< Hosea 8 >

1 “Weka tarumbeta katika midomo yako! Tai anakuja juu ya nyumba ya Bwana kwa sababu watu wamevunja agano langu na waliasi dhidi ya sheria yangu.
"Put the trumpet to your lips. Something like an eagle is over the LORD's house, because they have broken my covenant, and rebelled against my law.
2 Wananililia,'Mungu wangu, sisi katika Israeli tunakujua.'
They cry to me, 'My God, we Israel acknowledge you.'
3 Lakini Israeli amekataa mema, na adui atamfuata.
Israel has cast off that which is good. The enemy will pursue him.
4 Wameweka wafalme, lakini sio kwa shauri langu. Wamewafanya wakuu, lakini sikuwa na habari. Kwa fedha zao na dhahabu wamejifanyia sanamu wenyewe, ili wakatiliwe mbali.”
They have set up kings, but not by me. They have made princes, and I did not approve. Of their silver and their gold they have made themselves idols, that they may be cut off.
5 “Ndama yako imekataliwa, Samaria. Hasira yangu inawaka juu ya watu hawa. Kwa muda gani watakuwa na hatia?
Let Samaria throw out his calf idol. My anger burns against them. How long will it be until they are capable of purity?
6 Kwa maana sanamu hii ilitoka Israeli; fundi aliifanya; si Mungu! Ndama ya Samaria itavunjwa vipande vipande.
For this is even from Israel. The workman made it, and it is no God; indeed, the calf of Samaria shall be broken in pieces.
7 Kwa maana watu hupanda upepo na kuvuna kimbunga. Mbegu zilizosimama hazina vichwa; haitoi unga. Ikiwa itakomaa, wageni watakula.
For they sow the wind, and they will reap the whirlwind. He has no standing grain. The stalk will yield no head. If it does yield, strangers will swallow it up.
8 Israeli imemezwa; sasa wanalala kati ya mataifa kama kitu kisicho na maana.
Israel is swallowed up. Now they are among the nations like a worthless thing.
9 Kwa maana walikwenda Ashuru kama punda wa mwitu pekee. Efraimu ameajiri wapenzi kwa ajili yake mwenyewe.
For they have gone up to Assyria, like a wild donkey wandering alone. Ephraim has hired lovers for himself.
10 Hata ingawa wameajiri wapenzi kati ya mataifa, sasa nitawakusanya pamoja. Wao wataanza kupotea kwa sababu ya unyanyasaji wa mfalme wa wakuu.
But although they sold themselves among the nations, I will now gather them; and they begin to waste away because of the oppression of the king of mighty ones.
11 Kwa maana Efraimu imeongeza madhabahu kwa sadaka za dhambi, lakini zimekuwa madhabahu kwa kufanya dhambi.
Because Ephraim has multiplied altars for sinning, they became for him altars for sinning.
12 Niliweza kuandika sheria yangu kwao mara elfu kumi, lakini wangeiona kama kitu cha ajabu kwao.
I wrote for him the many things of my law; but they were regarded as a strange thing.
13 Kwa ajili ya dhabihu za sadaka zangu, hutoa nyama na kuila, lakini mimi, Bwana, siwakubali. Sasa nitafikiri juu ya uovu wao na kuadhibu dhambi zao. Watarudi Misri.
As for the sacrifices of my offerings, they sacrifice flesh and eat it; But the LORD doesn't accept them. Now he will remember their iniquity, and punish their sins. They will return to Egypt, and will eat unclean things in Assyria.
14 Israeli amenisahau mimi, Muumba wake, na amejenga majumba. Yuda ameimarisha miji mingi, lakini nitatuma moto juu ya miji yake; itaharibu ngome zake.
For Israel has forgotten his Maker and built palaces; and Judah has multiplied fortified cities; but I will send a fire on his cities, and it will devour its fortresses."

< Hosea 8 >