< Mwanzo 11 >

1 Sasa nchi yote ilikuwa inatumia lugha moja na ilikua na usemi mmoja.
And the whole earth was of one language and of one speech.
2 Ikawa waliposafiri upande wa mashariki, wakaona eneo tambarare katika nchi ya Shinari na wakakaa pale.
And it came to pass, as they journeyed east, that they found a plain in the land of Shinar; and they dwelt there.
3 Wakasemezana, “Haya njoni, tufanye matofari na tuyachome kikamilifu.” Walikuwa na matofari badala ya mawe na lami kama chokaa.
And they said one to another: 'Come, let us make brick, and burn them thoroughly.' And they had brick for stone, and slime had they for mortar.
4 Wakasema, “njoni, na tujenge mji sisi wenyewe na mnara ambao kilele chake kitafika angani, na tujifanyie jina. Kama hatutafanya, basi tutatawanyika katika uso wa nchi yote.”
And they said: 'Come, let us build us a city, and a tower, with its top in heaven, and let us make us a name; lest we be scattered abroad upon the face of the whole earth.'
5 Kwa hiyo Yahwe akashuka kuona mji na mnara ambao wazao wa Ibrahimu walikuwa wamejenga.
And the LORD came down to see the city and the tower, which the children of men builded.
6 Yahwe akasema, “Tazama, watu hawa ni taifa moja na lugha moja, na wameanza kufanya hivi! Hivikaribuni halitashindikana jambo watakalo kusudia kulifanya.
And the LORD said: 'Behold, they are one people, and they have all one language; and this is what they begin to do; and now nothing will be withholden from them, which they purpose to do.
7 Njoni, tushuke na tuvuruge lugha yao pale, ili kwamba wasielewane.”
Come, let us go down, and there confound their language, that they may not understand one another's speech.'
8 Kwa hiyo Yahwe akawatawanya kutoka pale kwenda pande zote za uso wa nchi na wakaacha kujenga mji.
So the LORD scattered them abroad from thence upon the face of all the earth; and they left off to build the city.
9 Kwa hiyo, jina lake ukaitwa Babeli, kwa sababu hapo Yahwe alivuruga lugha ya nchi yote na tangu pale Yahwe akawatawanya ng'ambo juu ya uso wa nchi yote.
Therefore was the name of it called Babel; because the LORD did there confound the language of all the earth; and from thence did the LORD scatter them abroad upon the face of all the earth.
10 Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Shemu. Shemu alikuwa na umri wa miaka mia moja, na akamzaa Alfaksadi miaka miwili baada ya gharika.
These are the generations of Shem. Shem was a hundred years old, and begot Arpachshad two years after the flood.
11 Shemu akaishi miaka miatano baada ya kumzaa Alfaksadi. Pia akazaa wana wengine wa kiume na wa kike.
And Shem lived after he begot Arpachshad five hundred years, and begot sons and daughters.
12 Wakati Alfaksadi alipokuwa ameishi miaka thelathini na mitano akamzaa Shela.
And Arpachshad lived five and thirty years, and begot Shelah.
13 Alfaksadi aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Shela. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
And Arpachshad lived after he begot Shelah four hundred and three years, and begot sons and daughters.
14 Wakati Shela alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Eberi.
And Shelah lived thirty years, and begot Eber.
15 Shela aliishi miaka 403 baada ya kumzaa Eberi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
And Shelah lived after he begot Eber four hundred and three years, and begot sons and daughters.
16 Wakati Eberi alipokuwa ameishi miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
And Eber lived four and thirty years, and begot Peleg.
17 Eberi aliishi miaka 430 baada ya kumzaa Pelegi. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
And Eber lived after he begot Peleg four hundred and thirty years, and begot sons and daughters.
18 Wakati Pelegi alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Reu.
And Peleg lived thirty years, and begot Reu.
19 Pelegi aliishi miaka 209 baada ya kumza a Reu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
And Peleg lived after he begot Reu two hundred and nine years, and begot sons and daughters.
20 Wakati Reu alipokuwa ameishi miaka thelathini na miwili, alimzaa Serugi.
And Reu lived two and thirty years, and begot Serug.
21 Reu aliishi miaka207 baada ya kumzaa Seregu. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
And Reu lived after he begot Serug two hundred and seven years, and begot sons and daughters.
22 Wakati Seregu alipokuwa ameishi miaka thelathini, akamzaa Nahori.
And Serug lived thirty years, and begot Nahor.
23 Seregu aliishi miaka mia mbili baada ya kumzaa Nahori. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
And Serug lived after he begot Nahor two hundred years, and begot sons and daughters.
24 Wakati Nahori alipokuwa ameishi miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
And Nahor lived nine and twenty years, and begot Terah.
25 Nahori aliishi mika 119 baada ya kumzaa Tera. Akawazaa pia wana wengine wa kiume na wa kike.
And Nahor lived after he begot Terah a hundred and nineteen years, and begot sons and daughters.
26 Baada ya Tera kuishi miaka sabini, akamzaa Abram, Nahori, na Haran.
And Terah lived seventy years, and begot Abram, Nahor, and Haran.
27 Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Tera. Tera alimzaa Abram, Nahori, na Harani, na Harani akamzaa Lutu.
Now these are the generations of Terah. Terah begot Abram, Nahor, and Haran; and Haran begot Lot.
28 Harani akafa machoni pa baba yake Tera katika nchi aliyozaliwa, katika Ur wa Wakaldayo.
And Haran died in the presence of his father Terah in the land of his nativity, in Ur of the Chaldees.
29 Abram na Nahori wakajitwalia wake. Mke wa Abram aliitwa Sarai na mke wa Nahori aliitwa Milka, binti wa Harani, aliyekuwa baba wa Milka na Iska.
And Abram and Nahor took them wives: the name of Abram's wife was Sarai; and the name of Nahor's wife, Milcah, the daughter of Haran, the father of Milcah, and the father of Iscah.
30 Sasa Sarai alikuwa Tasa; hakuwa na mtoto.
And Sarai was barren; she had no child.
31 Tera akamtwaa Abram mwanawe, Lutu mwana wa mwanawe Harani, na Sarai mkwewe, mke wa mwanawe Abram, na kwa pamoja wakatoka Ur wa Wakaldayo, kwenda katika nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani wakakaa pale.
And Terah took Abram his son, and Lot the son of Haran, his son's son, and Sarai his daughter-in-law, his son Abram's wife; and they went forth with them from Ur of the Chaldees, to go into the land of Canaan; and they came unto Haran, and dwelt there.
32 Tera akaishi miaka 205 kisha akafa hapao Harani.
And the days of Terah were two hundred and five years; and Terah died in Haran.

< Mwanzo 11 >