< Isaya 7 >

1 Siku zile wakati Ahazi mtoto wa Yothani mtoto wa Uzia, mfalme wa Yuda, Rezeni mfalme wa Amramu, na Peka mtoto wa Remaelia, mfalme wa Israeli, walienda Yerusalemu kupigana vita nao, lakini hawakuweza kushinda vita.
And it came to pass in the days of Achaz [the son] of Joatham, the son of Ozias, king of Juda, there came up Rasim king of Aram, and Phakee son of Romelias, king of Israel, against Jerusalem to war against it, but they could not take it.
2 Ilitaarifiwa kwa nyumba ya Daudi kwamba Amramu amejiunga na Efraimu. Moyo wake na moyo watu wake ukatetemeka, kama vile miti ya misitu inavyopepea kwa upepo.
And a message was brought to the house of David, saying, Aram has conspired with Ephraim. And his soul was amazed, and the soul of his people, as in a wood a tree is moved by the wind.
3 Ndipo Yahwe akamwambia Isaya, ''Nenda nje na kijana wako, Sheari Jashubu ukaonane na Ahazi mwisho wa mfereji wa birika la juu, katika njia kuu ya uwanja Dobi.
And the Lord said to Esaias, Go forth to meet Achaz, you, and your son Jasub who is left, to the pool of the upper way of the fuller's field.
4 Mwambie, 'awe makini, awe mtulivu, asiogope au vitisho kwa sababu ya mikia hii miwili ya vingi hivi vitokavyo moshi, kwa sababu ya hasira kubwa ya Resini na Amramu, na mtoto wa Remalia.
And you shall say to him, Take care to be quiet, and fear not, neither let your soul be disheartened because of these two smoking firebrands: for when my fierce anger is over, I will heal again.
5 Amramu, Ephraimu, na mtoto wa Remaeli wamepanga mabaya juu yako; wamesema, '' njooni tuwavamie Yuda na kuwaogopesha,
And [as for] the son of Aram, and the son of Romelias, forasmuch as they have devised an evil counsel, [saying],
6 njooni tujipange na tumueweke mfalme wetu ndani ya Yuda, mtoto wa Tabaeli.''
We will go up against Judea, and having conferred with them we will turn them away to our side, and we will make the son of Tabeel king of it;
7 Bwana Yahwe asema, ''haitatokea; haitaonekana,
thus says the Lord of hosts, This counsel shall not abide, nor come to pass.
8 maana kichwa cha Amramu ni Damaskasi, na kishwa cha Damaskasi ni Rezini. Ndani ya miaka sitini na tano, ndoto za Ephraimu zitasambaratishwa na hapatakuwa na watu.
But the head of Aram is Damascus, and the head of Damascus, Rasim; and yet within sixty and five years the kingdom of Ephraim shall cease from [being] a people.
9 Efraimu ni kichwa Samaria, na kishwa cha Samaria ni mtoto wa Remaria. Na kama hamtasimama imara katika imani yenu, hakika hamtakuwa salama''.
And the head of Ephraim is Somoron, and the head of Somoron the son of Romelias: but if you believe not, neither will you at all understand.
10 Bwana akaongea tena na Ahazi,
And the Lord again spoke to Achaz, saying,
11 ''Omba ishara ya Yahwe Mungu wako; omba juu ya hilo kwa kina au kwa kiwango cha juu.'' (Sheol h7585)
Ask for yourself a sign of the Lord your God, in the depth or in the height. (Sheol h7585)
12 Lakini Ahazi anasema, sintomba wala kumjaribu Yahwe.''
And Achaz said, I will not ask, neither will I tempt the Lord.
13 Hivyo Isaya akajibu, ''sikilizen, nyumba ya Daudi. Je haijatosha kwa watu kuujaribu uvumilivu wa watu? Je ni lazima kuujaribu uvumilivu wa Mungu?
And he said, Hear you now, O house of David; is it a little thing for you to contend with men? and how do you contend against the Lord?
14 Hivyo basi Mungu mwenyewe atawapa yeye mwenywe ishara: ona, mwanamke bikira atapata mimba na kumzaa mtoto, na atamwita Emanueli.
Therefore the Lord himself shall give you a sign; behold, a virgin shall conceive in the womb, and shall bring forth a son, and you shall call his name Emmanuel.
15 Atakula siagi na asali na wakati anapojua kuyakataa maovu na kuchagua mema.
Butter and honey shall he eat, before he knows either to prefer evil [or] choose the good.
16 Maana kabla mtoto ajajua kuyakataa maovu na kuchagua mema, nchi ambayo wewe unawachukia wafalme itakuwa ukiwa.
For before the child shall know good or evil, he refuses evil, to choose the good; and the land shall be forsaken which you are afraid of because of the two kings.
17 Yahwe ataleta juu yako, juu ya watu wako, na juu ya nyumba ya baba yako siku hazijatimmia tangu Efraimu alipompokea Yuda- atamleta mfalme wa Asiria.''
But God shall bring upon you, and upon your people, and upon the house of your father, days which have never come, from the day that Ephraim took away from Juda the king of the Assyrians.
18 Mda huo Yahwe atapuliza filimbikwa ajili ya kupaa kutoka mkondo wa umbali wa Misri, na maana nyuki kutoka nchi ya Asiria.
And it shall come to pass in that day that the Lord shall hiss for the flies, which [insect] shall rule over a part of the river of Egypt, and for the bee which is in the land of the Assyrians.
19 Zitakuja na kukaa chini ya korongo, ndani ya mapango ya miamba, kwenye vichaka vya miba, na kwenye malisho.
And they all shall enter into the clefts of the land, and into the holes of the rocks, and into the caves, and into every ravine.
20 Katika mda huo Bwana atamnyoa kichwani kichwani na nywele za miguuni kwa wembe ulioazimwa mto Efrarate— mfalme wa Asiria - na vilevile utasafisha ndevu zote.
In that day the Lord shall shave with the hired razor of the king of Assyria beyond the river the head, and the hairs of the feet, and will remove the beard.
21 Siku hiyo, mtu atahifadhi ndama na na kondoo wawili,
And it shall come to pass in that day, [that] a man shall rear a heifer, and two sheep.
22 na kwasababu ya maziwa yatakayo patikana ni mengi, atakula siagi, maana kila atakaye bakia kwnye nchi atakula siagi na asali.
And it shall come to pass from their drinking an abundance of milk, [that] every one that is left on the land shall eat butter and honey.
23 Mda huo, kutakuwa na maelfu ya mizabibu na thamani elfu za shekeli, hakutakuwa na kitu zaidi ya kuzalisha mbigiri na miiba.
And it shall come to pass in that day, [for] every place where there shall be a thousand vines at a thousand shekels, they shall become barren land and thorns.
24 Watu watenda pale kuwinda kwa upinde, kwa sababu nchi yote itazalisha mbigiri na miiba.
[Men] shall enter there with arrow and bow; for all the land shall be [barren] ground and thorns.
25 Watakaa mbali na vilima vitalimwa kwa jembe, kwa sababu ya hofu ya mbigiri na miiba, lakini hapo patakuwa mahali pa kuchungia ngo'mbe na kondoo
And every mountain shall be certainly ploughed: there shall no fear come there: for there shall be from [amongst] the [barren] ground and thorns that whereon cattle shall feed and oxen shall tread.

< Isaya 7 >