< Hosea 4 >

1 Sikilizeni neno la Bwana, enyi watu wa Israeli. Bwana ana mashtaka dhidi ya wenyeji wa nchi, kwa sababu hakuna ukweli au uaminifu wa agano, hakuna ujuzi wa Mungu katika nchi.
Hear the word of Jehovah, you children of Israel; for Jehovah has a charge against the inhabitants of the land: "Indeed there is no truth, nor goodness, nor knowledge of God in the land.
2 Kuna laana, uongo, mauaji, wizi na uzinzi. Watu wamevunja mipaka yote, na damu inakuja baada ya damu.
There is cursing, lying, murder, stealing, and committing adultery; they break boundaries, and bloodshed causes bloodshed.
3 Kwa hiyo nchi inakauka, na kila mtu aliyeishi ndani yake anaangamia; wanyama katika mashamba na ndege angani, hata samaki katika bahari, wanaondolewa.
Therefore the land mourns, and all those who dwell in it will waste away, along with the animals of the field and the crawling creatures of the earth and the birds of the sky, and even the fish of the sea will be taken away.
4 Lakini usiruhusu mtu yeyote kuleta mashtaka; msiruhusu mtu yeyote ahukumu mtu mwingine. Kwa maana ninyi ndio makuhani, ninaowashtaki.
"Yet let no man bring a charge, neither let any man accuse; For your people are like those who bring charges against a priest.
5 Ninyi makuhani mtajikwaa wakati wa mchana; manabii pia watajikwaa pamoja nanyi usiku, nami nitamwangamiza mama yako.
You will stumble in the day, and the prophet will also stumble with you in the night; and I will destroy your mother.
6 Watu wangu wanaharibiwa kwa sababu ya ukosefu wa maarifa. Kwa sababu makuhani wamekataa maarifa, nami nitawakataa msiwe makuhani kwangu. Kwa sababu umesahau sheria yangu, ingawa mimi ni Mungu wako, nami pia nitasahau watoto wako.
My people are destroyed for lack of knowledge. Because you have rejected knowledge, I will also reject you, that you may be no priest to me. Because you have forgotten your God's law, I will also forget your children.
7 Makuhani wengi waliongezeka, zaidi walifanya dhambi dhidi yangu. Walibadilisha heshima zao kwa aibu.
As they were multiplied, so they sinned against me. They have exchanged their glory into shame.
8 Wanajilisha dhambi ya watu wangu; wao ni wenye tamaa zaidi ya uovu wao.
They feed on the sin of my people, and set their heart on their iniquity.
9 Itakuwa sawa kwa watu kama kwa makuhani: nitawaadhibu wote kwa matendo yao; Nitawalipa kwa matendo yao.
It will be, like people, like priest; and I will punish them for their ways, and will repay them for their deeds.
10 Watakula lakini hawatashiba; watafanya uzinzi lakini hawataongezeka, kwa sababu wamekwenda mbali na Bwana.
They will eat, and not have enough. They will play the prostitute, and will not increase; because they have abandoned giving to Jehovah.
11 Wanapenda uasherati, divai, na divai mpya, ambayo imechukua uelewa wao.
Prostitution, wine, and new wine take away understanding.
12 Watu wangu hutaka shauri kwa sanamu zao za mbao, na fimbo zao za kutembelea huwapa unabii. Kwa maana mawazo ya uasherati yamewadanganya, na wamefanya kama makahaba badala ya kuwa mwaminifu kwa Mungu wao.
My people consult with their wooden idol, and answer to a stick of wood. Indeed the spirit of prostitution has led them astray, and they have been unfaithful to their God.
13 Wanatoa sadaka juu ya milima na kuteketeza uvumba kwenye milima, chini ya mialoni, milibua na miela, kwa sababu kivuli ni nzuri. Basi binti zenu hufanya uasherati, na binti zenu wanazini.
They sacrifice on the tops of the mountains, and burn incense on the hills, under oaks and poplars and shady terebinths, because its shade is good. Therefore your daughters play the prostitute, and your brides commit adultery.
14 Mimi siwaadhibu binti zako wakati wanachagua kutenda uasherati, wala binti zako wakati wazini. Kwa maana wanaume pia wanajitoa kwa makahaba, na hutoa dhabihu ili waweze kufanya vitendo vya uasherati na makahaba. Hivyo watu wasiofahamu wataangamizwa.
I will not punish your daughters when they play the prostitute, nor your brides when they commit adultery; because the men consort with prostitutes, and they sacrifice with the shrine prostitutes; so the people without understanding will come to ruin.
15 Ingawa wewe, Israeli, umefanya uzinzi, lakini Yuda asiwe na hatia. Ninyi msiende Gilgali; msiende hadi Beth Aven. Wala msiape, “Aishivyo Bwana.”
"Though you, Israel, play the prostitute, yet do not let Judah offend; and do not come to Gilgal, neither go up to Beth Aven, nor swear, 'As Jehovah lives.'
16 Kwa maana Israeli amefanya ukaidi, kama ndama mkaidi. Je! Bwana anaweza kuwaleta kwenye malisho kama kondoo mahali penye nafasi?
For Israel has behaved extremely stubbornly, like a stubborn heifer. Then how will Jehovah feed them like a lamb in a meadow.
17 Efraimu alijiunga na sanamu; mwache peke yake.
Ephraim, joined to idols, has placed stumbling blocks against himself.
18 Hata wakati kileo chao kimeondoka wakaendelea kufanya uzinzi; watawala wake hupenda sana aibu yao.
Their drink has become sour. They play the prostitute continually. Her rulers dearly love their shameful way.
19 Upepo utamfunga kwa mabawa yake; nao wataona aibu kwa sababu ya dhabihu zao.
The wind has wrapped her up in its wings; and they shall be disappointed because of their sacrifices.

< Hosea 4 >