< Hosea 5 >

1 Sikilizeni haya, makuhani! kuweni makini, nyumba ya Israeli! Sikilizeni, nyumba ya mfalme! Kwa maana hukumu itakuja juu yenu nyote. Mmekuwa mtego huko Mizpa na wavu uliosambazwa juu ya Tabori.
"Listen to this, you priests. Listen, house of Israel, and give ear, house of the king. For the judgment is against you; for you have been a snare at Mizpah, and a net spread on Tabor.
2 Waasi husimama sana katika mauaji, lakini nitawaadhibu wote.
The rebels are deep in slaughter; but I discipline all of them.
3 Najua Efraimu, na Israeli hajajificha kwangu. Efraimu, sasa umekuwa kama kahaba; Israeli ni unajisi.
I know Ephraim, and Israel is not hidden from me; for now, Ephraim, you have played the prostitute. Israel is defiled.
4 Matendo yao hayawataruhusu kumgeukia Mungu, maana mawazo ya uzinzi yako ndani yao, na hawatamjua Bwana.
Their deeds won't allow them to turn to their God; for the spirit of prostitution is within them, and they do not know Jehovah.
5 Kiburi cha Israeli kinawashuhudia; Kwa hiyo Israeli na Efraimu watajikwaa kwa hatia zao; na Yuda pia wataanguka pamoja nao.
The pride of Israel testifies to his face. Therefore Israel and Ephraim will stumble in their iniquity. Judah also will stumble with them.
6 Watakwenda pamoja na kondoo zao na ng'ombe zao kumtafuta Bwana, lakini hawatamuona, kwa kuwa amejiondoa kutoka kwao.
They will go with their flocks and with their herds to seek Jehovah; but they won't find him. He has withdrawn himself from them.
7 Walikuwa wasio waaminifu kwa Bwana, kwa kuwa wamezaa watoto haramu. Sasa sherehe mpya za mwezi zitawaangamiza na mashamba yao.
They are unfaithful to Jehovah; for they have borne illegitimate children. Now the new moon will devour them with their fields.
8 Piga tarumbeta huko Gibea, na tarumbeta huko Rama. Sauti ya kilio cha vita huko Beth Aveni 'Tutakufuata, Benyamini!'
"Blow the cornet in Gibeah, and the trumpet in Ramah. Sound a battle cry at Beth Aven, behind you, Benjamin.
9 Efraimu itakuwa ukiwa siku ya adhabu. Miongoni mwa makabila ya Israeli nimetangaza habari itakayotokea.
Ephraim will become a desolation in the day of rebuke. Among the tribes of Israel, I have made known that which will surely be.
10 Viongozi wa Yuda ni kama wale wanaondoao jiwe la mipaka. Nami nitamwaga ghadhabu yangu juu yao kama maji.
The princes of Judah are like those who remove a landmark. I will pour out my wrath on them like water.
11 Efraimu ameangamizwa; ameangamizwa kwa hukumu, kwa sababu ametembea kwa hiari kufuata sanamu.
Ephraim is oppressed, he is crushed in judgment; Because he is intent in his pursuit of idols.
12 Kwa hiyo nitakuwa kama nondo kwa Efraimu, na kama uozo kwa nyumba ya Yuda.
Therefore I am to Ephraim like a moth, and to the house of Judah like rottenness.
13 Efraimu alipoona ugonjwa wake, Yuda akaona jeraha lake; Efraimu akaenda Ashuru; Yuda akatuma wajumbe kwa mfalme mkuu. Lakini hakuweza kuwaponya watu au kuponya jeraha lako.
"When Ephraim saw his sickness, and Judah his wound, Then Ephraim went to Assyria, and sent to king Jareb: but he is not able to heal you, neither will he cure you of your wound.
14 Kwa hiyo nitakuwa kama simba kwa Efraimu, na kama simba kwa nyumba ya Yuda. Mimi, naam mimi, nitapotea na kwenda mbali; Nitawachukua, na hakutakuwa na mtu wa kuwaokoa.
For I will be to Ephraim like a lion, and like a young lion to the house of Judah. I myself will tear in pieces and go away. I will carry off, and there will be no one to deliver.
15 Nitakwenda na kurudi mahali pangu, mpaka watambue hatia yao na kutafuta uso wangu, hata wakanitafute kwa bidii katika dhiki yao.
I will go and return to my place, until they acknowledge their offense, and seek my face. In their affliction they will seek me earnestly."

< Hosea 5 >