< Mwanzo 8 >

1 Mungu akamtazama Nuhu, wanyama wote wa mwitu, na wanyama wote wa kufugwa ambao walikuwa pamoja naye kwenye safina. Mungu akafanya upepo uvume juu ya nchi, na maji yakaanza kuzama chini.
And God remembered Noah, and every living thing, and all the cattle that were with him in the ark; and God made a wind to pass over the earth, and the waters assuaged;
2 Chemichemi za vilindi pamoja na madirisha ya mbingu vikafungwa, na mvua ikakoma kunyesha.
the fountains also of the deep and the windows of heaven were stopped, and the rain from heaven was restrained.
3 Maji ya gharika yakaanza kuzama kidogo kidogo katika nchi. na mwisho wa siku miamoja na hamsini maji yakawa yamezama chini.
And the waters returned from off the earth continually; and after the end of a hundred and fifty days the waters decreased.
4 safina ikatulia katika mwezi wa saba, siku ya kumi na saba ya mwezi, juu ya milima ya Ararati.
And the ark rested in the seventh month, on the seventeenth day of the month, upon the mountains of Ararat.
5 Maji yakaendelea kuzama chini hadi mwezi wa kumi. Siku ya kwanza ya mwezi, vilele vya milima vikaonekana.
And the waters decreased continually until the tenth month; in the tenth month, on the first day of the month, were the tops of the mountains seen.
6 Ikatokea kwamba baada ya siku arobaini Nuhu alifungua dirisha la safina ambayo aliitengeneza.
And it came to pass at the end of forty days, that Noah opened the window of the ark which he had made.
7 Akatuma kunguru na akaruka hadi maji yalipo kauka katika nchi.
And he sent forth a raven, and it went forth to and fro, until the waters were dried up from off the earth.
8 Kisha akatuma njiwa kuona kama maji yamezama chini kutoka kwenye uso wa nchi,
And he sent forth a dove from him, to see if the waters were abated from off the face of the ground.
9 lakini njiwa hakuona sehemu ya kutua unyayo wake, na akarudi kwake ndani ya safina, kwa kuwa maji yalikuwa bado yamefunika nchi yote. Akanyoosha mkono wake, akamchukua na kumuweka ndani ya safina pamoja naye.
But the dove found no rest for the sole of her foot, and she returned unto him to the ark, for the waters were on the face of the whole earth; and he put forth his hand, and took her, and brought her in unto him into the ark.
10 Akasubiri siku saba zingine akatuma tena njiwa kutoka kwenye safina.
And he stayed yet other seven days; and again he sent forth the dove out of the ark.
11 Njiwa akarudi kwake jioni. Tazama! katika mdomo wake kulikuwa na jani bichi la mzeituni lililochumwa. Kwa hiyo Nuhu akatambua kuwa maji yamekwisha zama chini ya nchi.
And the dove came in to him at eventide; and lo in her mouth an olive-leaf freshly plucked; so Noah knew that the waters were abated from off the earth.
12 Akasubiri siku saba zingine na akamtuma njiwa tena. Njiwa hakurudi kwake tena.
And he stayed yet other seven days; and sent forth the dove; and she returned not again unto him any more.
13 Ikawa kwamba katika mwaka wa mia sita na moja, katika mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi, maji yalikuwa yamekauka katika nchi. Nuhu akaondoa kifuniko cha safina, akatazama nje, na akaona kwamba, Tazama, uso wa nchi ulikuwa umekauka.
And it came to pass in the six hundred and first year, in the first month, the first day of the month, the waters were dried up from off the earth; and Noah removed the covering of the ark, and looked, and behold, the face of the ground was dried.
14 Katika mwezi wa pili, siku ya ishirini na saba ya mwezi, nchi ilikuwa imekauka.
And in the second month, on the seven and twentieth day of the month, was the earth dry.
15 Mungu akamwambia Nuhu,
And God spoke unto Noah, saying:
16 “Toka nje ya safina, wewe, mke wako, wanao wa kiume, na wake wa wanao pamoja nawe.
'Go forth from the ark, thou, and thy wife, and thy sons, and thy sons' wives with thee.
17 Wachukuwe utoke nje pamoja nao kila kiumbe hai chenye mwili ambacho kiko nawe - ndege, wanyama wa kufugwa, na kila kitambaacho ambacho hutambaa juu ya nchi - ili kwamba viweze kukua na kuwa na idadi kubwa zaidi ya viumbe hai katika nchi yote, kwa kuzaliana na kuongezeka juu ya nchi.”
Bring forth with thee every living thing that is with thee of all flesh, both fowl, and cattle, and every creeping thing that creepeth upon the earth; that they may swarm in the earth, and be fruitful, and multiply upon the earth.'
18 Kwa hiyo Nuhu akatoka nje pamoja na watoto wake wa kiume, mke wake, na wake wa wa wanawe pamoja naye.
And Noah went forth, and his sons, and his wife, and his sons' wives with him;
19 Kila kiumbe hai, kila kitambaacho, na kila ndege, na kila kiendacho juu ya nchi, kwa kabila zao, wakaiacha safina.
every beast, every creeping thing, and every fowl, whatsoever moveth upon the earth, after their families; went forth out of the ark.
20 Nuhu akajenga madhabahu kwa Yahwe. Akachukua baadhi ya wanyama walio safi na baadhi ya ndege walio safi, na kutoa sadaka ya kuteketezwa juu ya madhabahu.
And Noah builded an altar unto the LORD; and took of every clean beast, and of every clean fowl, and offered burnt-offerings on the altar.
21 Yahwe akanusa harufu nzuri ya kuridhisha na akasema moyoni mwake, “Sita laani tena ardhi kwa sababu ya mwanadamu, ingawa nia za mioyo yao ni mbaya tokea utoto. Wala sita haribu kilakitu chenye uhai, kama nilivyo fanya.
And the LORD smelled the sweet savour; and the LORD said in His heart: 'I will not again curse the ground any more for man's sake; for the imagination of man's heart is evil from his youth; neither will I again smite any more every thing living, as I have done.
22 Wakati nchi isaliapo, majira ya kupanda mbegu na mavuno, baridi na joto, kiangazi na majira ya baridi, mchana na usiku havitakoma.”
While the earth remaineth, seedtime and harvest, and cold and heat, and summer and winter, and day and night shall not cease.'

< Mwanzo 8 >

A Dove is Sent Forth from the Ark
A Dove is Sent Forth from the Ark