< Wahebrania 1 >

1 Nyakati zilizopita Mungu alizungumza na mababu zetu kupitia manabii mara nyingi na kwa njia nyingi.
Dieu, ayant autrefois, en plusieurs temps et de diverses manières, parlé aux pères par les prophètes,
2 Lakini katika siku hizi tulizonazo, Mungu ameongea nasi kupitia Mwana, ambaye alimweka kuwa mrithi wa vitu vyote, na ambaye kupitia yeye pia aliumba ulimwengu. (aiōn g165)
nous a parlé, à la fin de ces jours, par son Fils, qu'il a établi héritier de toutes choses, par lequel il a aussi créé les mondes. (aiōn g165)
3 Mwanawe ni nuru ya utukufu wake, tabia pekee ya asili yake, na anayeendeleza vitu vyote kwa neno la nguvu zake. Baada ya kukamilisha utakaso wa dhambi, aliketi chini mkono wa kulia wa enzi huko juu.
Son Fils est le rayonnement de sa gloire, l'image même de sa substance, et il soutient toutes choses par la parole de sa puissance; après nous avoir purifiés par lui-même de nos péchés, il s'est assis à la droite de la majesté des cieux,
4 Amekuwa bora kuliko malaika, kama vile jina alilolirithi lilivyo bora zaidi kuliko jina lao.
étant devenu aussi supérieur aux anges que le nom plus excellent dont il a hérité est supérieur au leur.
5 Kwa maana ni kwa malaika gani aliwahi kusema, “Wewe ni mwanangu, leo nimekuwa baba yako?” Na tena, “Nitakuwa baba kwake, naye atakuwa mwana kwangu?”
Car auquel des anges a-t-il jamais dit, « Tu es mon fils. Aujourd'hui, je suis devenu ton père? » et encore, « Je serai pour lui un Père, et il sera pour moi un Fils? »
6 Tena, wakati Mungu alipomleta mzaliwa wa kwanza ulimwenguni, husema, “Malaika wote wa Mungu lazima wamwabudu.”
Lorsqu'il introduit à nouveau le premier-né dans le monde, il dit: « Que tous les anges de Dieu se prosternent devant lui. »
7 Kuhusu malaika asema, “Yeye ambaye hufanya malaika zake kuwa roho, na watumishi wake kuwa ndimi za moto.”
Des anges, il dit, « Il fait des vents à ses anges, et ses serviteurs une flamme de feu. »
8 Lakini kuhusu Mwana husema, “Kiti chako cha enzi, Mungu, ni cha milele na milele. Fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya haki. (aiōn g165)
Mais il dit du Fils, « Ton trône, ô Dieu, est pour les siècles des siècles. Le sceptre de la droiture est le sceptre de votre Royaume. (aiōn g165)
9 Umependa haki na kuchukia uvunjaji wa sheria, kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekupaka mafuta ya furaha kuliko wenzako.”
Tu as aimé la justice et haï l'iniquité; C'est pourquoi Dieu, ton Dieu, t'a oint d'une huile de jubilation au-dessus de tes semblables. »
10 Hapo mwanzo, Bwana, uliweka msingi wa dunia. Mbingu ni kazi za mikono yako.
Et, « Toi, Seigneur, au commencement, tu as posé les fondements de la terre. Les cieux sont l'œuvre de tes mains.
11 Zitatoweka, lakini wewe utaendelea. Zote zitachakaa kama vazi.
Ils vont périr, mais toi tu continues. Ils vieilliront tous comme un vêtement.
12 Utazikunjakunja kama koti, nazo zitabadilika kama vazi. Lakini wewe ni yuleyule, na miaka yako haitakoma.”
Tu les enrouleras comme un manteau, et ils seront changés; mais tu es le même. Vos années ne manqueront pas. »
13 Lakini ni kwa malaika yupi Mungu alisema wakati wowote, “Keti mkono wangu wa kulia mpaka nitakapowafanya adui zako kuwa kiti cha miguu yako”?
Mais lequel des anges a-t-il dit à un moment donné, « Assieds-toi à ma droite, jusqu'à ce que je fasse de tes ennemis le marchepied de tes pieds? »
14 Je, malaika wote siyo roho zilizotumwa kuwahudumia na kuwatunza wale watakaourithi wokovu?
Ne sont-ils pas tous des esprits serviteurs, envoyés pour servir ceux qui doivent hériter du salut?

< Wahebrania 1 >