaye huishi katika Nyumba ya Msitu wa Lebanoni, wewe aliyefanya kiota kati ya mierezi, utakuwa na hali ya kuhurumiwa utakapopata utungu kama wakati wa kuzaa.”
O inhabitant of Lebanon, that art nestled in the cedars, how gracious shalt thou be when pangs come upon thee, the pain as of a woman in travail!
24 “Kama mimi niishivyo-hili ndilo tamko la Bwana-hata kama wewe, Konia, mwana wa Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, ulikuwa alama ya mkono wangu wa kulia, ningekuangusha.
As I live, saith the LORD, though Coniah the son of Jehoiakim king of Judah were the signet upon My right hand, yet would I pluck thee thence;
25 Kwa kuwa nimewatia mikono ya wale wanaotaka uhai wenu na kwenye mkono wa wale ambao mnawaogopa, hata mkononi mwa Nebukadreza, mfalme wa Babeli na Wakaldayo.
and I will give thee into the hand of them that seek thy life, and into the hand of them of whom thou art afraid, even into the hand of Nebuchadrezzar king of Babylon, and into the hand of the Chaldeans.
26 Nitawatupa wewe na mama yako aliyekuzaa katika nchi nyingine, nchi ambayo hujazaliwa, na huko utakufa.
And I will cast thee out, and thy mother that bore thee, into another country, where ye were not born; and there shall ye die.
27 Na kuhusu eneo hili ambalo watataka kurudi, hawatarudi hapa.
But to the land whereunto they long to return, thither shall they not return.
28 Je! Hiki ni chombo kilichodharauliwa na kilichopasuka? Je, Konia ni chombo kilichodharauliwa? Kwa nini wamemtupa yeye na wazao wake, kumpeleka katika nchi wasiyoijua?
Is this man Coniah a despised, broken image? Is he a vessel wherein is no pleasure? Wherefore are they cast out, he and his seed, and are cast into the land which they know not?
29 Ee Ardhi, Ardhi, Ardhi! Sikieni neno la Bwana!
O land, land, land, hear the word of the LORD.
30 Bwana asema hivi, 'Andika juu ya mtu huyu Konia Yeye hatakuwa na mtoto. Hatafanikiwa wakati wa siku zake, wala hakuna hata mmoja kati ya uzao wake atakayefanikiwa au kuketi tena kwenye kiti cha Daudi na kutawala juu ya Yuda.'”
Thus saith the LORD: Write ye this man childless, a man that shall not prosper in his days; for no man of his seed shall prosper, sitting upon the throne of David, and ruling any more in Judah.

< Yeremia 22 >