< Isaya 49 >

1 Nisikilize mimi, enyi mkao pwani! na kuwa makini, enyi watu mkao mbali. Yahwe amenita mimi kutoka kuzaliwa kwa jina, mama yangu aliponileta duniani.
Sh'ma ·Hear obey·, islands, to me. Listen, you peoples, from afar: Adonai has called me from the womb; from the inside of my mother he has mentioned my name.
2 Amefanya mdomo wangu kuwa kama upanga mkali; amenificha mimi katika kivuli cha mkono wake; amenifanya mimi kuwa mshale unaong'aa; katika podo yake amenificha mimi.
He has made my mouth like a sharp sword. He has hidden me in the shadow of his hand. He has made me a polished shaft. He has kept me close in his quiver.
3 Amesema na mimi, ''Wewe ni mtumishi wangu, Israeli, kupitia yeye nitaonyesha utukufu wangu.''
He said to me, “You are my servant; Israel [God prevails], in whom I will be glorified.”
4 Lakini nilimjibu, ''Japo nilifikiria nilifanya kazi bure, nimetumia nguvu zangu bure, ikiwa haki yangu iko pamoja na Yahwe, na zawadi yangu iko kwa Mungu wangu.
But I said, “I have labored in vain. I have spent my strength in vain for nothing; yet surely the mishpat ·justice· due to me is with Adonai, and my reward with my God.”
5 Na sasa Yahwe asema hivi, yeye aliyeniumba mimi toka kuzaliwa na kuwa mtumishi wake, kumrejesha Yakobo tena kwake mwenyewe, na Israeli wakusanyike kwake. Mimi ninaheshimika katika macho ya Yahwe, na Mungu wangu amekuwa nguvu zangu.
Now Adonai says, he who formed me from the womb to be his servant, to bring Jacob [Supplanter] again to him, and to gather Israel [God prevails] to him, for I am honorable in Adonai’s eyes, and my God has become my strength.
6 Asema hivi, ''Ni kitu kidogo sana kwa wewe kuwa mtumishi wangu ili kuanzisha ukoo wa Yakobo, na kuwarejesha wanaoishi Israeli. Nitakufanya wewe kuwa mwanga kwa Wayunani, ili uwe wokovu wangu katika mipaka ya nchi.
Indeed, he says, “It is too light a thing that you should be my servant to raise up the tribes of Jacob [Supplanter], and to restore the preserved of Israel [God prevails]? I will also give you as a light to the nations, that you may be my yishu'ah ·salvation·to the end of the earth.”
7 Yahwe asema hivi, Mkombozi wa Israeli, Mtatakatifu wao, kwa yeye ambae maisha yake yamedharauliwa, kuchukiwa na mataifa, na mtumwa wa viongozi, ''Mfalme atakuona wewe na nyanyuka, na wakuu watakuona wewe na inama chini, kwa sababu ya Yahwe ambae ni mwaminifu, hata mtakatifu wa Israeli, aliyewachagua ninyi.''
Adonai, the Go'eil Isra'el [Redeemer of God prevails], and his Holy One, says to him whom man despises, to him whom the nation abhors, to a servant of rulers: “Kings shall see and rise up; princes, and they shall hawa ·bow low, prostrate· to worship; because of Adonai who is faithful, even the haKadosh Isra'el [the Holy One of God prevails], who has chosen you.”
8 Yahwe asema hivi, ''Kwa mda huu nimeamua kuwaonyesha neema yangu na nitawajibu ninyi, na siku ya wokovu nitawasaidi ninyi; Nitakulinda wewe; na nitawapa kama agano kwa watu, kuitengeneza tena nchi, kuwarihtisha urithi uliokuwa na ukiwa.
Adonai says, “In an acceptable time I have answered you, and in a day of yishu'ah ·salvation· I have helped you. I will preserve you, and give you for a covenant ·binding contract between two or more parties· of the people, to raise up the land, to make them inherit the desolate heritage:
9 Utasema kwa wafungwa, 'Tokeni nje; kwa wale mlio katika giza gerezani, 'Jionyeshe mwenyewe. 'Watachunga pembeni ya barabara, na juu ya miteremko ya wazi yatakuwa malisho yake.
saying to those who are bound, ‘Come out!’; to those who are in darkness, ‘Show yourselves!’ “They shall feed along the paths, and their pasture shall be on all treeless heights.
10 Hawatasikia njaa wala kiu; wala joto au jua halitawaunguza, kwa yeye mwenye huruma juu yao atawaongoza wao; atawaongoza wao kwenye mikondo ya maji.
They shall not hunger nor thirst; neither shall the heat nor sun strike them: for he who has racham ·merciful love· towards them will lead them. He will guide them by springs of water.
11 Na nitafanya milima yote kuwa barabara, na kufanya njia za juu kuwa sawa''
I will make all my mountains a road, and my highways shall be exalted.
12 Tazama, haya yatatoka kutoka mbali, baadhi kutoka kaskazini na magharibi; na wengine kutoka nchi ya Sinimi.
Behold, these shall come from afar; and behold, these from the north and from the west; and these from the land of Sinim.”
13 Imba, ewe mbingu, na uwe na furaha, ewe nchi pazeni sauti ya kuimmba enyi milima! maana Yahwe anawafariji watu wake, na watakuwa na huruma kwa wale wanoteseka.
Sing, heavens; and be joyful, earth; and break out into singing, mountains: for Adonai has comforted his people, and will have racham ·compassionate love· on his afflicted.
14 Lakin Sayuni asema, Yahwe ameniacha mimi, na Bwana amenisahau mimi.''
But Zion [Mountain ridge, Marking] said, “Adonai has forsaken me, and the Lord has forgotten me.”
15 ''Je mwanamke anaweza kumsahau mtoto wake, aliyemnyonyesha, hivyo hana huruma na mtoto aliye mzaa? ndio, hawakusahau, lakini siwezi kukusahau wewe.
“Can a woman forget her nursing child, that she should not have racham ·compassionate love· on the son of her womb? Yes, these may forget, yet I will not forget you!
16 Tazama, nimeliandika jina lako kwenye kiganja cha mkono wangu; Kuta zako zinaendelea kuwa mbele yangu.
Behold, I have engraved you on the palms of my hands. Your walls are continually before me.
17 Watoto wangu wamerudi haraka, wakati wale wanowaangaimiza nyie wameenda mbali.
Your children hurry. Your destroyers and those who devastated you will leave you.
18 Tazama karibu na uone, wote wamekusanyika na wanakuja kwako. Nitahakikisha kama ninaishi- hili ni tamko la Yahwe- hakika mtavivaaa kama kama kijiti; utajifungia kama bibi harusi.
Lift up your eyes all around, and see: all these gather themselves together, and come to you. As I live,” says Adonai, “you shall surely clothe yourself with them all as with an ornament, and dress yourself with them, like a bride.
19 Japo umeharibiwa na kuwa na ukiwa, nchi iliyoharibiwa, sasa itakuwa ndogo sana kwa wenyeji, na wale wanao waliokumeza watakuwa mbali,
“For, as for your waste and your desolate places, and your land that has been destroyed, surely now that land will be too small for the inhabitants, and those who swallowed you up will be far away.
20 Watoto watakaozaliwa katika kipindi cha msiba watasema mkiwa mnawasikiliza, 'Sehemu hii ni duni kwetu, tengeneza chumba kwa ajili yetu, ili tuweze kuishi hapa.
The children of your bereavement will say in your ears, ‘This place is too small for me. Give me a place to live in.’
21 Halafu utajiuliza mwenyewe, ni nani aliyewazaa watu hawa kwangu? Mimi nilifiwa na ni tasa, niliyefungwa na kupewa talaka. Ni nani aliyewalea hawa watoto? Tazama, niliachiwa yote mimi mwenyewe; Je haya yametoka wapi?''
Then you will say in your heart, ‘Who has conceived these for me, since I have been bereaved of my children, and am solitary, an exile, and wandering back and forth? Who has brought these up? Behold, I was left alone. Where were these?’”
22 Yahwe asema hivi, ''Tazama, nitanyanyua mkono wangu juu ya mataifa; Nitanyanyua bendera yangu ya ishara kwa watu. Watawaleta watoto wako kwenye mikono yao na watawabeba binti zako juu ya mabega yao.
Thus says the Lord Adonai, “Behold, I will lift up my hand to the nations, and lift up my banner to the peoples; and they shall bring your sons in their bosom, and your daughters shall be carried on their shoulders.
23 Wafalme watakuwa baba zako wa kambo, na malikia watakuwa wafanyakazi wa ndani; watakuinamia chini wewe kw uso wao kwa nchi na kukung'uta mavumbi ya miguu yenu; wale wanonisubiri mimi hawataabika.''
Kings shall be your foster fathers, and their queens your nursing mothers. They will bow down to you with their faces to the earth, and lick the dust of your feet; Then you will know that I am Adonai; and those who wait for me shall not be disappointed.”
24 Je mateka wanaweza kuchukuliwa kwa shujaa, au wafungwa kukombolewa kutoka kwa mkali?
Shall the plunder be taken from the mighty, or the lawful captives be delivered?
25 Lakini Yahwe asema hivi, ''Wafungwa watachukuliwa kutoka kwa shujaa, na maeteka watakombolewa; maana utampinga adui yako na kuwakomboa watoto wako.
But Adonai says, “Even the captives of the mighty shall be taken away, and the plunder retrieved from the fierce; for I will contend with him who contends with you, and I will save your children.
26 Na nitawalisha wanowaonea kwa mwili wao wenyewe; na watalewa kwa damu zao wenyewe, kama iliyo mvinyo; na watu wote watajua kwamba Mimi Yahwe, ni Mokozi wenu na Mkombozi wenu, yeye aliyemkuu wa Isareli.
I will feed those who oppress you with their own flesh; and they will be drunk on their own blood, as with sweet wine. Then all flesh shall know that I, Adonai, am the One who saves you, and your Redeemer, the 'Avir Ya'akov [Mighty One of Supplanter].”

< Isaya 49 >