< Isaya 12 >

1 Siku hiyo utasema, ''Nitakushukuru wewe, Yahwe. Japo ulikuwa na hasira na mimi, laana yako imeondoka mbali, na umenifariji mimi,
And in that day you shall say, I [will] bless you, O Lord; for you were angry with me, but you have turned aside your wrath, and have pitied me.
2 Ona Bwana ni wokovu wangu; nitamwamini na sitakuwa na hofu, kwa Yahwe, ndio, Yahwe ni nguvu yangu na wimbo wangu. Amekuwa wokovu wangu.''
Behold, my God is my Saviour; I will trust in him, and not be afraid: for the Lord is my glory and my praise, and is become my salvation.
3 Kwa furaha utachota maji kwenye kisima cha wokovu.
Draw you therefore water with joy out of the wells of salvation.
4 Siku hiyo utasema, ''Mshukuru Yahwe na ita jina lake; tangaza matendo yake miongoni mwa watu, tangaza jina lake limeinuliwa.
And in that day you shall say, sing to the Lord, call aloud upon his name, proclaim his glorious [deeds] amongst the Gentiles; make mention that his name is exalted.
5 Mwiimbie Yahwe, maana ametenda matendo yaliotukuka; acha hili lijulikane dunia nzima.
Sing praise to the name of the Lord; for he has done great [things]: declare this in all the earth.
6 Lia kwa nguvu na piga kelele kwa furaha, enyi wakazi wa Sayuni, maana katikati yenu ni mtakatifu wa Israeli.
Exalt and rejoice, you that dwell in Sion: for the Holy One of Israel is exalted in the midst of her.

< Isaya 12 >