< Hosea 8 >

1 “Weka tarumbeta katika midomo yako! Tai anakuja juu ya nyumba ya Bwana kwa sababu watu wamevunja agano langu na waliasi dhidi ya sheria yangu.
Put the trumpet to thy mouth! Like an eagle cometh an enemy against the house of Jehovah, Because they have transgressed my covenant, And have rebelled against my law.
2 Wananililia,'Mungu wangu, sisi katika Israeli tunakujua.'
They shall say to me, My God, we know thee, we, thine Israel!
3 Lakini Israeli amekataa mema, na adui atamfuata.
Israel hath cast away what is good; The enemy shall pursue him.
4 Wameweka wafalme, lakini sio kwa shauri langu. Wamewafanya wakuu, lakini sikuwa na habari. Kwa fedha zao na dhahabu wamejifanyia sanamu wenyewe, ili wakatiliwe mbali.”
They have set up kings, but not by me; They have made princes, and I knew it not. Of their silver and their gold have they made themselves idols, That they may be brought to destruction.
5 “Ndama yako imekataliwa, Samaria. Hasira yangu inawaka juu ya watu hawa. Kwa muda gani watakuwa na hatia?
An abomination is thy calf, O Samaria! Mine anger is kindled against them; How long will it be ere they can attain to purity!
6 Kwa maana sanamu hii ilitoka Israeli; fundi aliifanya; si Mungu! Ndama ya Samaria itavunjwa vipande vipande.
For from Israel it came; The workman made it, and it is no God; Yea, into fragments shall the calf of Samaria be broken.
7 Kwa maana watu hupanda upepo na kuvuna kimbunga. Mbegu zilizosimama hazina vichwa; haitoi unga. Ikiwa itakomaa, wageni watakula.
They have sown the wind, And they shall reap the whirlwind. They shall have no standing harvest; The ear shall yield no meal; If perchance it yield, strangers shall devour it.
8 Israeli imemezwa; sasa wanalala kati ya mataifa kama kitu kisicho na maana.
Israel is swallowed up; Soon shall they become among the nations As a vessel which no one desireth.
9 Kwa maana walikwenda Ashuru kama punda wa mwitu pekee. Efraimu ameajiri wapenzi kwa ajili yake mwenyewe.
For they have gone up to Assyria, Like a solitary wild-ass; Ephraim hireth lovers;
10 Hata ingawa wameajiri wapenzi kati ya mataifa, sasa nitawakusanya pamoja. Wao wataanza kupotea kwa sababu ya unyanyasaji wa mfalme wa wakuu.
But though they hire among the nations, Soon will I gather the nations against them; Then shall they rest a little while from the burden of their king, and their princes!
11 Kwa maana Efraimu imeongeza madhabahu kwa sadaka za dhambi, lakini zimekuwa madhabahu kwa kufanya dhambi.
Ephraim hath built many altars for sin, Therefore shall he have altars for sin.
12 Niliweza kuandika sheria yangu kwao mara elfu kumi, lakini wangeiona kama kitu cha ajabu kwao.
Though I write for him many laws, They are accounted as a strange thing;
13 Kwa ajili ya dhabihu za sadaka zangu, hutoa nyama na kuila, lakini mimi, Bwana, siwakubali. Sasa nitafikiri juu ya uovu wao na kuadhibu dhambi zao. Watarudi Misri.
As to the sacrifices which they should offer me, they slay flesh and eat it; Jehovah hath no pleasure in them. Now will he remember their iniquity, And punish their sins; To Egypt shall they return.
14 Israeli amenisahau mimi, Muumba wake, na amejenga majumba. Yuda ameimarisha miji mingi, lakini nitatuma moto juu ya miji yake; itaharibu ngome zake.
For Israel hath forgotten his Maker, and builded palaces, And Judah hath multiplied fenced cities; But I will send a fire upon his cities, And it shall devour his palaces.

< Hosea 8 >