< Mwanzo 10 >

1 Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya wana wa Nuhu, ambao ni, Shemu, Hamu, na Yafethi. Wana wa kiume walizaliwa kwao baada ya gharika.
Now these are the generations of the sons of Noah: Shem, Ham, and Japheth; and unto them were sons born after the flood.
2 Wana wa Yafethi walikuwa Gomeri, Magogu, Madai, Yavani, Tubali, Masheki, na Tirasi.
The sons of Japheth: Gomer, and Magog, and Madai, and Javan, and Tubal, and Meshech, and Tiras.
3 Na wana wa Gomeri walikuwa Ashikenazi, Rifathi na Togama.
And the sons of Gomer: Ashkenaz, and Riphath, and Togarmah.
4 Wana wa Yavani walikuwa Elisha, Tarshishi, Kitimu, na Dodanimu.
And the sons of Javan: Elishah, and Tarshish, Kittim, and Dodanim.
5 Kutoka kwa hawa watu wa pwani waligawanyika na kwenda kwenye ardhi zao, kila mtu na lugha yake, kufuatana na koo zao, kwa mataifa yao.
Of these were the isles of the nations divided in their lands, every one after his tongue, after their families, in their nations.
6 Wana wa Hamu walikuwa Kushi, Misraimu, Putu, na Kanaani.
And the sons of Ham: Cush, and Mizraim, and Put, and Canaan.
7 Wana wa Kushi walikuwa Seba, Havila, Sabta, Raama, na Sabteka. Wana wa Raama walikuwa Sheba na Dedani.
And the sons of Cush: Seba, and Havilah, and Sabtah, and Raamah, and Sabteca; and the sons of Raamah: Sheba, and Dedan.
8 Kushi akamzaa Nimrodi, ambaye alikuwa hodari wa kwanza juu ya nchi.
And Cush begot Nimrod; he began to be a mighty one in the earth.
9 Alikuwa mwindaji mkuu mbele ya Yahwe. Hii ndiyo sababu hunenwa, “Kama Nimrod mwindaji mkuu mbele za Yahwe.”
He was a mighty hunter before the LORD; wherefore it is said: 'Like Nimrod a mighty hunter before the LORD.'
10 Miji ya kwanza ya ufalme wake ilikuwa Babeli, Ereku, Akadi na Kalne, katika ichi ya Shinari.
And the beginning of his kingdom was Babel, and Erech, and Accad, and Calneh, in the land of Shinar.
11 Kutoka katika nchi ile alikwenda Ashuru na akajenga Ninawi, Rehoboth- iri na Kala,
Out of that land went forth Asshur, and builded Nineveh, and Rehoboth-ir, and Calah,
12 na Raseni ambao ulikuwa kati ya Ninawi na Kala. Ulikuwa mji mkubwa.
and Resen between Nineveh and Calah — the same is the great city.
13 Misraimu akazaa Waludi, Waanami, Walehabi, na Wanaftuhi,
And Mizraim begot Ludim, and Anamim, and Lehabim, and Naphtuhim,
14 Wapathrusi na Wakasluhi ( ambao kwao Wafilisti walitokea), na Wakaftori.
and Pathrusim, and Casluhim — whence went forth the Philistines — and Caphtorim.
15 Kanaani akamzaa Sidono, mwanawe wa kwanza, na Hethi,
And Canaan begot Zidon his firstborn, and Heth;
16 pia na Myebusi, na Mwamori, Mgirgashi,
and the Jebusite, and the Amorite, and the Girgashite;
17 Mhivi, Mwarki, Msini,
and the Hivite, and the Arkite, and the Sinite;
18 Mwarvadi, Msemari, na Mhamathi. Baadaye koo za wakanaani zikasambaa.
and the Arvadite, and the Zemarite, and the Hamathite; and afterward were the families of the Canaanite spread abroad.
19 Mpaka wa Wakanaani ulianzia Sidoni, katika mwelekeo wa Gerari, hata Gaza, na kama kuelekea Sodoma, Gomora, Adma, na Seboimu hata Lasha.
And the border of the Canaanite was from Zidon, as thou goest toward Gerar, unto Gaza; as thou goest toward Sodom and Gomorrah and Admah and Zeboiim, unto Lasha.
20 Hawa walikuwa wana wa Ham, kwa koo zao, kwa lugha zao, katika ardhi zao na katika mataifa yao.
These are the sons of Ham, after their families, after their tongues, in their lands, in their nations.
21 Pia walizaliwa wana kwa Shemu, ndugu yake mkubwa wa Yafethi. Shemu pia alikuwa baba yao na watu wote wa Eberi.
And unto Shem, the father of all the children of Eber, the elder brother of Japheth, to him also were children born.
22 Wana wa Shemu walikuwa Elamu, Ashuru, Alfaksadi, Ludi, na Aramu.
The sons of Shem: Elam, and Asshur, and Arpachshad, and Lud, and Aram.
23 Wana wa Aramu walikuwa ni Usi, Huli, Getheri, na Mashi.
And the sons of Aram: Uz, and Hul, and Gether, and Mash.
24 Arfaksadi akamzaa Sela, na Sela akamzaa Eber.
And Arpachshad begot Shelah; and Shelah begot Eber.
25 Eberi akazaa wana wawili wa kiume. Jina la mmoja aliitwa Pelegi maana katika siku zake nchi iligawanyika. Jina la ndugu yake aliitwa Yoktani.
And unto Eber were born two sons; the name of the one was Peleg; for in his days was the earth divided; and his brother's name was Joktan.
26 Yoktani akamzaa Almodadi, Shelefu, Hasarmawethi, Yera,
And Joktan begot Almodad, and Sheleph, and Hazarmaveth, and Jerah;
27 Hadoram, Uzali, Dikla,
and Hadoram, and Uzal, and Diklah;
28 Obali, Abimaeli, Sheba,
and Obal, and Abimael, and Sheba;
29 Ofiri, Havila, na Yobabi. Hawa wote walikuwa wana wa Yoktani.
and Ophir, and Havilah, and Jobab; all these were the sons of Joktan.
30 Mpaka wao ulikuwa unaanzia Mesha, hadi Sefari, mlima wa mashariki.
And their dwelling was from Mesha, as thou goest toward Sephar, unto the mountain of the east.
31 Hawa walikuwa wana wa Shemu, kulingana na koo zao na lugha zao, katika ardhi zao kulingana na mataifa yao.
These are the sons of Shem, after their families, after their tongues, in their lands, after their nations.
32 Hizi zilikuwa koo za wana wa Nuhu, kulingana na vizazi vyao, kwa mataifa yao. Kutokea kwa hawa mataifa yaligawanyika na kwenda juu ya nchi baada ya gharika.
These are the families of the sons of Noah, after their generations, in their nations; and of these were the nations divided in the earth after the flood.

< Mwanzo 10 >