< Yakobo 3 >

1 Ndugu zangu, siyo wengi wenu mnapaswa kuwa walimu, mkijua kwamba tutapokea hukumu kubwa zaidi.
Братя мои, не ставайте мнозина учители, като знаете, че ще приемем по-тежко осъждане.
2 Kwa kuwa wote tunakosea katika njia nyingi. Kama yeyote huwa hajikwai katika maneno yake, huyo ni mtu mkamilifu, aweza kudhibiti mwili wake wote pia.
Защото всички ние в много неща грешим; а който не греши в говорене, той е съвършен мъж, способен да обуздае и цялото тяло.
3 Sasa kama tunaweka lijamu za farasi katika vinywa vyao wanatutii, na tunaweza kuigeuza miili yao yote.
Ето, ние туряме юздите в устата на конете, за да ни се покоряват, и обръщаме цялото им тяло.
4 Tambua pia kwamba meli, ingawa ni kubwa na husukumwa na upepo mkali, zinaongozwa kwa usukani mdogo sana kwenda popote anakotaka nahodha.
Ето, и корабите, ако да са толкова големи, и се тласкат от силни ветрове, пак с твърде малко кормило се обръщат на където желае кормчията.
5 Vivyo hivyo, ulimi ni kiungo kidogo cha mwili, lakini hujisifia makuu sana. Angalia msitu mkubwa unavyoweza kuwashwa kwa cheche ndogo ya moto!
Така и езикът е малка част от тялото, но много се хвали. Ето, съвсем малко огън, колко много вещество запалва!
6 Ulimi pia ni moto, ni ulimwengu wa uovu, umewekwa miongoni mwa viungo vya mwili wetu, ambao hunajisi mwili wote na huiweka juu ya moto njia ya maisha, na wenyewe kuchomwa moto wa kuzimu. (Geenna g1067)
И езикът, тоя цял свят от нечестие, е огън. Между нашите телесни части езикът е, който заразява цялото тяло и запалва колелото на живота, ни, а сам той се запалва от пъкъла. (Geenna g1067)
7 Kila aina ya mnyama wa polini, ndege, kitambaacho na kiumbe cha baharini kinadhibitiwa na wanadamu.
Защото всякакъв вид зверове, птици, гадини, и морски животни се укротяват и укротени са били от човечеството;
8 lakini hakuna mwanadamu hata mmoja ambaye anaweza kudhibiti ulimi; ni uovu usiotulia, umejaa sumu ya kufisha.
но езикът никой човек не може да укроти; буйно зло е, пълен е със смъртоносна отрова.
9 Kwa ulimi twamtukuza Bwana na Baba yetu, na kwa huo twawalaani watu ambao wameumbwa kwa mfano wa Mungu.
С него благославяме Господа и Отца, и с него кълнем човеците създадени по Божие подобие!
10 Katika kinywa hichohicho husema maneno ya baraka na laana. Ndugu zangu mambo haya hayapaswi kuwa.
От същите уста излизат благословения и проклятия! Братя мои, не трябва това така да бъде.
11 Je, kisima kimoja huweza kutoa maji matamu na machungu?
Изворът пуща ли от същото отверстие сладка и горчива вода?
12 Ndugu zangu, Je, mti wa mtini unaweza kuzaa matunda ya mzeituni, au mzabibu unazaa matunda ya mtini? Wala chemchemi ya maji chumvi haitoi maji yasio na chumvi.
Възможно ли е, братя мои смоковницата да роди маслини, или лозата смокини? Така също не може солената вода да дава сладка.
13 Ni nani miongoni mwenu aliye na hekima na ufahamu? Hebu mtu huyo na aoneshe maisha mema katika kazi zake kwa unyenyekevu utokanao na hekima.
Кой от вас е мъдър и разумен? Нека показва своите дела чрез добрият си живот, с кротостта на мъдростта.
14 Lakini kama mnao wivu mkali na nia ya ubinafsi mioyoni mwenu, msijivune na kusema uongo mkiupinga ukweli.
Но ако в сърцето си имате горчива завист и крамолничество, не се хвалете и не лъжете против истината.
15 Hii siyo hekima ile ishukayo kutoka juu, lakini badala yake ni ya kidunia, si ya kiroho, na ni ya kipepo.
Това не е мъдрост, която слиза отгоре, но е земна, животинска, бесовска;
16 Kwa kuwa palipo na wivu na ubinafsi upo, kuna vurugu na kila matendo maovu
защото, гдето има завист и крамолничество, там има бъркотия и всякакво лошо нещо.
17 Lakini hekima itokayo juu, kwanza ni safi, kisha kupenda amani, upole na ukarimu, yenye kujaa rehema na matunda mema, bila kupendelea watu fulani, na kweli.
Но мъдростта, която е отгоре, е преди всичко чиста, после миролюбива, кротко умолима, пълна с милост и добри плодове, примирителна, нелицемерна.
18 Na tunda la haki hupandwa katika amani kwa wale ambao wanatenda mambo ya amani.
А плодът на правдата се сее с мир от миротворците.

< Yakobo 3 >